YESU NI JIBU

Jumatano, 30 Septemba 2015

TAMASHA LA KUONGEA NA RAIS MTARAJIWA UWANJA WA ZAMANI WA TAIFA.

Siku ya jumapili iliyoisha katika uwanja wa mpira wa Uhuru zamani kama uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam, kulifanyika tamasha kubwa la uimbaji lenye lengo la kuzungumza kupitia uimbaji na atakayekuwa Rais mtarajiwa wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Tamasha hilo liliandaliwa na kwaya ya Efatha kutoka Uhuru Moravian Kariakoo na kuhudhuriwa na watu mbalimbali pia kwaya hiyo ilitumia wasaa wa tamasha hilo kufanya live Recording yao
Baadhi ya kwaya zilizohudhuria tamasha hilo ni pamoja na Neema Gospel ya AIC Chang'ombe, Uinjilisti Kijitonyama, Eden Tabata Moravian, Uinjilisti Sayuni Kinondoni, Tumaini Shangilieni St James Arusha. Ambapo licha ya mahudhurio kutokuwa makubwa sana kama ilivyokuwa ikitazamiwa lakini watu waliofika waliweza kuburudika na lengo la tamasha hilo kufikiwa na vyombo vilivyotumika kutoleta shida kama matamasha mengi yanayofanyika uwanja wa taifa. 



 Baadhi ya watumishi amabo wamehudhuria katika Tamasha hilo.











NI NANI ANAHUSIKA NA KUCHOMAA MAKANISA MOTO HUKO MKOANI KAGERA NANI WA KUULIZWA NA KULAUMIWA.

Makanisa manne yameteketezwa katika mkoa wa Kagera, na kufikisha saba, idadi ya makanisa yaliyochomwa moto eneo hilo mwezi huu.
Hadi sasa haijabainika ni kundi gani linalohusika na vitendo hivyo, kwa mujibu wa polisi.
Lakini baadhi ya viongozi wa dini wameambia mwandishi wa BBC Leonard Mubali kuwa huenda ni matokeo ya uhasama wa kidini.
Kuchomwa kwa makanisa hayo kumeongeza hofu kwa viongozi wa makanisa na waumini kuhusu usalama wao.
Mchungaji Vedasto Athanasi ni Askofu wa kanisa la Living Water mkoani humo, ambaye kanisa lake limechomwa kwa mara ya tatu sasa, ni mmoja wa walioingiwa na wasiwasi.
“Kitendo hakiwezi kukafanyika mara tatu, na hakuna hatua zinazochukuliwa. Naona ufuatiliaji wa suala hili ni mdogo sana,” amesema.
Mkuu wa mkoa wa Kagera, John Mongela, ameiambia BBC kuwa mazingira ya matukio hayo yana utata kiasi kwamba ni vigumu kutambua mara moja kuwa yana malengo gani.
”Kwa jinsi ambavyo tuliona, hupati shida ya moja kwa moja, ujue kama ni siasa au ni nini. Kwa sababu haya yanafanyika wakati hakuna watu,” amesema.
”Lolote lile ambalo litakuja upande wetu, tutalifanyia kazi na kuona kama litatusaidia katika kutuelekeza.”
Crodward Edward, mwenyekiti wa muungano wa makanisa ya Kipentekoste mkoani Kagera, anasema anaridhishwa na hatua za mamlaka za usalama na kuwataka waumini kuwa watulivu kipindi hiki cha matukio haya.
Je wewe una maoni yako? 

Jumapili, 27 Septemba 2015

ASKOFU RASMI ATANGAZWA NA KIWANGO CHA KURA HUKO DODOMA NA MSIMAMIZI WA UCHAGUZI ASKOFU BATENZI.

 Mshauri mkuu wa kanisa la EAGT mchungaji Anyandile Mwakisyala. 
Na Mwandishi Yonathan Landa
DODOMA.
Hatimaye kitendawili cha Nani kuvaa Viatu vya Askofu Moses Kulola kimeteguliwa leo na Mkutano Mkuu taifa uliotishwa kwa mujibu wa Katiba ya kanisa la Evangelistic Assemblies Of Tanzania hii leo.
Katika Mkutano huo uliokidhi vigezo vya kikatiba umechagua viongozi watakaongoza kanisa hilo kwa muda wa miaka mitano tangu sasa.

 Mmoja wa wachungaji akihesabu kura

Nafasi ya Askofu mkuu iliyokuwa inakaimiwa na Makamu wa Askofu wa Kanisa ndugu Asumwisye Mwaisabila sasa nafasi hiyo amepata mrithi halali wa kupigiwa kura kwa mujibu wa Katiba ambaye ni Mchungaji Brown Mwakipesile aliyeshinda kwa kura 1526 dhidi ya Mchungaji John Mahene alipata kura 726.
Ikumbukwe kuwa Mwakipesile kabla Nafasi hiyo alikuwa ndiye Katibu Mkuu wa Kanisa hilo kwa kipindi kirefu sasa.
Nafasi ya Makamu wa Askofu imeshikiliwa na Mchungaji John Mahene alipata kura 1490 dhidi ya Mpinzani wake Leonard Mwizarubi aliyepata kura 563.


Aidha Nafasi ya Katibu wa Kanisa hilo imechukuliwa na Leonard Mwizarubi kwa ushindi wa kura 1408 dhidi ya Mchungaji Raphael Machimu aliyepata kura 416.

Vilevile nafasi ya mtunza Hazina wa kanisa hilo imekwenda  Kwa Mchungaji Pray-God Mgonja ambaye ameshinda kwa kura 1011 na kumuangusha kwa mbali aliyekuwa anashikilia nafasi hiyo Mchungaji Joshua Wawa kwa kupata kura 566.

Wakati huohuo Mkutano Mkuu kwa pamoja walimpitisha Mshauri Mkuu wa Kanisa hilo ndugu Anyandwile Mwakisyala pasipo kupingwa na mjumbe yeyote kwa kura ya ndiyo kuwa mshauri wao.
Uchaguzi huo uliongozwa na Kamati Maalumu ya PCPT chini ya Mkuu wa kanisa la FPCT Taifa Askofu Batenzi.


 Mshauri mkuu wa kanisa la EAGT mchungaji Anyandile Mwakisyala mwenye kinasa sauti akimpongeza Askofu Leornard Mwizarubi baada ya uchaguzi.


 Picha ya pamoja kati ya viongozi wapya wa kanisa la EAGT na mshauri mkuu.
Wasiliana nasi 0752834514,

Jumatano, 23 Septemba 2015

MRITHI WA VIATU VYA MWANAINJILI ASKOFU DR MOSES KULOLA APATIKANA.

Huyu Ndiye Askofu Mkuu Mteule wa Kanisa la EAGT. Brown Mwakipesile! Ndie Ameshika nafasi ya aliyekuwa Askofu Mkuu Babu Moses Kulola.
Hatimaye mrithi wa kiti cha mwanzilishi wa kanisa la Evangelist Assemblies of God Tanzania (EAGT), Mwanainjili, Dk. Moses Samwel Kulola, aliyemaliza kazi yake na kutwaliwa, atajulikana amejulikana baada ya wachungaji kutoka kila kona ya nchi watakapokutana mjini Dodoma, katika mkutano mkuu utakaomchagua Askofu Mkuu wa Pili wa kanisa hilo la kiroho.
Kiti cha Askofu Mkuu wa EAGT, kimekuwa kikikaimiwa na Makamu Askofu, Asumwisye Mwaisabila, tangu, Askofu Dk. Kulola alipoimaliza kazi, alhamisi Agosti 29, mwaka 2013, na kwa mujibu wa katiba ya kanisa hilo, mwaka huu ni wa uchaguzi na tayari maaandalizi yote yamekamilika.
Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini wa Kanisa la EAGT, Mch. John Henry Mfuko, kuhusu mwelekeo wa uchaguzi, sifa za anayestahili kukikalia kiti hicho na matarajio ya wana-EAGT, katika kipindi hiki muhimu.
Mzee huyu aliyetembea na Askofu Kulola katika safari za Injili wakitaabika nyikani, jangwani na mstuni katika hali zote alisema:
“Tunaelekea Dodoma kumchagua Askofu wa pili wa kanisa letu. Nitaenda Dodoma…lazima niende. Uchaguzi wa wakati huu ni tofauti sana kwa kuwa watu wameomba na tunaendelea kuomba na mkono wa Mungu uko juu yetu.”
Kisha aliongeza: “Si Yesu alisema ombeni nanyi mtapewa, tafuteni nanyi mtapata, bisheni nanyi mtafunguliwa? Tunakwenda kumpata yule aliyestahili kuliongoza kanisa na si kwa mazoea, ni yule ambaye ataliongoza kanisa kulingana na hitaji la sasa.”
Alisema; wakati wao Injili ilienezwa kwa mbinu tofauti na hali ilivyo sasa, wakati huu Kiongozi anayetakiwa wala si kwa kigezo cha elimu tu, bali ni yule atakayeongoza kwa vitendo kulipeleka mbele kanisa na si mtawala.
Mzee huyo wa Injili aliyezaliwa mwaka 1930, alisema kuwa Kiongozi wa anayestahili kuvaa viatu vya Askofu Kulola ni lazima akidhi malengo ya kikatiba ambayo ni kuhubiri Injili ya Yesu Kristo.
Pili; awe mtu atakayeliinua kanisa la EAGT na kuliletea maendeleo ya kiroho na kimwili, badala ya kujinufaisha yeye mwenyewe.
Tatu, awe mtu anayejitolea kuongoza wengine kwa vitendo akijitolea mapato yake kuwasaidia wenzake, sio mtawala ni Kiongozi.
Akasisitiza kuwa Askofu Kulola kamwe hakuwa mtawala bali alikuwa Kiongozi wa watu.
Sifa ya nne; alisema kuwa ni lazima mtu huyo awe ni yule anayeweza kueneza Injili na kuliinua kanisa la EAGT mbele ya jamii kwa njia ya habari, kwani hiyo ndiyo inayoweza kuwafikia mamilioni ya watu kwa dakika chache tu, badala ya watu kujilimbikizia fedha, wakati watu wanakufa dhambini.
Kiongozi huyo mkongwe katika mahojiano hayo yaliyofanyika nyumbani kwake, Temeke, mkabala na Uwanja wa Taifa, jijini Dar es Salaam, alisema kuwa hitaji la Injili kupitia vyombo vya habari ni muhimu sana wakati huu ili kukabiliana na wimbi la Imani potofu ambazo zinaenezwa kwa njia hiyo hiyo ya habari, hivyo kanisa ni lazima litumie vyombo hivyo kupeleka Injili iliyo sahihi.
Akitoa mfano alisema; Askofu Sylvester Gamanywa (WAPO MISSINON INTERNATIONAL) alifanya mkutano Mbeya na kuwafikishia habari mamiloni ya watu kwa muda mfupi sana kupitia vyombo vya habari na hiyo ndiyo Injili ya sasa.
Alipoulizwa nini mtazamo wake kuelekea uchaguzi, mwenyekiti huyo wa bodi ya wadhamini (chombo chenye dhamana ya mali za kanisa) alisema:
“Inaweza kuwashangaza watu sana kwani Mungu atajitwalia Joshua wa kuliongoza kanisa, anaweza kutoka katika kundi lisilotegemewa, kutoka watu wa chini tu ambaye amejitoa na anaonekana kujitolea kulitumikia kusudi la Injili na kuwajali wenzake.”
Alisema Mungu anakanuni zake, hanaangalii vigezo vya wanadamu kama elimu na mambo mengine, Yeye hulitazama kusudio lake, alimuita Petro akiwa mvuvi tu na akawa mtumishi wa Injili.
Alinukuu andiko la Biblia kwenye kitabu cha Matendo ya mitume 4:13; “Basi walipoona ujasiri wa Petro na Yohana, na kujua ya kuwa ni watu wasio na elimu, wasio na maarifa wakastaajabu, wakatambua ya kwamba walikuwa pamoja na Yesu.”
“Kanisa la EAGT, linahitaji Kiongozi mwenye kuwa na Yesu, kama alivyokuwa Askofu Kulola,”alisema kiongozi huyo wa kiroho na kufafanua kuwa Kiongozi hupimwa kwa matendo yake. Kiongozi wetu tunayemtaka ni lazima awe mtu wa kuwarehemu wachungaji wa chini, awakumbatie na kuwasaidia, si kuwaswaga, huku akijilimbikizia mali tena zinazotokana na kanisa la EAGT.
“Wewe si umekuja kwangu, umeona maisha yangu, kanisa langu lipo pale Keko Juu katika ukumbi wa shule, Mungu akinisaidi nikipata kiwanja kingine nitafurahi kanisa likiwa tofauti na ukumbi ule nilioutoa kwa ajili ya ibada bure miaka yote.”
“Mimi nimekuwa mdhamini wa kanisa tangu lilipoanza 1991, vijana wengi tumewapokea wakiwa hawana kitu, lakini leo ni matajiri wakutupwa, wakati kanisa halina maendeleo kama taasisi. Mimi ni mzee na kama wanasema mvi ni hekima basi wasikie wana-EAGT.”
Alisema kuwa uchaguzi wa sasa ni wa tofauti kwa kuwa kwa mara ya kwanza kanisa linafanya uchaguzi bila ya kuwepo kwa mwanzilishi wake, tangu lilipoanzishwa mwaka 1991.

Jumanne, 22 Septemba 2015

DAWA YA KUPUNGUZA MAKALI YA UKIMWI TEMBE MOJA KUTOKA DOLA $13.50 HADI $750.

Kampuni moja ya kutengeza madawa imelazimika kujitetea vikali baada ya kupandisha gharama ya dawa ya Ukimwi kwa asilimia 5,000.
Hii inamaanisha kuwa bei ya tembe moja ya dawa inayotumika kupunguza makali ya ukimwi itapanda kutoka dola $13.50 hadi $750.
Kampuni hiyo inayoitwa Turing Pharmaceuticals imelaumiwa na washika dau wa maswala ya Ukimwi kwa kuongeza bei ya dawa hiyo ya Daraprim ambayo imekuwa mstari wa mbele katika kuimarisha uwezo wa mwili wa mgonjwa aliyeathirika kupigana na maambukizi mapya.
Turing Pharmaceuticals ilinunua hati miliki ya dawa hiyo ya Daraprim mwezi uliopita Agosti.
Mkurugenzi mkuu wa kampuni hiyo Martin Shkreli amenukuliwa akisema kuwa faida itakapatikana baada ya mauzo ya dawa hiyo itasaidia kugharamia utafiti wa dawa mpya na zenye ubora zaidi.
Tembe moja ya dawa hiyo ya Daraprim inagharimu dola moja pekee kutengeneza.
Hata hivyo bwana Martin Shkreli anasema kuwa bei hiyo haijumuishi gharama ya kunadi dawa hiyo wala usambazaji wake ilihali gharama imeimarika maradufu katika miaka ya hivi punde.
''Katika siku za hivi punde dawa za kupunguza makali ya saratani zinagharimu dola laki moja (100,000) ilhali gharama yake asili inaweza kugharimu dola nusu milioni.
Daraprim inauzwa kwa bei nafuu zaidi ikilinganishwa na dawa zinazotibu magonjwa sawa.
Shkreli aliiambia runinga ya Bloomberg katika mahojiano ya kibinafsi.
Shkreli alimsuta mwandishi mmoja wa habari kupitia mtandao wa Kijamii akimuita kuwa ''mjinga'' kwa kutaka kujua kwanini kampuni yake ilikuwa inaongeza maradufu bei ya dawa hiyo muhimu katika vita dhidi ya Ukimwi haswa katika mataifa maskini duniani.
 Daktari Wendy Armstrong kutoka muungano wa wauguzi nchini Marekani HIV Medicine Association amekashifu sababu zilizotolewa kwaajili ya nyongeza hiyo kubwa ya bei ya dawa hiyo.
Muaniaji tikiti cha urais wa chama cha Democratic Hillary Clinton ameonya kuwa serikali yake itachukua hatua kali dhidi ya makampuni yanayofaidi kutokana na msiba wa watu kwa kupandisha bei ya madawa maalum.
Source BBC.

Alhamisi, 17 Septemba 2015

MAPINDUZI YA KIJESHI YAFANYIKA HUKO BURKINA FASSO

Yametokea mapinduzi nchini  Burkina Fasso, Afrika Magharibi ambako jeshi limevunja serikali ya mpito ya nchi hiyo na kutwaa madaraka.
 Kwa mujibu wa afisa mmoja wa jeshi aliyezungumza kwenye runinga ya nchi hiyo, Rais wa mpito Bwana MICHEL KAAFANDO amepokonywa madaraka bila kutoa maelezo zaidi.
Hatua hiyo imekuja baada ya Bwana KAFANDO na Waziri Mkuu wake Bwana ISAAC  ZIDA na baadhi ya mawaziri kukamatwa wakati kikao cha baraza la mawaziri na wanajeshi watiifu wa wa zamani, Bwana BLAISE COMPAORE aliyejiuzulu mwaka jana kufuatia maandamano dhidi yake.

Kukamatwa kwao kumelaaniwa vikali ndani na nje, huku jumuiya ya kimataifa kupitia Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa,  Bwana BAN KI-MOON,  ukitaka waachiliwe mara moja na Marekani imelaani jaribio lolote la kutwaa madaraka kinyume na katiba au kuondoa tofauti za siasa kwa kutumia jeshi.

JIFUNZE NA KUFAHAMU AINA TATU ZA MABABA WA KIROHO DUNIANI.

 (1Wakoritho 4:15) Imeandikwa=Ijapokua mna waalimu kumi elfu katika Kristo walakini hamna MABABA wengi, Maana mimi (Paulo) ndio nilio wa zaa kwa Injili.
BABA WAKIROHO NI YUPI?
Baba wa kiroho,sio yule aliye kuongoza heti sala ya Toba,sio kweli,hilo hata washirika wangu wana wasaidia watu kuwaunganisha na Mungu,kwa kuwaongoza ukili wa kutubu dhambi,baada ya kuwashuhudia habari za Mwokozi Yesu.
Wakimaliza huwaleta kanisani,na Mimi ninawazaa kwa ile Injili yangu ya Ukombozi wa Roho,nafsi,na Mwili,na wanakua watoto wangu wa Kiroho,lakini sala ya Toba waliongozwa na mtenda kazi tu na sio mimi.
Hivyo BABA wa KIROHO ni yule ambaye injili yake uliielewa na kuipenda,na ukaamua kuomba au ukajikuta unamfuata wewe mwenyewe ili akuongoze,wewe unakua mtoto kwake,na yeye anakua BABA WA KIROHO,na tokea hapo anaanza kudili ma maisha yako,sio KIROHO tu hata kimwili na kukuchonga kitabia,kwa kukufundisha,kukuonya,kukuelekeza,kukukemea popote,maana umemkabidhi uskani akuongoze,nawewe una wajibu kusikia,kuelewa na kutii,kwa anaye kuongoza.
AINA 3 ZA MABABA KIROHO NI ZIPI?
(Luka 10:30-37) 
=Huyu ni mshirika aliyekua anasafiri safari,lakini njia moja na viongozi wa Kiroho au MABABA WA KIROHO,na tena kwa bahati zuri yeye mshirika alikua mbele katangulia.
Ghafla akatokewa na wahuni,wakampiga na kumjeruhi vibaya akawa amezimia nusu ya kufa,na kila alicho kua nacho kilipolwa na vibaka wale. Nakusudi la MAONO yake ya mwendo wa kutoka Yerusalemu kwenda Yeriko ilikua,imekwamia pale.
MABABA 3 KATIKA NJIA MOJA.
Kwa Neena za Mungu,kabla hujatimiza kusudi la wewe kuepo hapa Duniani huwezi kufa,japo waweza kuteseka sana,katika kufikia kusudi lako.
(1) Ndipo akapita njia ile BABA wa kwanza,jina laki ni kuhani,au askofu leo akapita pembeni kabisa,ya huyu muumini aliye mahututi. Jamii ya Baba kama huyu,ndio wale ambao hukufurahia tu,ukiwa kanisani!! Unatoa zaka! Unaleta watu church!! Unaimba Praise!! Kama ni Bishop yeye huflahia tu wakati upo una chunga kituo cha kanisa lake,ukiwa na hatari za Mateso au ukifa!! Wanakuja church na kumfukuza mke wako na watoto, na pale church analetwa mchungaji wa kabila lake Bishop,tumeyaona hayo.
(2) Huyo Kuhani alipo pita pembeni ya mshirika,aliye mahututi, Ndipo tena akaja mlawi (Pastor) Naye ndio wale wale tu,wachungaji wa pesa (Mshahara)vikumi tu wakati ni mzima,huyu naye akalihepa tatizo la mshirika. Huyu namfananisha kama wale maaskofu,ambao ili uende kuombewa,ajabu na kweli unatozwa,kiasi flani cha pesa au kima,utazani unaenda kutazamiwa Ramri kwa mganga.
(3) Huyu wa tatu ndio BABA WA KIROHO WA KWELI, ambaye mimi na wewe tungependa kumfuata bila shaka yoyote.
Maana anatabia za kiungu kabisa,anaitwa BABA MSAMARIA YEYE ANATAMANI UWE NA MWENDO,KATIKA MAONO YAKO, hatamani kuona maono au makusudi yako yanafia njiani,kama anavyo amini my Senior Apostle Vincent Mkalla (Mdo 13:36)
KUMJUA BABA WA KWELI:
@ Akamwona akamuonea huruma.
@Alimfunga jeraha zake zote.
@Alikua na MAFUTA na divai akampaka.
@Akampandisha juu ya Punda wake.
@Akaenda kumpeleka kwenye nyumba ya wageni,akimhudumia kwa mali zake,au pesa tuseme,na sio kwa kunena kwa lugha mpya usiyo ijua,hapo ilikua moyo wa kulea na pesa ya Baba ndio inaongea.
@Bado tunasoma siku yapili,na zingine aliendelea kuja mpaka alipo kua amepona kabisaa.
@Biblia inatuonyesha alikua jirani naye, na tena Yesu anauliza katika hawa mababa wa kiroho 3 ni yupi aliyekua jirani yake? Wanaitika bila aibu ni Yule aliyo muonea Huruma,wakaambiwa nanyi fanyeni hivyo kama yule wa tatu.
PIGA PICTURE MABABA WENGI LEO WALIVYO.
@ Mtu mmoja aliwahi kuniambia,Apostle Bethania Simon mimi Baba yangu wa kiroho ni Nabii T.b Joshua,sababu zake sasa,heti siku moja alikua anamuangalia kwenye Tv akasema pokeeeaaaa basi alipo sema hivyo,huku anatunyoshea Mkono,mimi nikaanguka puuuuu chaliii,na toka siku hiyo akawa Baba yangu wa Kiroho. Mimi nikamwambia tu unapotea kwa kukosa ufahamu na akili nzuri za kiungu,maana hiyo siyo saini ya kua nibaba yako kiroho nk.
MABABA wengi leo wanaojiita,kua ni MABABA Hawana kabisa, moyo wa Kristo masiya.
Wengi hupenda kujipachika ubaba,wakati wao Bado ni watoto,ama Bado wana tabia za Kipagani,na utozi tozi tu,wakidhania huduma ni cheo,kama Meneja,au mhasibu.
Watu kadhaa wasio jitambua,na limbukeni wa kulewa heshima,za uanafunzi. Walikuja kuhubiri hapa church,na ikawa kawaida sana tu,cha ajabu na kweli ghafla unasikia mtu anatangaza Bethania ni Mwanangu wa Kiroho,Basi nacheeka tu kwakua yeye ndio kaongea ili apate sifa kupitia mimi kamanda wa vita, lakini nilijiuliza Ebo hivi!! Paka anaweza kumuongoza Simba? Au mjusi kafiri amuongoze,Mamba kweli? Teh tehe..Au mtu mwenye Roho wa Mungu aongozwe na mtu mwenye Roho mtakafedha?
DALILI ZA BABA ASIYEKUFAA KIROHO.
1.Ana Penda sana pesa na mali zako,kuliko kuku saidia usimame.
2.Anaye kuogopa kukushauri vizuri,ili usihame kanisa.
3.Anaye kutafutia tu madhaifu yako ili apate cha kuku hukumu.
4.Unapo muadithia usiri wako,yeye anakuhubiri madhabahuni j.p.
5.Ambaye mahubiri yake mengi,yamejaa kuitisha tu pesa,na kujisifu saana yeye.
6.Baba ambaye hakei kemei dhambi,kama vile Uzinifu nk Ogopa sana mtu anaye jilinda sana kwa mabaunsa,au kwa maneno yake,utasikia anahubiri,mimi mshirika anaye nisema vibaya atapata laana,na kufa ghafla,au nitayarudisha mapepo,na nagonjwa nilio yatoa, ukiona hivyo jua ndio wale waleeee.
7.Baba ambaye kwenye mapito yako,anajitenga nawewe,na anatoa tu visababu,oo lbd atakua amezini,au kanisema vibaya hivyo kapigwa huyu.
8.Mtumishi ambaye Mahubiri yake yamejaa,KUHUKUMU NA KUSHUSHA WATUMISHI WENGINE,NA KUWAZUSHIA UONGO,hapo kimbia  haraka.
9.Mtumishi anayeombea huku anakupapasa,maeneo Nyeti mwilini,hapo kimbia,maana kifuatachoni ni hatari .
10.Baba asiye tubisha watu,au kuhubiri wakovu na msamaha wa dhambi.
11.Pia jiepushe na Baba anayechukia na kuwa na uchungu,kwa watumishi wengine wanavyofanikiwa.Huyo ana Roho au mzimu wa umaskini,mkimbie haraka.
12.Baba anaye tumia sadaka au mbegu,kuhonga na kulala na makahaba,au hutumia kwa kulewa nk ukigungua kimbia huduma hiyo na umtafute baba wa kweli ambaye atakusaidia kuona mbingu,maana alivyo Baba ndiyo atakavyo kuwa mwanaye..ni mengi sana.
Unaweza kuwasiliana na Apostle Bethania kwa namba +255715 79 66 67. 
Unaweza kuwasiliana na blo hii kwa namba 0682672828.

Jumanne, 15 Septemba 2015

MANENO YA SHIKRANI KWA MTUMISHI WA MUNGU ENCY JACKSON MWALUKASA BAADA YA KUFIKA SIKU YA KUKUMBUKA KUZALIWA KWAKE.

 "Zaburi 92:1 ni neno jema kumshukuru bwana nà kuliimbia jina lake takatifu"aliyenisaidia nà kuniruhusu nifikie birthday yangu mwaka 2015 sept 15. Asante mungu kunilinda na kunitia nguvu na faraja hadi kufikia leo .katika miaka 30 ya kukutumikia .
Nawashukuru wote familia yangu ndugu marafiki na watumishi mlionisaidia 1: kumwimbia mungu vema 2: kuhubiri injili 3:kufundisha neno 4: kufundisha sifa nà kuabudu 5: kuhamasisha wanawake wainuke 6: kusaidia watoto yatima , vijana kiuchumi na wagonjwa. 7:kusaidia wachungaji kufungua makanisa nà kuyàjenga ktk imani 8: umisheni kwa mataifa 9: na kuchungà kondoo wa kanisa la lactan. 10. Kuwa mke mwema na mama wa watoto. Si kwa nguvu za kibinadamu ni kwa roho wa bwana nasema mungu ni ebeneza.

Hili ndilo ombi lake kwa mungu"Nàomba Mungu anisaidie kuingojea na Ile ndoto awamu ya pili ambayo imenigharimu kufa kwa muda na kupoteza yote ili nije nipate ya utukufu baadaye ninaomba nimalize wito wangu kwa ushindi". 

Alhamisi, 10 Septemba 2015

PAPA FRANCIS ANATARAJIA KUBADILISHA UTARATIBU AMBAYO UTAWARUHUSU WAFUASI WA KANISA KATOLIKI WALIOOA NA KUTOA TALAKA NA KUOLEWA TENA WAENDELEE KUWA WASHIRIKA WA KANISA HILO.

Papa Francis anatarajia kurahisisha taratibu zinazoruhusu wafuasi wa kanisa katoliki waliooana kutoa talaka na kuolewa tena huku wakibakia kuwa wafuasi wa katika kanisa hilo .
Maelezo ya taratibu hizo yanatarajiwa kutangazwa mjini Vatcan baadaye .
Papa aliunda tume ya wanasheria wa kanisa mwaka jana kupiga msasa mbinu ya kurekebisha taratibu hizo zinazoruhusu wanandoa kuachana na kupunguza gharama .
papa aliunda tume ya wanasheria wa kanisa mwaka jana kupiga msasa.
Bila sheria hiyo wanandoa wa kikatoliki wanaotalikiana na kuolewa upya hutazamwa kama wazinifu na hawaruhusiwi kupokea komunio.
Mwandishi wa BBC mjini Vatican anasema kuwa Papa Francis hatabadilisha mafunzo ya katoliki kuhusu kuachana kwa wanandoa , lakini atawezesha kurahisisha wanandoa wenye matatizo kuthibitisha kuwa ndoa yao haikuwa ya maana tangu mwanzo,
 na hapa Tanzania waumini wanamaoni gani.
Uamuzi wa Papa Francis kulegeza masharti ya utaratibu wa kubatilisha ndoa kwa waumini wa kanisa hilo umepokewa kwa hisia tofauti.
Uamuzi wa kuondoa urasimu katika ubatilishwaji wa ndoa ulitangazwa juzi na makao makuu ya Papa. Kesi zinazohusu maombi ya ubatilishaji ndoa sasa zitachukua muda mfupi zaidi na mchakato wake hautakuwa na urasimu kama ilivyokuwa awali.
Baadhi ya viongozi wa kanisa hilo na waumini waliozungumza na Mwananchi wameupongeza uamuzi huo kuwa unazingatia mazingira halisi ya kanisa hilo kwa sasa.
Askofu msaidizi wa Jimbo la Bukoba, Methodius Kilaini ameueleza uamuzi huo kuwa utaharakisha utendaji wa kazi za kanisa kwa kupunguza muda wa kusikiliza mashauri hayo na kuyapatia ufumbuzi. “Ni uamuzi mzuri unaoonyesha kwamba kiongozi huyo ana imani na maaskofu wake,” alisema Askofu Kilaini
Kwa upande wake, Padri Evodius Nachenga wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam alieleza kuwa kwa uamuzi huo, matatizo baina ya wanandoa yatakuwa rahisi kupatiwa mwafaka.
Mlei mmoja, John Lipingu alisema kuwa ni hatua nzuri kwa kuwa kanisa hilo limeangalia sheria na kanuni ambazo zimetumika karibu miaka 2,000 ambazo zimekuwa haziendani na hali halisi.
Papa Francis kupitia jopo la wataalamu wa sheria za kanisa na theolojia alipitisha sheria inayolegeza masharti ya kubatilishwa kwa ndoa, ambayo yamekuwa yakitumika tangu mwaka 1908.
Sheria hizo, ambazo zilipitishwa mwaka 1740 zimekuwa zikitaka masuala hayo kujadiliwa kwa ngazi ya jimbo, kupitia mahakama maalumu ya kanisa hilo, kisha mapendekezo kufikishwa makao makuu ya kanisa hilo, Vatican kwa uamuzi.
Hata hivyo, gharama za kufikisha shauri husika Vatican zilikuwa kubwa na utaratibu huo ukichukua muda mrefu na kuwaathiri wanandoa ambao wengine walikosa fedha za kufanya hivyo.
chanzo Mwananchi

Ijumaa, 4 Septemba 2015

KARANI KUFUNGWA JELA KWA KUKATAA KUTOA VYETI VYA NDOA KWA WATU WA JINSIA MOJA HUKO NCHINI MAREKANI.

Karani mmoja anayefanya kazi serikalini, amefungwa jela nchini Marekani kwa kukataa kutoa vyeti vya ndoa kwa watu wa jinsia moja.
Karani huyo, Kim Davis, anayefanya kazi kwenye jimbo la Kentucky, amesema hawezi kuruhusu watu wa jinsia moja kuoana, kwani hilo linakwenda kinyume na imani yake ya Kikristo.
Jaji aliyesimamia kesi ya Kim Davis amesema mshtakiwa amekiuka sheria ya Marekani ambayo sasa inaruhusu watu wa jinsia moja katika majimbo yote kufunga ndoa.
Aidha, jaji huyo amewataka wasaidizi wa Davis waahidi kwamba watatoa leseni za kufungisha watu ndoa, hata kama ni wa jinsia moja.
Ikulu ya Marekani imeunga mkono uamuzi wa mahakama, ikisema hakuna mtu aliye juu ya sheria.
Sheria ya kuhalalisha ndoa za watu wa jinsia moja ilipitishwa miezi miwili iliyopita. 

 chanzo ni DW.

ASKOFU MUSTAAFU KUTOKA AFRIKA KUSINI, DESMOND TUTU, AMERUHUSIWA KUREJEA NYUMBANI KUTOKA HOSPITALINI, AMBAPO AMELAZWA KWA ZAIDI YA WIKI MBILI ZILIZOPITA.

Kwa mujibu wa wakfu wake, Tutu alikuwa akiugua maambukizi yaliyokuwa yamemkumba kwa mara kadhaa.
Mshindi huyo wa tuzo ya amani ya nobel mwenye umri wa miaka 83, amekuwa na matatizo ya kiafya katika miezi ya hivi karibuni.
Hivi majuzi alilazwa hospitalini kutokana na maambukizi yaliyosababishwa na saratani ya tezi dume aliyokuwa akiugua.
Askofu tutu alistaafu rasmi mwaka wa 2011, lakini bado angali anasafiri kwa shughuli mbali mbali.
Taarifa iliyotolewa na wakfu wake ilisema kuwa Askofu huyo mstaafu amewashukuru wafanyakazi wa hospitali ya Cape Town kwa kumhudumia vyema.
Aidha alitoa shukrani kwa raia wa nchi hiyo kwa kumkumbuka kwa maombi yao na risala za heri njema.
chanzo BBC


Jumatano, 2 Septemba 2015

MAKAMU WA RAIS WA BARAZA LA MAASKOFU WA KATOLIKI TANZANIA (TEC) AMTAKA DR SLAA KUTOA USHAHIDI WA MADAI ALIYOYATOA JUU YA KUHONGWA KWA MAASKOFU WA KANISA HILO.

Makamu wa Rais wa Baraza la Maaskofu wa Kanisa Katoliki Tanzania (TEC), Askofu Severin Niwemugizi, amemtaka Dk. Slaa kutoa ushahidi wa madai yake kuwa maaskofu wa kanisa hilo wamehongwa na Edward Lowassa. Akizungumza na MTANZANIA kwa simu yake ya mkononi, Askofu Niwemugizi alieleza kushangazwa na tuhuma hizo zilizotolewa na Dk. Slaa dhidi ya maaskofu bila uthibitisho. “Hizo taarifa ndiyo nazisikia kwako, lakini kama kweli amesema hivyo kwa nini hakuweka ushahidi kuanzia majina ya maaskofu hao waliopewa fedha, kiasi na zilikopokelewa. Lakini kwa upande wangu binafsi sijapokea kiasi chochote kutoka kwa mtu yeyote. Askofu Niwemugizi alimtaka Dk. Slaa kutoa uthibitisho wa maaskofu wa kanisa hilo kupokea fedha kutoka kwa Lowassa waweze kutoa uamuzi. source: MTANZANIA

TINDU LISSU AJITOKEZA NA KUJIBU BAADHI YA YALE AMBAYO DR SLAA AMESEMA NDIYO KILICHOSABABISHA AAJIUZULU SIASA ILA ATABAKI KUWATUMIKIA WANANCHI.

Dr Slaa akizungumza na waandishi wa habari katika hoteli ya Serena jijini Dar es salaam.
Akihojiwa na redio station  redio Sauti ya Amerika VOA, Tundu amedai Dr Slaa ndio alihusika kufanya mpango wa kumkaribisha mgombea Urais wa UKAWA Edward Lowassa CHADEMA na si vinginevyo. mh.Lissu anasema ameshangaa sana maneno aliyoyasema Dr Slaa  kwenye mkutano wake na waandishi wa habari.

Anasema Dr.Slaa alikwisha kuteuliwa kuwa mgombea urais mwezi January na mwezi April akathibitishwa na kamati kuu,

Anaendelea kusema ameshangaa Dr.Slaa kusema Gwajima ndo alimleta Lowassa jambo ambalo siyo kweli kabisa, yeye Dr. Slaa mwezi wa tano ndo alianza kumtafuta Lowassa kwa kumtumia Gwajima

Anasema wakati Lowassa anapokelewa tarehe 27 July kwenye Kamati Kuu, Dr.Slaa hakulala nyumbani aliporudi nyumbani mchumba wake alimtupia mabegi nje na DR. alilala kwenye gari.

Anasema dr. slaa asiwadanganye watanzania tatizo ni urais na mchumba wake.

Anasema ameacha siasa tangu siku ya kikao cha kamati kuu alipoandika barua ya kujiudhuru kwa nini amepokea mshahara wa mwezi huu?? kwanini anaendelea kutumia gari la chama la katibu mkuu na nyumba aliyonunuliwa na chama muulizeni awaambie kwanini anaendelea kunufaika na hayo yote toka CHADEMA???

Jumanne, 1 Septemba 2015

UZINDUZI WA VITABU VITATU KWA PAMOJA AMBAYO "MJUE MWANAMKE, USIIPE HOFU NAFASI NA RAFIKI ANAYEKUFAA, VILIVYOANDIKWA NA MWALIMU LILIAN NDEGI.

Uzinduzi wa vitabi vitatu ambavyo vimeandikwa na mwalimu lilian Ndegi ambaye ni mke wa mchungaji kiongozi wa kanisa la Living water makuti lililopo Kawe jijini Dar es salaam.
hivi ndivyo vitabu ambavyo ameandika mwalimu Lilian Ndegi.
Uzinduzi huo umefanyika katika kanisa la  Living Water Center Makuti Kawe, tarehe 30/08/2015 katika Ibada maalum ambayo imeongozwa na Apostle Onesmo Ndegi, 
Mgeni rasmi katika uzinduzi huo ni Mheshimiwa Paul Makonda, Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni. 



Mkuu wa wilaya mhe. Paul Makonda akijiandaa kuzindua vitabu vilivyoandikwa na mwl Lialian.





Uzinduzi tayari umefanywa na mkuu wa wilaya.

Awali mkuu wa wilaya ya Kinondoni Paul Makonda akiwasili katika kanisa la Living water Kawe.
Mwl Lilian Ndegi akikata keki tayari kuwalisha watu waliohudhuria katika uzinduzi wa vitabu ambavyo ameviandika.


Mwl Lilian Ndegi akimlisha mkuu wa wilaya ya Kinondoni keki.



Mtume Onesmo Ndegi akimlisha mke wake mwl Lilian keki.








Mwimbaji wa nyimbo za Injili Upendo Nkone akiimba katika uzinduzi huo.


 Waumini ambao wamehuduria katika uzinduzi wa vitabu vya mwl Lilian.