Madiga Timotheo ni mmoja wa waimbaji wa nyimbo za injili wa hapa nchini Tanzania,amekuwa akishirikiana na jeshi la polisi katika kuhamasisha juu ya ulinzi shirikishi ambayo imekuwa ikisaidia sana kuwafichua wahalifu mbalimbali.
Amekuwa pia akihudumu kwenye makongamano mbalimbali ya injili katika sehemu mbalimbali hapa nchini Tanzania akitumika kueneza injili ya Yesu na pia amekuwa akishiriki shughuli mbalimbali za kiserikali.na pia unaweza kuwasiliana naye kwa shughuli mbalimbali kama mikutano ya injili semina tumia namba 0752187043 na 0714267875.
YESU NI JIBU
Ijumaa, 14 Desemba 2012
Jumapili, 9 Desemba 2012
Hatuwezi kuzuia mfumuko wa “imani Potofu” hata kama zina madhara kiimani
Tafsiri mpya ya msamiati wa
“Imani potofu”
Siku
hizi jamii imeanza kuchanganyikiwa na kile kinachoitwa “kuongezeka kwa imani
potofu” zenye kudanganya na kuathiri imani za wengi kiitikadi.
Kutokana
na uchunguzi wangu binafsi, nimekuja kubaini kwamba, mahali tulipofikia kumbe
tafsiri yake ina utata mkubwa na maana nyingi tena tofauti hata kama matamshi ni yale yale. Ninachotaka kuelezea hapa ni
kwamba, kila inayoitwa “imani potofu” na wengine, kumbe nayo inaziona imani
nyingine nje yake ndizo zimepotoka! Kwa maelezo mengine, tumefikia mahali
ambapo “Usahihi” wa imani yako ni “upotofu” wa imani kwa mwingine aliye tofauti
na wewe kiitikadi.
Ni
kutokana na utata huu, Mamlaka za nchi mbali mbali duniani zilifikia hatua za
ama kupiga marufuku “imani zote” na kubakia dini moja au chache zinazokubalika.
Kisha baadaye ikaonekana huu ni udikteta usiotenda haki kwa binadamu na hivyo likaanzishwa “Tamko la Haki za
binadamu ulimwenguni” ambalo pamoja na mambo mengine limejumuisha “haki ya
kuabudu” na kujiunga au kubadili dini. Kwa mujibu wa tamko hili fursa imetolewa
kuwepo kwa imani nyingi, zilizopo hivi sasa, na kuanzishwa mpya, ili mradi mtu
havunji sheria za nchi
Kwa
kupitia haki ya uhuru wa kueneza imani, kila mtu anapata fursa ya kuchagua au
kuacha, kujitenga au kujiunga na imani ile ambayo anaiona ndiyo sahihi kwa
uelewa na utashi wake binafsi. Kwetu sisi Tanzania, uhuru wa kuabudu ni haki
ya kikatiba.
Baada
ya kutoa maelezo ya msingi kuhusu utata wa tafsiri ya “Imani potofu”; naomba
sasa nije kwenye kuwasilisha tafsiri mpya ya msamiati wa “Imani potofu”.
Tafsiri hii kwa hivi sasa ndiyo inayotumika na sehemu kubwa ya jamii. Tafsiri
yenyewe ni kama ifuatavyo:
“imani yoyote inayokera imani nyingine; na
inapata umaarufu mkubwa kiasi cha kuwa tishio la kuvutia wafuasi wa imani
nyingine kujiunga nayo”
Imani
hiyo inaweza kuwa ni sahihi au potofu kulingana na mtazamo wa kila mtu kwa
itikadi yake, lakini kigezo kinachozingatiwa katika kuibatiza jina la “Imani
potofu”; ni pale ambapo “wafuasi wengi wa imani za dini nyingine wanaondoka au
kuyahama madhehebu yao na kujiunga na imani hiyo” ! Katika harakati za kujaribu
kudhibiti matishio ya imani hiyo, na kuwakinga waumini wao wasijiunge nayo ni
kuitangaza rasmi kuwa ni “imani potofu”
Naomba
nijihami mapema msomaji kwa kusema kwamba, kwa kusema haya sina nia ya
kuhalalisha “Imani potofu” kupitia mada hii. Naomba nisieleweke kwamba sio kila
“imani inayoshawishi maelefu ya watu kujiunga nayo ni sahihi au ni potofu”.
Hoja
ninayotaka kuiweka bayana ni kuhoji uhalali wa matumizi ya kigezo cha
“ushawishi na umaarufu mkubwa” kutafsiriwa kuwa imani husika ni potofu kwa
sababu hiyo tu! Ingelikuwa kigezo hiki kina mantiki, basi tungeweza kutilia
mashaka imani zote zenye wafuasi wengi kuwa zimefanikiwa kwa sababu nazo ni
“imani potofu”!
Mtazamo
wangu, na uzoefu wangu binafsi, imani zote, ziwe potofu au sahihi, ziwe mpya au
za zamani, zote zikiweka bidii kikamilifu katika kujieneza kwa jamii zinaweza
kuwa na wafuasi wengine pasipo kujali sana
usahihi au upotofu wake kiitikadi. Lakini naweza kukubali kwa sehemu kwamba
usahihi au upotofu wa imani unaweza kuchangia kwa kiasi fulani kufuatwa na
wafuasi wengine kwa kutegemea ni mbinu gani ya kimawasiliano inayotumika.
Dhana ya imani potofu kuwa na
wafuasi wengi kuliko imani sahihi
Baada
ya kuelezea tafsiri ya msamiati wa imani potofu kwamba ni ushawishi na umaarufu
wa kupata wafuasi wengi kwa haraka; na baada ya kubainisha waziwazi kwamba nia
ni kujaribu kuwakinga waamini wasihame na kujiunga na imani inayovuma kwa
wakati husika; sasa nije kwenye chimbuko la tafsiri hii iliyoshika hatamu
katika jamii.
Kwa
karne nyingi imekuwepo dhana kwamba, imani potofu ina uwezo wa kuwa na wafuasi
wengi kwa sababu zimetokana na Shetani mwenyewe. Tena yapo na maandiko
yatumikayo katika kusimamia dhana hii ua kwamba hata Yesu mwenyewe alitabiri
juu ya manabii wa uongo ambayo watadanganya wengi. (Math…….) Maandiko mengine
ni ya mitume akina Petro na Paulo yaliyolitahadharisha kanisa kwamba watakuwepo
mitume na manabii wa uongo ambao watatengeneza wafuasi wengi kwa ushawishi na
udanganyifu wao.
Kwanza kabisa, naomba kuthibitisha kwamba ni
kweli imani potofu zinapata wafuasi wengi kwa sababu zimejaa udanganyifu wa
Shetani. Tena naweza kuongezea uzito katika hoja hii kwa kusema kwamba,
kinachofanya imani potofu kupata wafuasi wengi ni kwa sababu hazina masharti
yenye maadili ya kiungu, na zimejaa uwashiwi unaohamasisha tamaa binafsi au
wanaotafuta msaada binafsi.
Lakini,
ninapenda kuzungumuzia udhaifu wa dhana hii. Sio kweli hata kidogo kwamba,
imani sahihi haipati wafuasi wengi kwa sababu yenyewe ndiyo imetokana na Mungu
wa kweli. Ingelikuwa hii ndiyo maana sahihi, basi Yesu Kristo mwenyewe, enzi za
mwili wake duniani, asingefuatwa na makumi elfu ya wafuasi wengi! Maneno yake
na mafundisho yake yalikuwa magumu na mifano mingi ilikuwa na mafumbo lakini
bado umati mkubwa wa watu ulimfuata na kumsikiliza na kushuhudia kwamba huyu ni
Mwalimu kweli kweli!
Kana
kwamba hii haitoshi, baada ya kufufuka na kupaa kwake, mitume wake nao
walitengeneza maelfu ya wafuasi na wanafunzi wengi kama
ilivyokuwa nyakati za Yesu mwenyewe. Kanisa la kwanza lilianza kwa kishindo cha
wafuasi 3000 kwa siku moja na katika muda wa miaka 40 mfululizo lilikuwa na
wafuasi wasiopungua 30,000 wanaokusanyika kwa wiki jijini Yerusalemu!
Ni
nini ninachotaka kusema hapa? Napenda kuweka bayana ukweli huu, kwamba hata
“Imani sahihi katika Kristo”, kama kweli kweli ikihubiriwa kwa usahihi kama Yesu na mitume wake wa kwanza; kazi zile zile
zilizofanyika enzi za karne ya kwanza pia zitatendeka hata sasa. Kwa matokeo
hayo makumi elfu ya watu wataikimbilia imani hii kwa wingi kama
ilivyokuwa karne ya kwanza.
Pamoja na ukweli kwamba “Imani potofu” zina
ushawishi wa kupata wafuasi wengi; lakini sio kwamba hao wafuasi wenyewe hutoka
kwenye imani sahihi na kisha kuijunga na imani potofu! Wengi wao hawakuwahi
hata kuijua “imani sahihi” tangu kuzaliwa kwao na ndio maana ni rahisi kwao
kujiunga na imani nyingine potofu!
Kwanini imani potofu
zimeruhusiwa
kuwepo sambamba na imani sahihi?
Kitu
ambacho kinatatiza watu wengi na hasa wale ambao ni wapenzi wa imani sahihi, ni
kuona jinsi ambavyo imani potofu zinaendelea kufumuka na kuendelea kupoteza
wafuasi wengine wasioijua au kuwa na imani sahihi. Wengine wanafunga na kuomba
wakijaribu kudhibiti ongezeko la imani potofu. Hata hivyo, ukweli halisi bado
imani potofu zinaongezeka kila siku.
Ningependa
kujibu swali hili gumu kwanza kwa kutahadharisha athari zitokanazo na shinikizo
la kutumia nguvu za dola kudhibiti imani potofu. Kujaribu kudhibiti mfumuko wa
imani potofu kupitia nguvu za Dola, kwanza ni kinyume cha katiba na tamko la
haki za binadamu. Pili, kila itikadi katika dini inatafsriwa kuwa potofu na
itikadi nyingine zinazotofautiana kiitikadi. Tatu nitalieleza kwa mujibu wa
mafundisho ya Bwana Yesu Kristo. Kabla sijaanza kufafanua hebu tuyasome maneno
ya Yesu kwa mfano alioutoa:
“Akawatolea
mfano mwingine, akisema, ufalme wa mbinguni umefanana na mtu aliyepanda mbegu
njema katika konde lake; lakini watu walipolala akaja adui yake akapanda magugu
katikati ya ngano, akaenda zake. Baadaye majani ya ngano yalipomea na kuzaa,
yakaonekana na magugu. Watumwa wa mwenye nyumba wakaenda wakamwambia, Bwana,
hukupanda mbegu njema katika konde lako? Limepata wapi basi magugu? Akawaambia
adui ndiye aliyetenda hivi. Watumwa wakamwambia, basi wataka twende
tuyakusanye? Akasema la; msije mkakusanya magugu na kuzing’oa ngano pamoja
nayo. Viacheni vyote vikue hata wakati wa mavuno; na wakati wa mavuno
nitawaambia wavunao, yakusanyeni kwanza magugu, myafunge matita matita mkayachome;
bali ngano ikusanyeni ghalani mwangu.” (Math.13:24-30)
KANISA LACHOMWA MARA TATU MARA TATU LIKIKARABATIWA HUCHOMWA TENA WAHUSIKA WADAIWA NI WAUMINI WA DINI YA KIISLAMU
Wakati serikali ikijitahidi kukabiliana na vitendo vya uchomaji
moto makanisa nchini vinavyofanywa na baadhi ya wanaharakati wa Kiislamu,
imebainika kuwa Kanisa la Salvation
Ministry for all Nations (SMAN) lililoko Mbezi Juu Jijini Dar es Salaam, limechomwa moto zaidi ya mara
tatu.
Uongozi wa Kanisa hilo umelimbia Gazeti hili kuwa licha ya
matukio hayo ya hujuma wanazofanyiwa na waumini wa Kiislamu kutoka katika
msikiti wa Al Mubarak ulioko jirani na Kanisa hilo, usiku wa Jumapili iliyopita
ya Desemba 2, 2012 , waumini hao walilibomoa Kanisa hilo na kufanya jaribio
jingine tena la kulichoma moto.
Kwa mujibu wa Mchungaji kiongozi wa Kanisa hilo
la SMAN Freddy Mwamtembe na Msaidizi
wake Mch. Eliya Sudi, matukio matano ya hujuma mbaya dhidi yao yameripotiwa katika vituo vya polisi Mbezi
Juu na Kawe na kufunguliwa majalada yanayoeleza
jinsi hujuma hizo zilivyofanyika kwa muda na nyakati tofauti.
Hujuma ya kwanza ya uharibifu mali na uchomaji moto wa
Kanisa hilo iliripotiwa katika akituo cha polisi Kawe Februari 25, 2012 na kufunguliwa jalada nambari KW/RB/1743/2012
la kuchoma moto choo cha kanisa hilo,
ambapo jalada la pili la siku hiyo hiyo lilifunguliwa katika kituo cha Polisi
Mbezi Juu likiwa na nambari MBJ/RB/586/2012 likitaarifu juu ya tukio la
kuchomwa moto Kanisa hilo na kuharibu mali majira ya saa saba usiku.
Jalada jingine lilifunguliwa Machi 10, 2012 katika kituo cha
Polisi Mbezi juu na kupewa nambari
MBJ/RB/714/2012, likitoa taarifa juu ya hujuma ya kuchomwa moto kwa Kanisa hilo
la SMAN.
Hujuma nyingine lililofanyiwa kanisa hilo imo katika jalada
la kituo cha Polisi Kawe lenye nambari KW/RB/7974/2012 kama taarifa ya tukio lililofanywa Agosti 12, 2012 na waumini
28 wa msikiti wa Al Mubarak kwa kuvamia ibada,
kujeruhi waumini na kuharibu mali za Kanisa hilo, ambapo Mchungaji Msaidizi
Eliya Sudi alijeruhiwa akiwa madhabahuni.
Aidha uongozi wa Kanisa hilo ulilikabidha gazeti hili waraka
unaoelezea jinsi waumini wa msikiti huo wanavyoshirikiana na mama mmoja
kulifanyia fujo kwa kufukia msingi wa jengo lake na kisha mama huyo kuchimba
msingi na kuanza ujenzi wa nyuma yake katika kiwanja cha Kanisa hilo.
Uongozi huo wa Kanisa la SMAN ulisema ulilifikisha suala hilo katika ofisi
ya Serikali ya Mtaa wa Ndumbwi kupitia
mjumbe wa nyumba kumi shina namba 40 Mbezi
Juu Bwana Bonifasi Matiku kwa ajili ya
utatuzi, lakini hawakupatiwa msaada wowote, hadi ikabidi wamwandike barua Afisa
Mtendaji wa kata ya Mbezi Juu, kumtaarifu juu ya kiwanja cha kanisa lao kuvamia
na mama huyo ambaye kwa sasa jina lake limehifadhiwa.
Mjumbe huyo alidhibitisha juu ya kuwepo kwa hujuma dhidi ya
Kanisa hilo na
hatua alizochukua,ambapo liitaka serikali kutumia sheria ili kukabiliana nazo
na kuzikomesha.
“Nakumbuka siku nilipofika ofisini kwa Mtendaji wa Kata ya Mbezi Juu, niliishia kutukanwa na wajumbe niliowakuta
pale (majina tumeyahifadhi kwa sasa), wakinieleza mbele ya Mtendaji huyo kwamba
ni lazima mama huyo atajenga katika eneo
la kiwanja chetu cha Kanisa. Nilimtahadharisha Mtendaji juu ya matusi
niliyotukanwa lakini akanitaka niondoke akidai atashughulikia suala hilo. Mwandishi hadi leo hakuna kilichofanyika”, alisema
Mchungaji Mwamtembe.
Alisema tayari amelifikisha suala la hujuma za Waislamu dhidi ya Kanisa lake katika
ofisi za Kamanda wa Mkoa wa Kipolisi wa Kinondoni alikoahidiwa kushughulikiwa
haraka kwa mujibu wa sheria.
“Kwa kweli sisi Wakristo ni wavumilivu sana kwa vile tunapenda amani na utakatifu.
Tunaiomba sana
serikali iwashughulike watu hawa wachache wasiopenda amani na wanaochochea
vurugu za kidini. Ugomvi wa kidini ni mbaya sana. Tunaomba serikali iwe makini katika
hili”, alisema Mch. Mwamtembe.
Alisema waumini hao korofi wa Kiislamu wanaolihujumu Kanisa lake
kwa kulichoma moto, kuharibu mali na kujeruhi
washirika ni watu wanaofahamika wazi na hufanya hujuma hizo wazi wazi,
wakitamka wazi kuwa hawataki Kanisa
katika maeneo yao; jambo ambalo ni kinyume kabisa na Katiba ya nchi inayoruhusu uhuru wa kuabudu kwa kila mtu
Mmoja wa Mashehe wa Msikiti
wa Al Mubarak Mbezi Juu aliyetajwa kuwa mstari wa mbele kuhamasisha
waumini wake kulihujumu kanisa la SMAN, hakuweza kupatikana kutokana na
kutofika msikitini hapo kwa uwazi, akiogopa kukamatwa na Polisi wanaomsaka.
Aidha juhudi za kumpata mama aliyetajwa kushirikiana na
waumini wa msikiti wa Al Mubarak kulihujumu kanisa hilo hazikuzaa matunda, kutokana na makazi yake kutojulikana.
Jumatano, 31 Oktoba 2012
ELIMU YA UJASIRIAMALI NA USHAURI KUTOLEWA VIJANA NMA WAJANE NA TAASISI YA RUTH'S FAITH RFO
Elimu ya ujasiriamali na ushauri ni vyema ikatolewe
kwa vijana na wajane ili kuweza kuwakwamua la tatizo la umaskini ambalo linawakabilisanjari
na kuwafundisha neno la Mungu.
Kauli hiyo ilitolewa na jijini Dar es saalam naaskofu
wa huduma ya Pentekoste Gospel Mission Askofu Barnabas Kimbe wakati wa uzindizi
wa taasisi ya Ruth's Faifh Organization ambapo alisema kuwa ni vyema elimu ya
ujasiria mali itolewe kwa vijana na wajane hasa itolewe kwa vitendo.
Aidha alisema kuwa katika nyumba ya Mungu kuna vipawa
mbalombali na inastahili kutumiwa kwa lengo la kuujenga mwili wa kristona kuu
shauri pia ili kuweza kuondokan na wimbi la umaskini ambalo linawakabili watu
wengi kwa sasa.
Huduma hii ya RFO ni vyema zaidi ikaenea nchi nzima
ili kuwakwamua vijana na wajane na wimbi la umaskini kwa kutoa elimu ya
ujasiriamali itakayowasaidia.
Naye mwenyekiti wa taasisi ya Ruth's Faith mwalimu
Claudia simba alisema kuwa lengo kubwa la kuanzishwa kwa taasisi hiyo ni
kuwasaidia ,kufundisha na kushauri vijana ambao wengi wao wamekosa washauri na
kubaki kujiongoza wenyewe katika ujana wao hususani vijana wa kiume na watoto
wa wachungaji.
Aidha Bi Simba alisema kuwa taasisi hiyo itakuwa
ikitoa ushauri katika maeneo ya
mahusiano katika uchumba na ndoa kwa wazazi hususani wachungaji ambao ndoa zao
zinalegalega na kutoa elimu kwa jamii hasa upande wa kukopa na kurejesha mikopo
hiyo.
Kutokana hayo taasisi hiyo ilibaini kuwa ndani ya
jamii kuna watu wengi wanaoweza kukopa na kushindwa kurudisha mikopo hiyo hivyo
elimu itatolewa ya ujasiriamali ,utunzaji wa fedha na juu ya biashara kwa
ujumlasambamba na kuwasaidia wajasiria mali hao kuwatafutia masoko ya bidhaa
zao ndani na nje ya nchi ili waweze kujiendeleza katika shughuli zao bila kuwa
na mashaka wapi watapeleka bidhaa zao wakisha tengeneza.
Hata hivyo itahusika kutoa ushauri kwa wake wa
viongozi wa dini kwa kuwafundisha ujasiriamali na kujitegemea kuwatia moyo
kufanya changizoili kuwawezesha kupata mitaji bila kubagua dini, dhehebu ,rangi
jinsia ,utaifa na kabila.
Pamoja na hayo taasisi hiyo itahusika na jamii ya watu
wenye ulemavu ,wajane ,yatima,watatoto wanoishi katika mazingira magumu kwa
kuwapa nyenzo zitakazowasidia katika maisha yao.Taasisi hiyo ilianzisha juni
mwaka 2011 ikiwa na maona hayo ya kusaidia jamii ila kutokana na kutokuwa na
wafadhili ilikwama mpaka kufikia wakati huu.
MAOMBI YA KUHAMASISHA AMANI KATIKA TAIFA LA TANZANIA
MAOMBI YA KUHAMASISHA AMANI KATIKA TAIFA LA TANZANIA
Suala la amani na usalama ndani ya nchi ama taifa ni
jukumu la kila mwananchi kuhakikisha kuwa unadumu sanjari na kumwomba Mungu juu
ya jambo hilo.
Kauli hiyo ilitolewa jijini Dar es saalam na askofu
Daktari Mgulu kilimba wa huduma ya christian mission Fellowship wakati wa ibada
maalum yamaombi ya kuhamasisha amani nchini.
Aidha askofu DK Kilimba alisema neno la
Mungu limetuagiza katika 1timotheo 2:1-2; kuwa kabla ya mambo yote nataka dua,
sala, maombezi na shukurani vifanyike kwa watu wote; kwaajili ya Wafalme na
wenye mamlaka, tuishi kwa utulivu na amani, katika utauwa wote na ustahivu ,tukiwa
Kanisa la Mungu, tumechukua hatua hii ya kuanza kuliombea Taifa kwa kuugua mno
ili Amani tuliyopewa na Mungu na
kuenziwa na waasisi wa Taifa hili iweze kudumishwa.
"ndugu zangu watanzania sote tufahamu
kuwa, msimamo tuliyojiwekea katika katiba yetu ya jamhuri ya muungano wa tanzania, ni
kupiga marufuku kila namna ya ubaguzi ukiwemo wa kijinsia, rangi na kidini.
Katiba ya 1977 ibara 13(5) ambapo kwa upande wa madhehebu ya dini tanzania tuna
dini kubwa tatu na nyingine ndogondogo dini kubwa ni ukristo, uislamu na dini
za kijadi.toka mwanzo wakristo na waislamu tumekuwa tukishirikiana pamoja
katika misiba, sherehe mbalimbali, kuoleana, kuishi katika nyumba moja na kufanya shughuli za kijamii kwa pamoja
bila kubaguana kabla na baada ya miaka
hamsini ya uhuru nchi yetu" alisema askofu dk kilimba .
Aliongeza kuwa wakristo na watanzania kwa
ujumla ni vyema kufahamu kuwa, hakuna nchi
yeyote katika bara la afrika
yenye idadi kubwa ya wakristo na waislamu wanaoishi kwa amani na upendo kama tanzania,ila kwa sasa watu wasioitakia
amani nchi yetu wanataka kupenyeza chuki za kidini ili isiwe nchi ya amani bali ya vurugu.
Kutokana na hayo hivi karibuni tumeshuhudia
kuwepo kwa vitendo vinavyoashiria ubaguzi wa kidini kwa baadhi ya vikundi toka
makundi ya dini kubwa kudai haki zao ambazo kimsingi wanaona wanastahili kuwa
nazo sawa na dini nyingine, hali hii imefanya vikundi hivi vitumie vyombo vya
habari hususani redio, magazeti na machapisho mbalimbali kueleza hisia zao kwa
jamii, jambo ambalo limesababisha kuwepo kwa mgawanyiko katika jamii iliyokuwa
imeshikamana na mgawanyiko huu unazidi kukua siku hadi siku na kusababisha hali
ya chuki kwa mamlaka ya nchi na hatimaye dini moja na nyingine.
"Baada ya kufanya utafiti wa kina
kwanini kuwepo na chuki baina ya makundi ya dini na serikali tumeona kuwa,
makundi haya ya dini yanaiona serikali inawanyima haki zao na inapendelea dini moja na hivyo kutumia mfumo wake katika
utawala, ambapo madai ya kundi hilo
yanawapelekea kuwafanyia vurugu waumini wa kundi wanalosadiki kuwa
linapendelewa na serikali, jambo ambalo linawafanya wanaofanyiwa vurugu
wasitumie uhuru wao wakufanya ibada
ambayo kimsingi walipewa mungu na kuandikwa katika katiba ya nchi yetu",
aliongeza.
Pamoja na hayo tukiwa kanisa la mungu, hali hii
inatupelekea kuona kuwa bado serikali yetu haijawajibika ipasavyo katika
kuelekeza sera na shughuli zake kwa lengo la kuhakikisha kuwa sheria za nchi
zinalindwa na kutekelezwa, kimsingi haki na uhuru wa watu wengine au maslahi ya
umma vinapaswa kutoathiriwa kabisa na
matumizi mabaya ya uhuru wa haki za watu binafsi.
Hivyo askofu Dk Kilimba aliongeza kusema kanisa baada
ya kumlilia mungu kwa machozi na maombi mengi, tumeamua kuchukua mwelekeo wa
uwajibikaji usio wa maneno tu, kwani
suala la kutoa matamko ya kulaani
limefanywa na dini na serikali kwa mkazo mkubwa. Na kwa upande wa
serikali, watawala wa nchi yetu wamekuwa
wakilaani na kukemea, ubaguzi wa dini,
rushwa na ufisadi katika taifa hili bila mafanikio na hata leo tunawaona
vijana wanatwangana hadharani kutokana na kushamili kwa rushwa ,hii yote ni kwa
sababu hayo ni vita ya kiroho na
inapaswa kukemewa na viongozi wa dini na watawala wanapaswa kuchukua hatua. Kwa
jinsi hii, kanisa limelitazama jambo hili kiroho zaidi kwa kutambua kuwa chuki
na rushwa ni roho kamili inayotoka kwa shetani, hivyo watu wa kiroho tunalo
jukumu la kuzipinga hila zote za shetani kwa dua,
sala na maombi ili kuleta amani ya kudumu katika taifa letu, ambalo linasifika
kuwa ndiyo kitovu cha amani afrika na duniani.
Akielezea kwa hisia alisema "Ndugu zangu wakristo
na viongozi wa dini, ikumbukwe na
izingatiwe kuwa nyumba za ibada ni
sehemu ya kumwabudu mungu, hivyo
zitumike kuhubiri dini tuliyo amuriwa na mungu na sio siasa, na pasiwe mahali
pa kuandaa na kuchochea vurugu na chuki miongoni mwetu kwani viongozi wa
dini wanaaminiwa sana na waumini wao
na lolote watakalo waambia waumini,
huaminiwa kuwa limetoka kwa mungu".
Aidha aliongeza kuwa ikumbuke kuwa, tunafanya kila kitu
vizuri zikiwemo ibada zetu kwasababu ya amani tuliyonayo, amani isipokuwepo
hakuna kitu kinaweza kufanyika katika nchi iwe kwa waumini na wasio wauimini,
iwe kwa maskini au matajiri. Amani ikishaondoka, matajiri au wenye pesa
watakimbia na kuwa wakimbizi wa nchi zingine, huku masikini wakikosa mahali pa
kwenda na kuishia kuuawa na kupoteza maisha. Kwa hiyo ni vema kuitunza amani
yetu na kuilinda,kamwe tusiichezee amani tuliyonayo katika nchi yetu, hii ni
tunu tuliyopewa na mungu na kuachiwa na waasisi wa nchi yetu ili tuienzi, hivyo
kila mmoja wetu ni mdau wa amani. Mkulima anahitaji amani ili aweze kupata
mazao shambani mwake; daktari anahitataji amani ili afanye kazi zake vema
hospitalini, kadhalika mfanya biashara na mwanasiasa wote wanahitahi amani.
Pamoja na hayo yote askofu Dk Kilimba alisema kuwa kamanda
Suleiman Kova wa kanda maalum ya dar es saalamkwa ameonesha juhudi zake za kuifanya Dar-es-saalam iendelee kuwa
bandari ya amani, ameonesha ushupavu na umadhubuti mkubwa katika kauli zake,
kwani mchango wake umeleta heshima iliyotukuka katika vyombo vya dola
nchini na kwa watanzania wote.
Katika maombi hayo ya kuhamasisha amani nchini yalitanguliwa
na maombi ya watu 12 waliowakilisha zaidi makabila 120 ya tanzania kwa kutumia lugha za makabila hayo kama
alama ya umoja na mshikamano.
NAMNA YA KUMSIFU NA KUMWABUDU MUNGU--MWALIMU MGISA
Tumejifunza mambo mengi sana yaliyokuhamasisha na yaliyokupiga deni uwe
kiumbe wa kumsifu na kumtukuza Mungu. Tunapomsifu mtu, huwa
tunaelezea yale ambayo yanamtofautisha na wengine. Hivyo basi, ufikapo
katika muda wa kumsifu na kumwabudu Mungu, ujue namna ya kuifanya sifa
yako na ibada yako kwa usahihi.
Na ili kumpa Mungu sifa na ibada, ni lazima na ni muhimu sana ujue
mambo ambayo yanamstahilisha Mungu wetu kusifiwa na kutukuzwa. Kwa
kutumia sifa na tabia za Mungu, utaweza kumsifu na kumwabudu vizuri.
Hakuna kiumbe kingine chochote kinazo zile sifa kuu tano za Mungu,
isipokuwa yeye Mungu Jehova peke yake.
Kwahiyo, na hizo ndizo zinayomstahilisha yeye kusifiwa na viumbe
wake. Katika sura ya nane, tumeshajifunza mambo yanayomstahilisha Mungu
kupewa sifa. Kwakuwa sasa unayajua, basi tumia mambo hayo uendapo
mbele za Mungu katika katika ibada yako ili kumsifu na kumwabudu.
Unapomueleza Mungu sifa zake na tabia zake (vile alivyo) hapo unakuwa
unamsifu na kumwabudu.
Tofauti ya kusifu na kuabudu
Naomba urudie kuisoma sura ya kwanza ya kitabu hiki, ambapo nimefundisha
vizuri maana ya kumshukuru Mungu, kumsifu Mungu na kumwabudu Mungu.
Hii itakusaidia kutofautisha mambo haya kwa nia ya kuyaelewa au kuyaelezea
kwa mtu mwingine. Nilisema hivi,
Ibaba ni kitendo cha mtu kumtukuza, kumhimidi, kumwinua, kumwadhimisha,
kumshukuru na kumheshimu Mungu kwa vile alivyo na kwa yale aliyoyatenda.
(Appreciation and admiration for who God is and for what He has done).
Lakini haya mambo matatu, yanayofanana sana na si rahisi sana
kuyatenganisha kimaelezo au kivitendo.
Lakini tuendapo mbele za Mungu kwa ibada, iwe ni chumbani kwako
au sebuleni kwako au kwenye gari lako au kanisani kwako, kusifu na kuabudu
na kushukuru, ni mambo yanayofanyika kwa kuingliana sana. Sio sheria
kwamba, hautakiwi kuchanganya sifa na kuabudu na kushukuru, hapana.
Hebu soma tena sura ya kwanza vizuri. Kati ya mengi, nilisema hivi;
Haya mambo matatu, kusifu, kushukuru na kuabudu, ni mambo
yanayofanana sana. Inaweza ikawa vigumu kidogo kuyatenganisha kimaelezo
au kivitendo. Ni ngumu kidogo, kufanya kimoja pasipo wenzake, kwasababu ni
mambo yanayokwenda kwa pamoja sana. Lakini kwa tafsiri zake, yako hivi;
1. Kumshukuru Mungu;‐ Ni ile hali ya kumueleza Mungu jinsi
tunavyothamini (Appreciate and Admire) wema wake, fadhili zake na
baraka zake katika maisha yetu.
2. Kumsifu Mungu; ‐ Ni kumueleza Mungu juu ya matendo yake makuu
na ya ajabu aliyoyafanya. Au ni kuwaeleza wengine kuhusu matendo
makuu ya Mungu aliyoyafanya katika maisha yetu au kwa watu
wengine.
3. Kumwabudu Mungu; ‐ Ni kumueleza Mungu tukuzo zetu, heshima yetu
na upendo wetu kwake kwasababu ya uzuri wa tabia zake kwetu.
(Credentials and Characters).
Kwahiyo, tuendapo mbele za Mungu kwa ibada, iwe ni chumbani kwako au
sebuleni kwako au kwenye gari lako au kanisani kwako, ili kumsifu na
kumwabudu na kumshukuru Mungu, uwe huru kujimimina mbele za Mungu
kwa kufanya vyote vitatu, kwa namna moyo wako utakavyokuwa unaongozwa
na Roho Mtakatifu. Vyote vitatu vinatengeneza ibada takatifu kwa Mungu.
Katika sura inayokuja, nimefundisha vizuri namna ya kuingia katika
ibada na hata kupenya na kufika katika chumba cha ndani kabisa cha uwepo
na utukufu wa Mungu; ili unapokwenda mbele za Mungu wetu, uweze
kukutana na nguvu zake katika utukufu wake.
Lakini hapa chini nimeziweka kwa ufupi ili kukukumbusha. Na pia
nimekuongezea na mambo mengine yanayotakiwa katika kumsifu na
kumtukuza Mungu. Kwahiyo, utengapo muda wa kukaa mbele za Mungu wetu
kwa ibada, msifu na kumtukuza Mungu kwa mambo yafuatayo,
1. Mtukuze Mungu kwa Sifa zake za Uungu (ambazo hakuna mwingine
aliye nazo) Kwamba;
a) Jehova ni Mungu wa Milele
b) Jehova ni Mungu Mtakatifu
c) Jehova ni Mungu Aliye kila mahali
d) Jehova ni Mungu Anayejua mambo yote
e) Jehova ni Mungu Aliye na nguvu zote na
anaweza kufanya mambo yote kabisa.
Nimezielezea vizuri hizi sifa za Uungu, katika sura ya kwanza. Hizi ni baadhi tu
ya sifa za Mungu, sio zote. Kwa hivyo basi, pamoja na namna nyingine ambazo
utajifunza kumsifu na kumwabudu Mungu, hebu uwe unamsifu Mungu kwa
mambo haya au kwa sifa zake hizi pia.
Msifu Mungu kwa;
2. Kwasababu ya Tabia zake
3. Kwasababu ya Matendo yake ya Ajabu
4. Kwasababu ya Fadhili nyingi na kuu mno
5. Kwasababu ya Ahadi zake kubwa za thamani2. Mtukuze Mungu kwa Tabia zake
Neno la Mungu, linatuonyesha jinsi ambavyo Mungu wetu ana tabia na
kawaida nyingi nzuri ambazo kwa hizo, tunavutiwa na tunapigwa deni kumsifu
na kumwabudu. Kwa mfano ; Biblia inasema kwamba, Mungu wetu amejaa
Upendo, usio na mwisho. Ni Mwingi wa huruma, Si mwepesi wa hasira, sifa
yake ni kuwa na rehema daima. Soma mistari ifuatayo, ili uone zaidi. Lakini
kwasababu ya sifa hizi (Tabia zake), tunapigwa deni kumsifu na kumwabudu.
*Zaburi 103:8, Kutoka 34 :6,
*Efeso 3 :18‐19, Daniel 9 :4, Ufunuo 19 :11
3. Mtukuze Mungu kwa Matendo yake ya ajabu.
Mungu wetu ni Mungu aliyefanya mambo ambayo hakuna tena, awezaye
kufanya. Kwa mfano; ndiye aliyeziumba na kuzitundika sayari zote za
ulimwengu huu, bila minyororo wala nguzo. Mungu wetu ndiye
anayesababisha mioyo yetu inadunda, bile kuwekewa betrii wala chaji
(charge). Au ni lini ulichomeka moyo wako katika soketi ya umeme kama
unavyochomeka simu yako ili kupata umeme?
Nina uhakika, hakuna mtu anayefanya hivyo. Sasa unadhani moyo
wako unadundaje? Hizo ni kazi za ajabu za Mungu wetu.na hakuna mtu
awezaye kuzifanya. Kwasababu ya matendo yake ya ajabu, Mungu wetu
anastahili kusifiwa na kutukuzwa. Soma mistari ifuatayo kwa umakini.
Utaweza kuona kwa uchache, jinsi maandiko yanavyoeleza juu ya matendo
makuu ya Mungu.
Haya ni maelezo ya watu wa Mungu ambao kwa kumjua Mungu, waliweza
kueleza ukuu wake vizuri, ili na sisi tunaosoma maandiko yao, tunajifunza juu
ya ukuu wa Mungu, uweza wa Mungu na tabia za Mungu wetu. Soma vizuri
Kitabu cha Daniel 6:25‐27, Nehemia 9:6, Zaburi 147:1‐18, na Zaburi sura ya
136:4‐26
4. Mtukuze Mungu kwa Fadhili zake.
Mungu wetu ni Mungu atupaye baraka na fadhili nyingi kila siku. Fikiri wema
ambao Mungu amekufanyia maishani mwako, na hata katika siku ya leo tu.
Kuna vingi ametupa ambavyo wengi walitamani, lakini hawakupewa. Uhai,
afya, ulinzi, rehema, chakula, fedha, shule, simu, gari, nyumba, ajira, mke,
mume, watoto, na hata wazazi.
Sio kila mtu bado ana wazazi. Na wengine wamezaliwa hawajawahi
kuwajua wazazi wao. Kwakweli fadhili na baraka za Mungu ni nyingi sana;
ukiamua kuziorodhesha, utakesha. Sasa, kwa fadhili zote hizi alizotujalia, basi
Mungu wetu anstahili kusifiwa.
*Zaburi 103:1‐5, Zaburi 107:21, 2Nyakati 20:21
5. Mtukuze Mungu kwa Ahadi zake.
Ni Mungu aliyetuahidi watu wake, mambo mengi sana mazuri. Ametupa ahadi
kubwa mno na za thamani sana. Ni ahadi za kutupa baraka, heshima na utajiri.
Kwa ahadi hizi pia, anastahili kusifiwa * 2Petro 1:3‐4, Efeso 1:3‐4, Kumbu 4:4‐
8 Kwa ufupi, hivi ndivyo unavyotakiwa kumsifu na kumwabudu Mungu.
Kadri unavyoanza kufanya hivi kwa vitendo, utaendelea kujifunza kufanya
huduma hii ipasavyo, nawe utajikuta unakutana na nguvu za Mungu kwa
namna ya tofauti maishani mwako.
MSIFU MUNGU KWA MAJINA YAKE.
Majina ya Mungu, hueleza sifa za Mungu, Tabia za Mungu au Matendo ya
Mungu. Mfano; Wayahudi wanamwita Mungu El‐Shaddai. Ni neno lenye
majina mawili ndani yake. ‘El’ maana yake Mungu, na ‘Shaddai’ lenye maana
itokanayo na neno ‘Shad’ yaani Titi (Ziwa) la mama anyonyeshaye.
Kutokana na ukweli kwamba, titi/ziwa la mama anyonyeshaye,
linampa mtoto mchanga kila kitu anchohitaji. Maziwa ya mama yake, humpa
mtoto kila kitu mtoto anachohitaji. Ndani ya maziwa kuna vitamini, protini,
wanga, mafuta, madini, maji, na kila kitu mtoto anachohitaji. Maziwa ya
mama, yanamtosheleza mtoto kwa kila kitu. Hivyo, Waisraeli wanapomwita
Mungu El‐Shaddai, wanamaanisha kuwa, kama ziwa linavyo mtosheleza
mtoto, vivyo hivyo, Mungu ni ‘Mtoshelezi’ kwetu. Halleluyah!
Hivyo, kila jina la Mungu, linabeba aidha Sifa yake au Tabia yake au
Matendo yake. Ndio maana Mfalme Daudi anasema
“Mpeni Bwana, enyi wana wa Mungu … Mpeni Bwana utukufu kwa
jina lake. Mwabuduni Bwana kwa uzuri wa utakatifu.” (Zab 29:1‐
2) Msifuni Bwana kwa kuwa Bwana ni mwema, Liimbieni Jina
lake, kwakuwa lapendeza.(Zaburi 135:3).
Na Bwana Yesu alitufundisha kuanza sala namna hii;
Baba yetu uliye mbinguni, jina lako tukutuzwe, hakafu Ufalme
wako uje hapa duniani.
Kwahiyo, unaweza pia kumsifu Bwana kwa majina yake. Majina ya Mungu,
hueleza aidha sifa za Mungu au tabia za Mungu au Matendo makuu ya
Mungu. Yafuatayo hapa chini, ni baadhi ya majina ya Mungu kwa lugha ya
Kiebrania, yatakayokusaidia kumsifu, kumwabudu na kumshukuru Mungu.
MAJINA YA MUNGU
Jina la Mungu Maana yake Mstari wa Biblia
1. Adonai ‐ Mungu Mwenye enzi yote ‐ Mwa 15:2‐8, Kut 6:2‐32. El‐Ohim ‐ Mungu Muumbaji ‐ Mwa 33:20, Kol 1:16‐17
3. El‐Elyon ‐ Mungu Aliye juu zaidi ‐ Mwa14:18, Dan 4:34
4. El‐Gibbor ‐ Mungu Mwenye Nguvu ‐ Isa 9:6, Zab 147:5
5. El‐Hai ‐ Mungu Aliye Hai/Anaishi ‐ Josh 3:10, 1Sam17:26
6. El‐Olam ‐ Mungu wa Milele ‐ Ufu 4:8, Kut 3:14
7. El‐Roi ‐ Mungu Aonaye kila kitu ‐ Mith 15:3, Zab 32:8
8. El‐Shaddai ‐ Mungu Mtoshelezi ‐ Mdo 17:28, Kumb 8:4
9. Jehovah ‐ Ajitegemeaye kuwepo ‐Kut 6:2‐8, Mdo 17:24‐25
10. Jehovah Shalom ‐Mungu Amani yetu ‐ Amu 6:22‐24
11. Jehovah Rapha ‐ Mungu Atuponyaye ‐ Kut 15:26
12. Jehovah Jireh ‐ Mungu Mtoaji wetu ‐ Mwa 22: 8, 14
13. Jehovah Nissi ‐ Mungu Ushindi wetu ‐ Kut 14:13‐14
14. Jehovah Saboath ‐ Bwana wa Majeshi ‐ Malaki 3:7
15. Jehovah Shammah ‐ Bwana ni Aliyepo ‐ Kut 3:14
16. Jehovah Rohi ‐ Bwana ni Mchungaji wangu ‐ Zab 23:1
17. Jehovah Tsidkenu ‐ Bwana ni Haki yetu ‐ Yer 23:6
18. Jehovah Mekaddishem ‐ Bwana Atutakasaye ‐ Kut 31:13
Namna za kumshukuru, kumsifu, na kumwabudu Mungu wetu.
Kwahiyo, katika maisha yetu sisi, kama waumini, tunatakiwa kumpa Mungu
wetu ibada, (kumshukuru, kumsifu na kumwabudu) kwasababu ya mambo
yote hayo niliyoyataja. Tunatakiwa kumtukuza Mungu kwasababu ya sifa zake,
na kwasababu ya tabia zake, na matendo yake na fadhili zake na ahadi zake
kwetu.
Sasa basi, hapa chini, nimekuwekea njia kuu tatu ambazo unaweza
kumsifu na kumtukuza Mungu kwazo. Utengapo muda wa kwenda mbele za
Mungu, unaweza kutuia njiia kuu zifuatazo; Kumtukuza Mungu kwa,
1. Kumwimbia nyimbo za kumsifu na kuwabudu
2. Kumweleza au kusimulia kwa maneno
3. Kumtolea Mungu sadaka na dhabihu
Wako katika kazi ya Mungu
Mwl. Mgisa Mtebe
+255 713 497 654
mgisamtebe@ yahoo.com
www.mgisamtebe.org
Jumatano, 24 Oktoba 2012
KANISA LA KKKT KUFUNGA NA KUOMBA TAREHE 28 OCTOBA 2012 KUOMBEA AMANI TAIFA
Kufuatia matukio ya Uvunjifu wa Amani unaofanywa na kikundi cha watu
wachache kwa mwamvuli wa "dini". Kanisa La Kiinjili la Kilutheri
Tanzania (KKKT) limetoa waraka elekezi wa wachungaji Wake Wote Tanzania
kuelekeza kuifanya siku ya tarehe 28 Oktoba, 2012 kuwa ya Kufunga na
Kuomba kwa ajili ya amani nchini.
KKKT linakuwa kanisa la kwanza Tanzania kupitisha siku ya kikanisa la kufunga na kuomba kwa ajili ya amani ya nchi ilivyo Sasa.
Blog hii ambayo imefanikiwa kuutia machoni waraka huo uliotumwa na Maaskofu Dayosisi zote KKKT Wakuu wa Vituo vya Kazi za Umoja, KKKT na nakala yake kutumwa manaibu katibu wakuu, wasaidizi wa Maaskofu, Dayosisi zote KKKT, makatibu wakuu dayosisi zote kuwaelekeza kwamba tarehe 28 Oktoba ni siku ya kufunga na kuomba.
KKKT linakuwa kanisa la kwanza Tanzania kupitisha siku ya kikanisa la kufunga na kuomba kwa ajili ya amani ya nchi ilivyo Sasa.
Blog hii ambayo imefanikiwa kuutia machoni waraka huo uliotumwa na Maaskofu Dayosisi zote KKKT Wakuu wa Vituo vya Kazi za Umoja, KKKT na nakala yake kutumwa manaibu katibu wakuu, wasaidizi wa Maaskofu, Dayosisi zote KKKT, makatibu wakuu dayosisi zote kuwaelekeza kwamba tarehe 28 Oktoba ni siku ya kufunga na kuomba.
Waraka huo
umeelekeza "Kufuatia matukio ya kuchoma Makanisa yaliyotokea hivi
karibuni,barua inawataarifu kuwa siku ya Jumapili tarehe28 Oktoba 2012
imepangwa kuwa siku maalum ya kuombea amani katika nchi yetu. Pamoja na
mambo mengine yaliyokwisha kupangwa kufanyika siku hiyo (28
Oktoba 2012)' tafadhali sharika, mitaa na vituo vya kazi za umoja vyote
vya Kanisa letu vifanye maombi hayo"
Kwa mujibu wa barua hiyo ya mtendaji mkuu wa KKKT, inawataka waumini wa Kanisa hilo kuendelea kuhimizwa kufunga na kuomba kwa kadri Roho wa Bwana atakavyowaongoza kuombea amani ya Tanzania.
Kwa mujibu wa barua hiyo ya mtendaji mkuu wa KKKT, inawataka waumini wa Kanisa hilo kuendelea kuhimizwa kufunga na kuomba kwa kadri Roho wa Bwana atakavyowaongoza kuombea amani ya Tanzania.
Blog ikinukuu
sehemu ya mwisho ya barua hiyo inaeleza kuwa "Baada ya maombi ya
siku hiyo, washarika wahimizwe kuendelea kufunga na kuomba kadiri Roho wa
Mungu atakavyowaongoza"
Ipo haja na kanisa la Tanzania kuungana pamoja na Kanisa la Kiinjili La Kilutheri Tanzania katika kuombea amani ya nchi.
Ipo haja na kanisa la Tanzania kuungana pamoja na Kanisa la Kiinjili La Kilutheri Tanzania katika kuombea amani ya nchi.
SamSasali.Blogspot.com
Ijumaa, 19 Oktoba 2012
KIKAO CHA MAASKOFU NA WACHUNGAJIWA UMOJA WA MAKANISA YA KIPENDEKOSTE MKOA WA DSM WALIPOKUSANYIKA KWENYE KIKAO
Maaskofu na wachungaji wameitaka serikali ichukue hatua madhubuti kutokomeza wimbi la uchomaji wa makanisa sambamba na uharibifu wa mali kwani hali hiyo inaweza kusababisha amani kupotea katika taifa hili la Tanzania
Kauli hiyo imetolewa na umoja wa makanisa ya kipentekoste kupitia kwa katibu wake jijini Daar es salaam ambao wamekutanika kutafuta ufumbuzi wa tatizo la uchomaji wa makanisa
Akizungumza na waandishi wa habari waliofika katika kikao hicho askofu DAvid Mwasota ambaye ndiye katibi alisema kuwa kikao hicho kilikuwa na lengo la kutathimini uharibibu wa majengo na mali zingine za kanisa na jinsi ya kumaliza tatizo hili ambalo linaonekana kama ni endelevu
Baadhi ya wachungaji pamoja na mbunge wa kigamboni mhe. Faustine Ndungulile wakitembelea makanisa ambayo yameharibiwa na watu wanaosadikiwa kuwa ni waislamu
Mheshimiwa Ndugulile akizungumza na maaskofu na wachungaji kuendelea kuwa na uvumilivu kwa tatizo lililojitokeza
Mwenyekiti waumoja wa makanisa ua kipentekoste mkoa wa Dar es salaam askofu Bruno Mwakibolwa akimwelezea mbunge jambo mhe. Ndugulile
hivyo divyo hali ilivyokuwa
Askofu John Zakaria jimbo la Kinondoni na askofu Bruno Mwakibolwa wa jimbo la Temeke wakimsikiliza mbunge wa Kigamboni kwa makinisa Mhe.Faustine ndugulile.
Katibu wa PCT askofu David Mwasota akielezea hali ilivyojitokeza juu ya suala la uchomaji wa makanisa
waandishi wakichukua habari baada ya kikao cha maaskofu na wachungaji waliofika kutathmini hasara na jinsi ya kutafutia ufumbuzi tatizo hilo
Hizi ni baadhi ya CD ambazo ni vielelezo ambazo viongozi hao walisema kuwa wamepeleka kwa viongozi wa serikali jinsi walivyokuwa wajipanga kuangamiza ama kuaharibu makanisa.
Alhamisi, 4 Oktoba 2012
Hatimaye ufumbuzi wa mafundi mitambo wa vitengo vya sauti umepatikana mara baada ya wakufunzi kutoka Afrika ya kusini kuwasili nchini na kuanza kuwafundisha ili kuweza kutafutia ufumbuzi tatizo hilo.
Wataalamu kutoka makanisa mbalimbali wamefika kujifunza jinsi ya kutatua tatizo hilo katika sehemu zao za kazi na wakufunzi hao wameletwa na HUDUMA VOICE OF HOPE MINISTRY.
Mafunzo hayo yalifanyika kwa muda wa siku mbili 28 na 29 septemba katika ukumbi wa kanisa TAG Mwenge iliyopo Mwenge jijini Dar es saalam
Mchungaji Gay kutoka Afrika ya kusini akiwa na mtafsiri wake ambaye alikuwa akifundisha somo katika semina ya siku mbili ya mafundi mitambo wa sauti na viongozi wa vikundi vya kusifu na kuabudu.
Mchungaji Gay akiwa na mke wake pamoja na mtaalamu wa sauti bwana Wesley ambaye yeye alikuwa akifundisha juu ya soun engineering kwa wataalamu mbalimbali waliofika katiak ukumbi wa kanisa la Mwenge kujifunza.
Waimbaji wa kikundi cha Messengers Band wakitumbuiza katika kongamano la mafundi mitambo.
Kiongozi wa Messengers Band ndugu Noel akiongoza katika kusifu na kuabudu katika kongamano.
Mmoja wa wapiga vyombo wa benbdi ya Messengers ndugu Waziri akionesha umahiri wake.
Ndug Gadrody Mng'anga mwenye shati blue pamoja na wanafunzi wenzake waliofika katika kongamano la mafundi mitambo.
Ni mafundi mitambo kutoka sehemu mbalimbali wakifuatilia kwa makini mafunzo ambaye yalitolewa na wataalamu kutoka Afrika ya Kusini.
Wataalamu kutoka makanisa mbalimbali wamefika kujifunza jinsi ya kutatua tatizo hilo katika sehemu zao za kazi na wakufunzi hao wameletwa na HUDUMA VOICE OF HOPE MINISTRY.
Mafunzo hayo yalifanyika kwa muda wa siku mbili 28 na 29 septemba katika ukumbi wa kanisa TAG Mwenge iliyopo Mwenge jijini Dar es saalam
Mchungaji Gay kutoka Afrika ya kusini akiwa na mtafsiri wake ambaye alikuwa akifundisha somo katika semina ya siku mbili ya mafundi mitambo wa sauti na viongozi wa vikundi vya kusifu na kuabudu.
Mmoja wa wanafunzi waliofika kwenye Kongamano la mafundi mitambo akifuaatilia kwa makini akielekezwa na maalamu na pia ni mmoja wa waimbaji wa bendi ya Dar es saalam Goespel |
Engineer Wesley akiwa na mtafsiri wake Mbuto wakati akitoa mafunzo juu ya vifaa vya sauti( sound system) |
Kiongozi wa Messengers Band ndugu Noel akiongoza katika kusifu na kuabudu katika kongamano.
Mmoja wa wapiga vyombo wa benbdi ya Messengers ndugu Waziri akionesha umahiri wake.
Ndug Gadrody Mng'anga mwenye shati blue pamoja na wanafunzi wenzake waliofika katika kongamano la mafundi mitambo.
Ni mafundi mitambo kutoka sehemu mbalimbali wakifuatilia kwa makini mafunzo ambaye yalitolewa na wataalamu kutoka Afrika ya Kusini.
Jumatano, 26 Septemba 2012
MCHUNGAJI MTIKILA ASHINDA KESI, ASEMA YESU AMEMJIBU MAOMBI YAKE.
Mwenyekiti wa Chama cha Democratic Party (DP), Mchungaji Christopher Mtikila, ameshinda kesi ya uchochezi iliyokuwa inamkabili.
Inadaiwa kuwa Oktoba 21 mwaka jana katika maeneo ya Shirika la Nyumba
la Taifa (NHC), Ilala, jijini Dar es Salaam Mchungaji Mtikila alitoa
maneno ya uchochezi, dharau na kujenga chuki dhidi ya Serikali na Rais.
Akizungumza na mtandao wa Global Publishers baada ya kushinda kesi hiyo, Mtikila amesema “Ushindi huu niliutarajia maana hata asubuhi kabla ya kuja mahakamani niliongea na Yesu na sasa amenijibu”.
Mara baada ya kushinda kesi hiyo lilizuka timbwili lingine baada ya mtu
mmoja kujitokeza akiwa na RB (Report Book) akimtuhumu Mchungaji Mtikila
kuwa alimtishia kumuua na ni mwizi wa viwanja. Baada ya kutaka kukamatwa
na polisi mmoja aliyekuwa na cheo cha Koplo, Mchungaji alikataa kwa
madai kuwa yeye ni kiongozi wa kitaifa hivyo hawezi kukamatwa na polisi
mwenye cheo cha Koplo, labda polisi mwenye cheo cha SSP (Senior
Superintendent of Police). Kwa kauli hiyo polisi alishindwa kumtia
nguvuni.
MKUTANO MKUBWA ULIOFANYIKA KATIKA VIWANJA VYA KWEMBE JIJINI DAR ES SALAAM
MWINJILISTI BWA KIMATAIFA ANDULILE BWILE ALIKUWA AKIHUBIRI NENO LA MUNGU KATIKA MKUTANO WA SIKU SABA KWEMBE
Ni vyema kutii sheria bila shuruti imekuwa ni mojawapo ya njia yav kuwafundisha wananchi kutojichukulia sheria mkononi.
Mwinjilisti Andulile amesema ni vyema wananchi weakatii sheria na kuacha uovu na kumrudia Mungu na hiyo itasaidia sana katika maendeleo ya taifa
Hapa mwinjilisti Andulile akifurahia jambo na wachungaji wenzake madhabahuni
Mwinjilisti Andulile akisoma neno la Mungu wakati akihubiri
Hapo ni maeneo ya kwembe ambapo Magida alikuwa mmoja wa waimbaji katika mkutano wa injili
umati wa watu wakisikiliza neno la Mungu kwa makini likihubiriwa na mwinjilisti Andulile wakiwa na shauku ya kutaka kufahamu kwa undani neno la Mungu
MMOJA WA WAIMBAJI WA NYIMBO ZA INJILI AMBAYE AMEKUWA AKIMBA KATIKA MIKOA MBALIMBALI TANZANIA
Madida Timotheo ni miongoni mwa waimbaji wa nyimbo za injili ambaye amekuwa akishirikiana na wainjilisti mbalimbali kueneza neno la Mungu kwa njia ya uimbaji.
Hata hivyo mwimbaji Magida amewahi kuimba wimbo wa polisi jamii unahusu utii wa sheria bila shuruti kwa kushirikiana na baadhi ya waimbaji wa jeshi la polisi
Hapa ni jukwaani mwimbaji Magida akiwatumbuiza watu waliofika kusikiliza neno la Mungu hawapo pichani |
Hapo anaonesha umahiri wake kwa kuimba huku akipiga magoti
hapa shughuli ilikuwa kubwa mtumishi wa Mungu akiimba kwa staili zote ili watu waweze kumfahamu kristo na kumkubali kama bwana na mwokozi wa maisha yao
Mwenyewe utashuhudia watu walivyojitokeza na kukaa kando ya nyumba zao kuangalia na kufurahia huduma ya uimbaji ambayo Magida alikuwa akitoa
Hivyo ndivyo mtumishi wa kristo alivyokuwa akiwajibika katika jukwaa kuhakikisha kuwa watu wanfikiwa na injili kwa njia ya uimbaji
Mdida akishirikiana na mimbaji Pascal Kasian ambaye alishawahi kuwa mshindi wa bongo star search wakiimba pamoja na Sapula katika jukwaa moja katika mkutano wa injili.
Waimbaji wakisimama mbele ya kanisa kujitambulisha mmoja baada ya mwingi hapa yupo Enock Jonath na vijana wake wawili anaoshirikiana nao akiwa amevaa suti na shart njano ,mwenye microphone ni Pascal Kasian mwenye suruali nyeupe ni Sapula na mwenymiwani meusi na suti na Magida Timotheo,
hapo ilikuwa siku ya jumapili.
hapo ilikuwa siku ya jumapili.