Kauli hiyo imetolewa na askofu wa huduma ya New life
Deliverence Church kutoka Uganda nabii Joseph Kabuye jijini Dar es Salaam
katika hafla ya kuwaweka wakfu wachungaji wa huduma ya City Havesty International Church na kuelezea uwepo wa nguvu za Mungu katika maisha ya kila mwamini ndani ya kanisa.
Aidha askofu kabuye alisema kuwa katika shamba la Bwana mavuno ni mengi lakini
watendakazi ni wachache hivyo ni vyema kila mwamini ajitolee kufanya kazi ya Mungu kwa
wakati wote na kuongeza kuwa Mungu ni moto na hivyo waumini wakimtafuta kwa juhudi
ataonekana na kuwasaidia katika maisha yao na zaidi huwaweka huru ndani ya
maisha yao ya kila siku.
Akinukuu kitabu cha kutoka 3:1-4 alisema MUNGU alitokewa Musa
katika kichaka ambacho hakiteketi huku kikiwaka na hapo alisikia sauti ya Bwana
MUNGU ikimwita alipogeuka na kujisemea nitaangali nione maono haya makubwa
ndipo Mungu alimwita hivyo ni dhairi kuwa yeye ni moto.
Akielezea umuhimu wa siku hiyo ya kuwaweka wakfu
wachungaji mchungaji kiongozi na mwwasisi wa huduma ya City Haversty
International Church hapa Tanzania Dr Livingstone Banjagala alisema kuwa huduma
hiyo imesambaa katika mataifa mbalimbali hivyo watendakazi ni wachache na ndiyo
maana wameamua kuwaweka wakfu wachumbaji hao zaidi ya sita katika ibada hiyo ya
jumapili.
Hata hivyo aliongeza kuwa mpaka sasa huduma hiyo hufanya
jitihada mbalimbali pamoja na kuwasaidia watu wenye mahitaji maalum pamoja na
kuwasaidia watoto wanaoishi katika mazingira magumu,na pia wanaweka mikakati ya
kujenga kituo cha watoto yatima na wazee kwa lengo la kuwasaidia watu hao ambao
wengi jamii imewatenga.
“mpaka sasa tuna huduma katika mataifa mbalimbali hivyo tuna
kila sababu ya kuhakikisha kuwa tunawafikia watu wengi kwa wakati kwa lengo ni
kuwafikishia neno la MUNU ili wafunguliwe katika matatizo yao”alisema Dr
Banjagala.Mch. Dr livingstone kushoto amevaa joho akiwa na mke wake katikaibada ya kuweka wakfu wachungaji sita wa huduma hiyo.
Hawa ndiyo wachungaji ambao wamewekwa wakfu.
Kulia ni nabii Joseph Kabuye na katikati ni apostle Dr livingstone kushoto i mtafsiri wake.
Nabii Kabuye akiwaombea waumini katika ibada ya kuwekwa wakfu wachungaji.