YESU NI JIBU

Ijumaa, 28 Novemba 2014

HATUA SITA AMBAZO UNAWEZA KUTUMIA ILA KUMPATA TENA RAFIKI YAKO WA KWANZA AMBAYE UMEKOSANA (UMEACHANA )NAYE:


MAISHA YA KILA SIKU.
Upendo wa kwanza katika maisha ya kila mtu inaacha nafasi nzuri na kumbukumbu katika maisha ya mtu binafsi.Kama ulishawahi kuachana na rafiki yako wa kwanza ni vigumu ama sio rahisi kuwa naye tena ama kurudisha mahusiano tena naye, ila bado inawezekana kuwa naye katika maisha yako.
Kila mwanadamu kuna kitu anatakiwa kukumbuka na kufuata ni kutokumbuka kitu ambacho kilishawahi kumuumiza hivyo endelea kuufuatilia kwa makini mambo sita ambazo unatakiwa kufahamu ili kumrundisha rafiki yako wa awali ambaye unampenda.
    
 1.Epika kumtafuta kwenye mtandao wa kijamii (Facebook)
Kama hautaweza kuvumilia kutomtafuta rafiki yako(mpenzi)wako ambaye mmekosana au mmetofautiana kwenye mtando wa kijamii Facebook ,basi kuna uwezekano mdogo sana ya kumpata tena.Kwani Itakuwa vigumu kufahamu kuwa anafanya nini? na anaongea na nani anawasiliana na nani kwa muda huo.
Hivyo ni vyema kujitahidi kumfungia katika profile yako maana ataendelea kusababisha maumivu katika maisha yako.

2.Tupilia mbali vitu vyote ambavyo vinaweza kusababisha ukaanza kumkumbuka.
Njia mojawapo nzuri ya kumpata rafiki yako wa kwanza ni kutupilia mbali mambo yote ambayo ulikutendea ndivyo sivyo na hapo unaweza kurudisha upendo wa awali.
Amini usiamini ni lazima utafute njia ya kufuta kumbukumbu yote ambayo alikutendea ndivyo sivyo.Kama mlitumiana ujumbe mfupi,barua pepe wakati mmetofautiana ni vyema kufuta hizo jumbe zote hiyo itakusaidia kumsamehe,ila nji hii inaonekana kuwa ngumu ila ndiyo njia pekee inayoweza kukusaidia kumsamehe na kutokumbuka.  

3. Baadilisha mtazamo wako wa maisha.
Baadala ya kuendelea kufikiria yaliyopita ni vyema ukawaza yali yalioko mbele yako.uwe na tumaini jipya,fanya kazi kwa bidii kuliko kawaida ili kufikia malengo yako.jiweke taratibu ya kujishughulisha  kwa ukichoka kwwa ukweli ni njia ya kusahau yali uliyokosewa ma yule ambaye umekosana naye.

4. Soma habari ambazo zinasababisha faraja kwako.
Soma vitabu vya hadithi ambazo zinaweza kukusaidia kupata furaha ambayo itasaidia kusahau yale yote ambayo ulitendewa.Unaweza kusoma hadithi kwenye majarida,vitabu na hata kwenye mtandaona utambue jinsi wengine walivyotatua matatizo na kutambua kuwa kumpoteza rafiki wako wa kwanza ni jambo la kawaida

5.Fikiria juu mazuri ambayo ulikuwanayo katika mahusiano yako.
Acha kuwa na kumbukumbu mbaya juu ya mahusiano yako ulikuwa nayo badala yake fikiria juu ya mazuri ambayo ulikuwa nayo na rafiki yako.Ni vyema kukumbuka kuwa muda uliyokuwanayo haikuwa bure.

6. Upate muda wa kutosha na marafiki zako.
Kwa kuhitimisha ni vyema kushikishana uzoefu na marafiki zako wa karibu na kusikiliza maoni yao na itakusaidia kujisikia vizuri katika maisha yako.Msaada wao wa kimawazo itakusaidia kujisikia vizuri na kuona kuwa maamuzi uliyochukua nia sahihi na utaanza kumsahau rafiki yako wa mwanzo.
Kama rafiki yako atakuwa naye amepitia kama hayo ambayo umepitia unaweza linganisha na kuona kuwa kumrudisha rafiki yako wa mwanzo(mpenzi) ni jambo ambalo linawezekana.
Nawe msomaji umempataje rafiki yako wa mwanzo Tafadhali tushirikishe.