Apostle Dr Livingstone Banjagala akiongoza waumini katika maombi na maombezi huko Shenzen China
YESU NI JIBU
Jumatatu, 29 Februari 2016
Jumapili, 28 Februari 2016
MWALIMU WA SHULE YA MSINGI MSIGANI APIGWA RISASI WAKATI AKIFUNGA BIASHARA YAKE.
Na Masau Bwire,
Mwalimu wa kike mwenye umri wa miaka 25 wa Shule ya msingi Msigani, Kimara Manispaa ya Kinondoni Jijini Dar es salaam ameuawa kwa kupigwa risasi siku ya Jumamosi saa 2 usiku!
Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Kipolisi Kinondoni, Dar es salaam, Kamishina Msaidizi wa Polisi (ACP) Christopher Sprian Fuime amesema mwalimu huyo aliuawa kwa kupigwa Risasi hiyo wakati akijiandaa kufunga kibanda chake cha biashara kilichopo pembeni mwa uwanja wa Shule anayofundisha.
Kamanda Fuime amesema, wauaji hao ambao walifika katika kibanda cha mwalimu huyo wakiwa wamepakizana kwenye pikipiki, walivunja kioo cha kibanda hicho, mmoja mwenye bastola akaingia ndani na kumpiga Risasi iliyomsababishia kifo papo hapo, kisha wao kuondoka bila kuchukua kitu chochote!
Amesema juu ya meza katika kibanda cha biashara cha mwalimu huyo kulikutwa shilingi laki tatu, vocha za simu na simu kadhaa za mkononi ambazo hazikuguswa na watu hao, hali ambayo inalifanya Jeshi la Polisi lishindwe kubaini kwa haraka mpaka hapo uchunguzi utakapofanyika sababu za mauaji hayo.
Kamanda Fuime amesema, Serikali kupitia Jeshi la Polisi itahakikisha hakuna jambazi anayepata ushindi na kufanya raia waishi kwa hofu katika nchi yao na kuongeza kwamba, kutoa uhai wa mtu kwa ajili ya Mali, chuki na uhasama ni vitendo ambavyo havitavumiliwa na Jeshi la Polisi, litapambana na watu wenye tabia hizo, kuwakamata na kuwafikisha katika vyombo vya dola.
Aidha Kamanda Fuime ametoa mwito kwa wananchi kutoa ushirikiano kwa Jeshi la Polisi ili kuwezesha kupatikana na kukamatwa kwa watu hao na wahalifu wengine.
Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Kipolisi Kinondoni, Dar es salaam, Kamishina Msaidizi wa Polisi (ACP) Christopher Sprian Fuime amesema mwalimu huyo aliuawa kwa kupigwa Risasi hiyo wakati akijiandaa kufunga kibanda chake cha biashara kilichopo pembeni mwa uwanja wa Shule anayofundisha.
Kamanda Fuime amesema, wauaji hao ambao walifika katika kibanda cha mwalimu huyo wakiwa wamepakizana kwenye pikipiki, walivunja kioo cha kibanda hicho, mmoja mwenye bastola akaingia ndani na kumpiga Risasi iliyomsababishia kifo papo hapo, kisha wao kuondoka bila kuchukua kitu chochote!
Amesema juu ya meza katika kibanda cha biashara cha mwalimu huyo kulikutwa shilingi laki tatu, vocha za simu na simu kadhaa za mkononi ambazo hazikuguswa na watu hao, hali ambayo inalifanya Jeshi la Polisi lishindwe kubaini kwa haraka mpaka hapo uchunguzi utakapofanyika sababu za mauaji hayo.
Kamanda Fuime amesema, Serikali kupitia Jeshi la Polisi itahakikisha hakuna jambazi anayepata ushindi na kufanya raia waishi kwa hofu katika nchi yao na kuongeza kwamba, kutoa uhai wa mtu kwa ajili ya Mali, chuki na uhasama ni vitendo ambavyo havitavumiliwa na Jeshi la Polisi, litapambana na watu wenye tabia hizo, kuwakamata na kuwafikisha katika vyombo vya dola.
Aidha Kamanda Fuime ametoa mwito kwa wananchi kutoa ushirikiano kwa Jeshi la Polisi ili kuwezesha kupatikana na kukamatwa kwa watu hao na wahalifu wengine.
Imechapishwa na
Amaninafuraha
kwa
10:34
Hakuna maoni
:
Tuma Hii kwa Barua pepe
Blogu Hii!
Shiriki kwenye Twitter
Shiriki kwenye Facebook
Shiriki kwenye Pinterest
Lebo:
Kamishina Msaidizi wa Polisi (ACP) Christopher Sprian Fuime
,
Kimara
,
Manispaa ya Kinondoni Jijini Dar es salaammwalimu kuuwawa kwa kupigwa risasi
Ijumaa, 26 Februari 2016
FGBF MKURANGA IMEKUANDALIA MKUTANO WA INJILI UNAOENDELEA KATIKA VIWANJA VYA SOKO JIPYA MKURANGA
Mkutano huo watu wengi wamefunguliwa na kuwekwa huru mbali na mateso ya pepo wachafu.
mkutano huo umeandaliwa na kanisa la Full Gospel Bible Fellowship Mkuranga chini ya mchungaji Elineus Mbalilaki.
mkutano huo umeandaliwa na kanisa la Full Gospel Bible Fellowship Mkuranga chini ya mchungaji Elineus Mbalilaki.
Katika mkutano huo wa injili wahubiri mbalimbali watakuwepo kuhubiri neno la Mungu akiwepo mchungaji Steven Mapunda.
Jumapili, 21 Februari 2016
KILA MMOJA ANA NJIA YA KUFIKA MAHALI AMA KUFIKIA MALENGO ILA YESU NI NJIA YA UZIMA NA MILELE BILA YEYE HUWEZI KUMWONA MUNGU.
Askofu Geofrey Masawe askofu wa jimbo la Mashariki Kasakazini na pia ni mchungaji kiongozi wa kanisa la TAG Sahara Spiritual Center
Mwinjisti Kambona Mwansasu Akifundisha somo la Njia ni Yesu katika kanisa la TAG sahara Spiritual Center.Alhamisi, 18 Februari 2016
Jumatano, 17 Februari 2016
MWINJILISTI AWATAKA WANAOJIITA MANABII WAJITOKEZE NDANI YA SIKU 14 KUWAOMBA RADHI WATANZANIA KWA KUWADANGANYAKUWA WAO NI MANABII.
MWINJILISTI DAUDI MASHIMO AKIZUNGUMZA NA WAANDISHI WA HABARI HAWAPO PICHANI KATIKA UKUMBI WA HABARI MAELEZO JIJINI DAR ES SALAAM,
MTUME BETHANIA AMBAYE KATIKA SIKU ZA NYUMBA PICHA ZAKE ZILITEMBEA NA KUZAGAA KUTOKANA NA MFANO ALIOTOA WAKATI AKIFUNDISHA SOMO LA ROHO YA MAUTI NA KUZIMU.
Mtume Bethania akijieleza wakati akihojiwa na blog hii ya amaninafuraha
Watumishi Daniel,Briton na Briton ni Watendakazi pamoja na apostle Bethania ambao walitumika kutoa mfano wa apostle akifundisha somo la SOMO LA ROHO YA MAUTI NA KUZIMU.Jumanne, 16 Februari 2016
Jumapili, 14 Februari 2016
SHIMO LISIFUTE NDOTO YAKO
Siku zote mwenye ndoto hakosi vikwazo, vikwazo vitainuka vingi sana ili kufuta ndoto ya mwenye ndoto maana shetani anajua kuwa ndoto ikifutika tu basi haitoweza kutimia maana nguvu za kutimia kwa ndoto zipo ndani ya mtazamo wa mwenye ndoto kupitia uwezo wa mungu juu ya wakati sahihi uliyoamriwa.