YESU NI JIBU

Jumanne, 28 Oktoba 2014

HOJA YA ASKOFU SYLVESTER GAMANYWA JUU YA ONGEZEKO LA IMANI ZA UCHAWI MAKANISANI TANZANIA:

Katika toleo lililopita tulianza makala na Marejeo ya athari za imani za uchawi makanisa; kisha tukagusia kwa ufupi historia ya uchawi ambao mwasisi wake anasadikiwa kuwa ni Nimrodi; na tukikomea kwenye kipengele kinachohusu ”Nguvu za uchawi na uganga dhidi ya Musa” ambapo tulishuhudia jinsi wachawi wa Farao walivyopambana na Musa kwa kuigiza miujiza aliokuwa akiifanya Musa. Leo tunaendelea na uchambuzi huo:



Ukomo wa nguvu za uchawi

katika kuigiza miujiza ya Musa 
“BWANA akamwambia Musa, Mwambie Haruni, Nyosha fimbo yako, ukayapige mavumbi ya nchi, ili kwamba yawe chawa katika nchi yote ya Misri.  Nao wakafanya; Haruni akaunyosha mkono wake na fimbo yake, na kuyapiga mavumbi ya nchi, nayo yakawa chawa juu ya wanadamu na juu ya wanyama; mavumbi yote ya nchi yakawa ni chawa katika nchi yote ya Misri.  Hao waganga nao wakafanya mfano wa hayo kwa uganga wao, ili kwamba walete chawa, lakini wasiweze; nako kulikuwa na chawa juu ya wanadamu, na juu ya wanyama.  Ndipo wale waganga wakamwambia Farao, Jambo hili ni chanda cha Mungu; na moyo wake Farao ukawa mgumu asiwasikize; vile vile kama BWANA alivyonena.” (KUT. 8:16-19)

 Maandiko tuliyonukuu hapa juu, yanadhihirisha jinsi ambavyo hapo mwanzo wachawi wa Farao walijaribu kuigiza miujiza ya Musa ili kushindana naye. Na ukweli wa macho walionekana kufanikiwa na kumpa Farao Kiburi. Hali ingeliweza kumchanganya Musa, kuona wachawi nao wanafanya miujiza ile ile anayoifanya. Lakini Musa hakuteteleka kiimani, badala yake alimwamini Mungu kujitetea kwa kudhihirisha uweza wake dhidi ya nguvu za wachawi wa Farao. Hatimaye, tunashuhudia katika maandiko wachawi walikwama kuigiza “muujiza wa kuleta chawa”. Tunasoma kwamba: “….Hao waganga nao wakafanya mfano wa hayo kwa uganga wao, ili kwamba walete chawa, lakini wasiweze;….” Baada ya kushindwa ilibidi wakiri waziwazi kwa Farao wakisema kwamba: ”jambo hili ni chanda cha Mungu…”
Kana kwamba hii haikutosha, miujiza mingine iiliyofuatia ya mapigo ya Musa dhidi ya Farao; hata waganga wake hawakusalimika. Tunajionea kupitia maandiko kuhusu muujiza wa pigo la majipu ambapo tunasoma: “Basi wakatwaa majivu ya tanuu na kusimama mbele ya Farao; na Musa akayarusha juu mbinguni nayo yakawa majipu yenye kufura na kutumbuka juu ya wanadamu na juu ya wanyama. Nao wale waganga hawakuweza kusimama mbele ya Musa kwa sababu ya hayo majipu, kwa maana hao waganga walikuwa na majipu, na Wamisri wote walikuwa nayo.” (Kut.9:10-11)



Mapambano kati ya Simoni mchawi

na Filipo aliyejaa Roho Mtakatifu



Injili iliyohubiriwa na mitume na wainjilisti wa kanisa la kwanza nayo pia iliambatana na ushindani dhidi ya nguvu za uchawi. Ili kuupata ushahidi wa haya nisemayo, hebu twende kwenye kitabu cha Matendo ya Mitume na kuangalia kisa cha mchawi aliyekua maarufu sana katika jimbo la Wasamaria:



“Na mtu mmoja, jina lake Simoni, hapo kwanza alikuwa akifanya uchawi katika mji ule, akiwashangaza watu wa taifa la Wasamaria, akisema ya kuwa yeye ni mtu mkubwa.  Wote wakamsikiliza tangu mdogo hata mkubwa, wakisema, Mtu huyu ni uweza wa Mungu, ule Mkuu.  Wakamsikiliza, kwa maana amewashangaza muda mwingi kwa uchawi wake.  Lakini walipomwamini Filipo, akizihubiri habari njema za ufalme wa Mungu, na jina lake Yesu Kristo, wakabatizwa, wanaume na wanawake.  Na yeye Simoni mwenyewe aliamini akabatizwa, akashikamana na Filipo; akashangaa alipoziona ishara na miujiza mikubwa inayotendeka. (MDO 8:9-13)

Kwa mujibu wa maandiko tuliyosoma tunathibitisha kwamba, mchawi Simoni aliwashangaza Wasamaria kwa muda mwingi kwa uchawi wake; tena akasifiwa sana kwamba alikuwa na “uweza mkuu wa Mungu”. Na kwa kuwa hapakuwepo mshindani wake, aliteka usikivu wa watu wote kuanzia mdogo hadi mkubwa. Bila shaka alifanya utapeli huu kwa miaka mingi.
Lakini wakati muafaka ulifika dhidi ya Mchawi Simoni kupata changamoto. Tumesoma habari za Mwinjilisti Filipo ambaye aliingia Samaria na kukuta Simoni akiendelea na mazingaombwe yake. Filipo hakutaka kushindana na Simoni ana kwa ana kwa kumkemea na kumgombeza kwa matamko ya matishio ya maneno. Filipo aliamua kuihubiri Injili ya Kristo na kumruhusu Roho Mtakatifu afanye kazi yake.
Tumeshuhudia jinsi ambavyo Filipo alitumiwa kufanya miujiza iliyovunja rekodi ya uchawi wa Simoni, na wateja wote wa Simoni walimwamini Yesu Kristo aliyehubiriwa na Filipo wakafunguliwa katika vifungo vya pepo na kuponywa magonjwa na kuponywa ulemavu wa viungo vya mwili. Hatimaye tumeshuhudia mchawi SImoni naye “akibwaga manyanga” yake na kujisamilisha kwa nguvu za Roho Mtakatifu aliyekuwa naye Filipo.


Paulo alivyoshindana

 na mchawi Bar-Yesu

 Walipokwisha kupita katikati ya kisiwa chote mpaka Pafo, wakaona mtu mmoja, mchawi, nabii wa uongo, Myahudi jina lake Bar-Yesu;  mtu huyu alikuwa pamoja na liwali Sergio Paulo, mtu mwenye akili. Yeye liwali akawaita Barnaba na Sauli waje kwake, akataka kulisikia neno la Mungu.  Lakini Elima, yule mchawi (maana ndiyo tafsiri ya jina lake), akashindana nao, akitaka kumtia yule liwali moyo wa kuiacha ile imani.  Lakini Sauli, ambaye ndiye Paulo, akijaa Roho Mtakatifu, akamkazia macho,  akasema, Ewe mwenye kujaa hila na uovu wote, mwana wa Ibilisi, adui wa haki yote, huachi kuzipotoa njia za Bwana zilizonyoka?  Basi, angalia, mkono wa Bwana u juu yako, nawe utakuwa kipofu, usilione jua kwa muda. Mara kiwi kikamwangukia na giza, akazunguka-zunguka na kumtafuta mtu wa kumshika mkono na kumwongoza.  Ndipo yule liwali, alipoyaona yaliyotendeka, akaamini, akiyastaajabia mafundisho ya Bwana. (MDO 13:6-12)


Kwa mujibu wa maandiko haya, tunashuhudia jinsi ambavyo uchawi unaweza kutafsiriwa kuwa ni huduma ya kinabii. Kwa sababu ya miujiza ya kimazingaombwe inayofanywa na wachawi/waganga, watu wengine hudanganyika kwa kudhani kuwa hizo ni nguvu za Mungu, hasa pale ambapo mchawi husika anapoamua kutumia mwavuli wa dini kama kinga ya kuficha uchawi wake. Lakini, pamoja na hao wachawi, kujificha chini ya mwavuli wa dini; hawawezi kushindana na utendaji halisi wa nguvu za Roho Mtakatifu! Tunamwona Paulo akitumia nguvu za Roho Mtakatifu kumdhibiti Bar-Yesu!

  Itaendelea toleo lijalo
TOA MAONI YAKO HAPA CHINI.

UZINDUZI WA ALBUMU YA YU MWEMA YAKE MWIMBAJI IBRAHIMU SANGA KATIKA UKUMBI WA HOTELI YA LANDMARK JIJINI DAR ES SALAAM:

Uzinduzi wa albamu ya mwimbaji wa nyimbo za injili Ibrahimu Sanga Imefana sana kiasi kwamba waliofika akiongozwa na mgeni rasmi wamechangia katika huduma ya mwimbaji huyo huku waimbaji wenzake wa injili wakimsindikiza katika uzinduzi huo.
Mgeni rasmi katika uzinduzi huo ni Naibu waziri wa fedha mbunge mheshimiwa Mwigulu Nchemba ambaye amewaongoza mamia ya watu walofika kitiaa uzinduzi huo hivi karibuni katika ukumbi wa hoteli ya Landmark iliyopo Ubungo jijini la Dar es salaam.

 
Naibu waziri wa fedha mheshimiwa Mwigulu Nchemba mwenye suti nyeusi kushoto akisalimiana na mwimbaji Ibrahimu Sanga kulia mwenye skafu ya bendera ya taifa ni mwimbaji Joshua Makondeko.



 Hapo sasa mwimbaji Ibrahimu Sanga na Timu yake wakiwajibika jukwaani wakati wa uzinduzi wa albamu yake Yu ni mwema  ndani ya ukumbi wa Landmark.

Mwimbaji Bitres Mwaipaja hakuwa nyuma katika kutumbuiza kwa wimbo wake maarufu kama KUMBE NI KWA NEEEMA TU.
Upendo nkone akiwa kwenye pozii huku Mess Jacob Chengula akitabasamu.
waimbaji akiongozwa na Upendo Nkone wakitazama kwa makini jukwaani kuangalia kinachoendelea.

KIU YA NENO YAAONGEZEKA HUKU NAYO MAASI YAKIONGEZEKA MTEULE KAA TAYASI SIKU SI MBALI:

 Kwa sasa katika kila kona ya dunia kiu ya neno la MUNGU inaongezeka huko nayo maasi yakizidi kupanda kwa kasi kiasi kwamba wanadamu wanauana hata bila sababu za msingi kiukweli inasikitisha sana ,ni kazi ya wateule kufanya kazi kwa bidii kabla jioni haijaingia.
Ndugu msomaji wa blog hii leo tunaangazia katika mkutano wa injili ambao umefanika kuko Ifakara Morogoro ulioendeshwa na Daktari Mtume Dustani Maboya wa kanisa la Calvary Assemblie ambapo  wananchi wa mji wa Ifakara wanasema haijawahii tokea maelfu na maelfu kufika katika viwanjani kusikiliza neno la Mungu na kumpokea Yesu kama bwana na Mwokzi wa maisha yao huku wengine wakiponywa magonjwa na kufunguliwa katiaka nguvu za giza na mateso mbalimbali.



 DR mtume Maboya akihubiri neno katika mkutano huo wa injili.


Mamia ya wagonjwa walifika kufunguliwa na ililazimu kuwepo na ibada tatu kwa siku toka watumishi wa Mungu walipowasili Ifakala,hapa zoezi la maombezi limeanza.



 Dr Mtume Maboya akiimba jukwaani na mwimbaji wa nyimbo za injili Mess Jacob Chengula akiwa na waimbaji wenzake.
 




 Mess Chengula akimiliki jukwaa kwa makini na kibao cha wimbo wake maaru kwa jina Mungu wetu Habadiliki.




 YESU afanya makuu katika mkutano wa Mtume Maboya ifakala ambapo watu waliomkubali Bwana Yesu kama bwana na Mwokozi wa maisha yao kun'gania wabatize wenyewe ambapo mtumishi wa Mungu alilazimika kuingia Mto kilombelo na kuwabatiza mamia ya watu.





 Zoezi la kubatiza ndani ya mto Kilombero   Dr.apostel Dustani Maboya akianza kuwabatiza watu walioamua kubatizwa kama unavyooona msomaji.
Toa maoni yako.

Ijumaa, 24 Oktoba 2014

HOFU,WASIWASI MASWALI JUU YA MCHEZAJI PETER BIAKSANGZUALA KUFARIKI DUNIA BAADA KUUMIA VIBAYA AKISHANGILIA BAO ALILOFUNGA:

Ligi ya Mizoram ikimuombolea mchezaji Peter Biaksangzuala 
 Unaweza kuwa na maswali mengi ,mshangao zaidi kuwaza sana kuwa inakuwaje,na ni kitu gani kinasababisha mchezaji kufa akiwa uwanjani ama akishangilia bao ambalo amefunga au lilofungwa na mwenzake.
Hivi karibu habari za kimichezo ambayo imetawala vyombo vya habari mbalimbali duniani ya mchezaji wa soka nchini India Peter Biaksangzuala kufariki baada kukimbizwa hospitalini kwa matibabu baasa ya kuanguka vibaya uwanjani akishangilia bao lake.
Kiukweli tunajifunza mengi kutokana na kifo cha mchezaji huyo kwani kuna mbinu za adui ya kuangamiza maisha ya wanadamu hasa wale maarufu kwani ukibahatika kupata kitabu kilichoandikwa na Emmanuel Agyarko kilichotafsiriwa na mchungaji Godwin Gunewe ukurasa wa kumi na tatu utajua kinachoendelea.
Mnamo mwaka 2003 kwa mujibu wa kitabu hicho mchezaji maarufu ambaye alijulikana kwa jina la Marc-Vivian Foe kutoka nchi ya Cameroon alifariki dunia uwanjani akiwa Ufaransa.
Kuna baadhi ya watu maarufu kujiunga na imani nyingine ili kupata nguvu na uwezo wa kuwa maarufu na wengine wanashindwa kutimiza masharti ambayo wamewekeana.
Ndugu msomaji ni shauku ya mwandishi na msimamizi wa blog hii kuwa makini sana na kusoma neno la Mungu(BIBLIA) ambayo ndiyo dira kamili katika maisha ya kiroho,na pia kuwasihi wacheza mpira na mashabiki wao kutafakari kwa makini.
Jitahidi kutafuta vitabu ambavyo vitakusaidia kujifunza yale yanayompendeza Mungu.
sasa endelea kupata kisa kilichotokea katika tibu Bethlehem Vengthlang FC.
 Mchezaji wa soka nchini India, Peter Biaksangzuala amefariki kutokana na majeraha aliyoyapata baada ya kuanguka vibaya uwanjani akisherehekea bao lake.
Mchezaji huyo alikuwa na umri wa miaka 23 na alijeruhi uti wake wa mgongo baada ya kupiga pindu uwanjani akisherehekea bao lake la kusawazisha kwa timu yake Bethlehem Vengthlang FC dhidi ya Chanmari West FC.
Biaksangzuala alikimbizwa hospitalini na kufanyiwa upasuaji lakini baadaye alifariki.
Taarifa kutoka kwa ligi hiyo kupitia kwa mtandao wa Facebook, ilisema : ''imekuwa siku yenye huzuni mkubwa kwa ligi ya Mizoram na kifo cha mchezaji wetu kimetushtua sana pamoja na wachezaji wenzake, wachezaji wa soka na mashabiki wa Mizoram. ''
"Peter alikuwa mchezaji mzuri na milizni mzuri sana, na pia alikuwa mchapa kazi.''
 Toa maoni  yako.

Jumapili, 19 Oktoba 2014

BAADA YA KUKAA KIMYA KWA MDA MREFU KWENYE UIMBAJI ANAKUJA KWA KISHINDO AKIWA NA UJUMBE WA NINA NDOTO YANGU SI MWINGINE MCHUNGAJI MWANSASU:

Mchungaji kiongozi wa huduma ya Hossana Life Mission Mchungaji Efrahim Mwansasu afunguka na kuweka wazi kwanini amekuwa kimya kwa mda mrefu,na sasa arudi kwa kishindo.
 Mchungaji Efrahim Mwansasu akiimba.
Watu hujiuliza na bila kupata majibu na kusema utawezaje kufanya mambo mawili kwa wakati mmoja ,ila wanashindwa kuelewa kanakwamba unapokuwa mchungaji lazima utafundisha na unapofundisha ili mtu akuelewe lazima uwe mbunifu na namna ya kutochosha waumini wako .

Mchungaji Mwansasu ana wito na kazi ya mungu hivyo ni lazima atumie kipaji chake ya kipekee kipaji cha uimbaji na anakitumia ipasavyo awapo madhabauni na baada ya kuona anakipawa cha uchungaji akaona si vyema kuacha kufanya kazi ya Mungu na awapo popote pale aachi kuimba na pia kuwa mchungaji ni vitu ambavyo mtumishi wa Mungu ni wajibu kutumia vitu hivyo kwa wakati mmoja .
 Aidha ieleweke wazi sio kambwa nipo kimya huwa kila muda na siku haipiti bila kuimba,na uimbaji wangu kutoa albamu pia sio  jambo la kuamka na kukurupuka na kukimbili studio ni jambo la kusema na Mungu nifanye nini katika hiki kipaji ulichonipa kwa ajili ya nchi yangu na mkoa wangu hata katika mataifa mengine.
Ni jambo la  kila mwimbaji kukaa na kutafakari unapotoka na unapokwenda na tujiulize kwa nini nyimbo za zamani hazipitwi na wakati za injili  na kizazi hiki nicha kumuomba Mungu sana kwani tumekuwa tukiimba bila kujua nini tunakifanya waimbaji wa injili tumejisahau na kusema ni utandawazi kumbe sivyo watu wamungu tunapaswa kuwa ,hivyo tuwe na upendo na kurudi chini na kumtumikia Mungu tusitafute pesa kwa kupoteza jamii katika maadili ya kumcha mungu ,bali tutafute kwanza ufalme na kumjengea Mungu.

Na safari hii nakuja kivingine huwa nina ndoto yangu ya maisha na ndiyo maana Mungu ananitunza, nyimbo zangu natamani sana Mungu anisaidie kwa kuangali na kuzitafakari ukisikiliza upate ujumbe na ni wakila mmoja wetu hivyo yakupasa kufanyia kazi.

Kipawa  ch uimbaji na uchungaji namshukuru Mungu kwa kutumia roho mtakatifu na kwa kunitumia,
 Mwaka 1998,Albamu yangu ya kwanza ilifahamika kwa jina la Tutatesa milele ikiwa na ujumbe wa kuwainua wacha Mungu na kuwataadharisha wanaopenda dunia waache na kumrudia mungu ikiwa na nyimbo nane .

Mwaka 2001 Albamu ya pili ,Umepoteza namba,inamaanisha mtu unaemtafuta Mume wa mtu au mke wa Mtu aache mara moja

Mwaka 2005 Albamu ya tatu Msigombane,Niliona ni kama kuna wakati tutagombana Viongozi wa dini katika huduma na katika dini ,upendo utatoweka katika madhehebu mbali mbali na viongoza wa dini na yametimia katika Mwaka 2013 Hadi sasa mfano makanisa kuchomwa moto mashehe kugombana amani inatoweka.

Mwaka 2010 Wosia wa baba .ninamaanisha kila unapoongea na  mzazi iwe mzazi wako au aliyekuzidi umri lazima anapokupa wosia usiupuuzie mzazi maadili yake huwa yanatokea.

Na safari hii kweli linatimia ukimuomba mungu Mwaka huu ninazindua Albamu yangu ya tano inakwenda kwa jina la Nina ndoto yangu Mabano I have a dream,namaanisha kila mtu ana ndoto yake duniani na zipo ndoto ndogo, ya kati, na kubwa,lakini wenye ndoto kubwa  wanamambo makubwa,na madogo ni madogo,hivyo mwenye ndoto lazima awe na maadui.
 Kipawa changu cha kuimba ni kutokana na mazingira ninayopita na Mungu hunitumia kwa kupitia uwezo wa Roho mtakatifu na hadi mimi mwenyewe najishangaa vinatoka wapi na mwisho wa siku vinatokea.

Kufanya mambo mawili kwa wakati mmoja ,uimbaji na mchungaji ni utaratibu unajiwekea ratiba yako tena unaweza kufanya zaidi kutokana na wewe mwenyewe unavyojiwekea utaratibu wako wa kazi ,na pia kuimba na kuubiri ni vitu vinavyoenda sambamba.

Jumatatu, 13 Oktoba 2014

KONGAMANO LA WWI NA MKUTANO WA INJILI LIMEFANA SANA KATIKA VIWANJA VYA SABASABA WILAYANI TEMEKE JIJINI DAR ES SALAAM.

Kongamano ambalo limeandaliwa na chama cha Wanawake watumishi WWI jimbo la Temeke ambalo limefanyika katika viwanja vya sabasaba maarufu kama viwanja vya mwalimu Julias Kambarege Nyerere limefana sambamba na mkutano wa injili ambao umeendelea katika viwanja hivyo na maaskofu,wachungaji mbalimbali walihudhuria waumini wa madhehebu na dini tofauti pamoja na watu wenye mahitaji mbalimbali.
Konganano hilo na mkutano ulipambwa na waimbaji mbalimbali ambao walifika kumpa Mungu sifa na utukufu na watu wengi wamefunguliwa na kuponywa magonjwa na matatizo mbalimbali.
 Askoku mkuu wa jimbo la Temeke EAGT,mwenyekiti wa Jumuiya ya Makanisa ya Kipentekoste Tanzania(CPCT) na ni mchungaji kiongozi wa kanisa la EAGT Mito ya Baraka Askofu Bruno Mwakibolwa.

 Askofu Mwakibolwa anakabithiwa zawadi na mkurugenzi wa WWI taifa EAGT kwenye mkutano wa Injili katika viwanja vya sabasaba


 Picha ya pamoja kati viongozi wa WWI taifa na jimbo la Temeke na baadhi ya viongozi wa jimbo hilo.
 Mchungaji wa kanisa la EAGT city Center mchungaji Florian Katunzi akifuatilia kwa makini mafundisho katika kongamano la wamama jimbo la temeke.

 Mchungaji Katunzi akipokea mkono wa pongezi na zawadi ambaye anakabidhiwa na mkurungezi wa WWI taifa akiwa na mkrugenzi WWI jimbo la Temeke mama Rachael Katunzi anayeshika zawadi.

  Viongozi wa WWI jimbo la temeke wakiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa Taifa WWI.

 Kutoka kulia ni mkurugezi wa WWI jimbo la Temeke mama Rachael Katunzi,wa pili ni mrs Paul Chisolo makamu mkurugenzi,wa tatu ni Mrs Kazoka ambaye ni katibu na wa nne ni mhasibu Carolin Kilango.



 


 Wanachama wa WWI jimbo la Temeke wakiwa katika picha ya pamoja na viongozi wao wa jimbo hilo







Hapa sasa ni mwendo wa kupongezana kati ya wanachama wa WWI na viongozi wao katika viwanja vya Sabasaba wilayani Temeke Jijini Dar es salaam.
 Mkurugenzi wa WWI jimbo la Temeke mama Rachael Katunzi akisisitiza jambo katika kongamano la wanawake

Makamu mkurugenzi mrs Paul Chisolo akiwasalimia wajumbe waliofika katika kongamano.
 Katibu Mrs Kazoka akisema jambo kwa wanachama wake ambao walihudhuria kongamano.
 Mhasibu Carolin Kilango hakuwa nyuma kuwasalimia wajumbe akiwa na makamu mkurugenzi.

 Askofu Mwakibolwa wa kwanza kulia kwenye mkutano wa injili sabasaba Temeke.









 Mchungaji wa kanisa la EAGT City Center akiwaombea wakina mama ambao walihudhuria kongamano la wanawake wa Injili jimbo la Temeke.
 Kundi la kusifu na kuzunguka uwanjali wakiwa na vibendera.
 Mwimbaji Jacob Mess Chengula akiwajibika katika  mkutano wa injili Temeke.


 Mwimbaji Solomo Mkubwa kutoka Nairobi Kenya akihudumu katika mkutano maarufu kwa wimbo wake utukufu apewe Mungu.

 Martha Mwaipaya Akiwa na mdogo wake Betris Mwaipaya wakiwajibika katika mkutano huko nyuma mchungaji akionekana akifuatilia kwa makini

 Kiukweli waimbaji walikuwa wengi sana hapa naye yupo Ibrahim Sanga na timu yake wakiwajibika.

 Mwimbaji kutoka Mbeya Emanuel Mgogo maarufu kwa wimbo wake msikilize Mungu akiwa na Bonny Mwaitege. 

 Bony mwaitege kulia na katikati ni Upendo Nkone na kushoto ni Rebeca Magaba.

Bony Mwaitege na vijana wake wakiwa jukwaani.




Mtangazaji wa WAPO Radio Sailas Mbise akiwajibika na timu yake ya kusifu na kuabudu kutoka kanisa la EAGT Mito ya Baraka wakimwabudu Mungu.


 Baadhi ya washiriki wa Kongamano na mkutano wakiserebuka.