YESU NI JIBU

Jumamosi, 11 Julai 2015

YALIYOJIRI DODOMA KATIKA UCHAGUZI WA KUMTEUA MTU AMBAYE ATAPEPERUSHA BENDERA YA CCM KATIKA KUWANIA URAIS.

Wapambe wa Mbunge  wa Monduli Edward Lowassa  wamefanya maandamano makubwa nje ya ofisi za CCM, makao makuu ya CCM wakipinga Mbunge huyo kuchujwa katika tano bora.

Katibu wa Siasa Itikadi na Uenezi Nape Nnauye alithibitisha Dk Asha Rose Migoro, Dk Pombe John Magufuli, Benard Membe, Januari Makamba na Balozi Amina Salum Alli kupenya katika tano bora kati ya wagombea 38 waliojitokeza kuwania nafasi ya kuteuliwa na chama hicho kugombea urais.

Wapambe hao walisikika wakiimba nyimbo mbalimbali za kukiponda chama cha Mapinduzi kwa madai kuwa chama hicho sio cha kindugu na  pia sio cha kifalme.

Wachambuzi wa mambo ya siasa wanasema hali si shwari mkoani Dodoma ambapo sintofahamu imetawala kuhusiana na Edward Lowassa kukatwa.

Bado haijulikana nini hatma ya kikao cha Halmashauri Kuu kinachoendelea kwa kuwa wajumbe wengi wanapinga Lowassa kuchujwa.

Wajumbe hao waliimba nyimbo ya kuonesha kuwa na imani na Lowassa, wakati Rais Jakaya Kikwete na marais wastaafu wakiingia ukumbini.

“Tuna imani na Lowassa, oyaa, oyaa, oyaa, Lowassa oyee, oyee…oyee…oyee…oyee oyee Lowassa, Lowassa safi, safi……”


Rais Kikwete na viongozi wengine walijikuta katika mazingira yaliyowalazimisha kuimba wimbo huo, tofauti na matarajio yao.  

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni