YESU NI JIBU

Ijumaa, 14 Desemba 2012

MWIMBAJI WA NYIMBO ZA INJILI MAGIDA AKIZUNGUMZA JAMBO NA MHE.RAIS JAKAYA KIKWETE

Madiga Timotheo ni mmoja wa waimbaji wa nyimbo za injili wa hapa nchini Tanzania,amekuwa akishirikiana na jeshi la polisi katika kuhamasisha juu ya ulinzi shirikishi ambayo imekuwa ikisaidia sana kuwafichua wahalifu mbalimbali.
Amekuwa pia akihudumu kwenye makongamano mbalimbali ya injili katika sehemu mbalimbali hapa nchini Tanzania akitumika kueneza injili ya Yesu na pia amekuwa akishiriki shughuli mbalimbali za kiserikali.na pia unaweza kuwasiliana naye kwa shughuli mbalimbali kama mikutano ya injili semina tumia namba  0752187043 na 0714267875.

Jumapili, 9 Desemba 2012

Hatuwezi kuzuia mfumuko wa “imani Potofu” hata kama zina madhara kiimani




Tafsiri mpya ya msamiati wa “Imani potofu”

Siku hizi jamii imeanza kuchanganyikiwa na kile kinachoitwa “kuongezeka kwa imani potofu” zenye kudanganya na kuathiri imani za wengi kiitikadi.
Kutokana na uchunguzi wangu binafsi, nimekuja kubaini kwamba, mahali tulipofikia kumbe tafsiri yake ina utata mkubwa na maana nyingi tena tofauti hata kama matamshi ni yale yale. Ninachotaka kuelezea hapa ni kwamba, kila inayoitwa “imani potofu” na wengine, kumbe nayo inaziona imani nyingine nje yake ndizo zimepotoka! Kwa maelezo mengine, tumefikia mahali ambapo “Usahihi” wa imani yako ni “upotofu” wa imani kwa mwingine aliye tofauti na wewe kiitikadi. 
Ni kutokana na utata huu, Mamlaka za nchi mbali mbali duniani zilifikia hatua za ama kupiga marufuku “imani zote” na kubakia dini moja au chache zinazokubalika. Kisha baadaye ikaonekana huu ni udikteta usiotenda haki kwa binadamu  na hivyo likaanzishwa “Tamko la Haki za binadamu ulimwenguni” ambalo pamoja na mambo mengine limejumuisha “haki ya kuabudu” na kujiunga au kubadili dini. Kwa mujibu wa tamko hili fursa imetolewa kuwepo kwa imani nyingi, zilizopo hivi sasa, na kuanzishwa mpya, ili mradi mtu havunji sheria za nchi
Kwa kupitia haki ya uhuru wa kueneza imani, kila mtu anapata fursa ya kuchagua au kuacha, kujitenga au kujiunga na imani ile ambayo anaiona ndiyo sahihi kwa uelewa na utashi wake binafsi. Kwetu sisi Tanzania, uhuru wa kuabudu ni haki ya kikatiba.
Baada ya kutoa maelezo ya msingi kuhusu utata wa tafsiri ya “Imani potofu”; naomba sasa nije kwenye kuwasilisha tafsiri mpya ya msamiati wa “Imani potofu”. Tafsiri hii kwa hivi sasa ndiyo inayotumika na sehemu kubwa ya jamii. Tafsiri yenyewe ni kama ifuatavyo:
 “imani yoyote inayokera imani nyingine; na inapata umaarufu mkubwa kiasi cha kuwa tishio la kuvutia wafuasi wa imani nyingine kujiunga nayo”
Imani hiyo inaweza kuwa ni sahihi au potofu kulingana na mtazamo wa kila mtu kwa itikadi yake, lakini kigezo kinachozingatiwa katika kuibatiza jina la “Imani potofu”; ni pale ambapo “wafuasi wengi wa imani za dini nyingine wanaondoka au kuyahama madhehebu yao na kujiunga na imani hiyo” ! Katika harakati za kujaribu kudhibiti matishio ya imani hiyo, na kuwakinga waumini wao wasijiunge nayo ni kuitangaza rasmi kuwa ni “imani potofu”
Naomba nijihami mapema msomaji kwa kusema kwamba, kwa kusema haya sina nia ya kuhalalisha “Imani potofu” kupitia mada hii. Naomba nisieleweke kwamba sio kila “imani inayoshawishi maelefu ya watu kujiunga nayo ni sahihi au ni potofu”.
Hoja ninayotaka kuiweka bayana ni kuhoji uhalali wa matumizi ya kigezo cha “ushawishi na umaarufu mkubwa” kutafsiriwa kuwa imani husika ni potofu kwa sababu hiyo tu! Ingelikuwa kigezo hiki kina mantiki, basi tungeweza kutilia mashaka imani zote zenye wafuasi wengi kuwa zimefanikiwa kwa sababu nazo ni “imani potofu”!
Mtazamo wangu, na uzoefu wangu binafsi, imani zote, ziwe potofu au sahihi, ziwe mpya au za zamani, zote zikiweka bidii kikamilifu katika kujieneza kwa jamii zinaweza kuwa na wafuasi wengine pasipo kujali sana usahihi au upotofu wake kiitikadi. Lakini naweza kukubali kwa sehemu kwamba usahihi au upotofu wa imani unaweza kuchangia kwa kiasi fulani kufuatwa na wafuasi wengine kwa kutegemea ni mbinu gani ya kimawasiliano inayotumika.



Dhana ya imani potofu kuwa na
wafuasi wengi kuliko imani sahihi

Baada ya kuelezea tafsiri ya msamiati wa imani potofu kwamba ni ushawishi na umaarufu wa kupata wafuasi wengi kwa haraka; na baada ya kubainisha waziwazi kwamba nia ni kujaribu kuwakinga waamini wasihame na kujiunga na imani inayovuma kwa wakati husika; sasa nije kwenye chimbuko la tafsiri hii iliyoshika hatamu katika jamii.
Kwa karne nyingi imekuwepo dhana kwamba, imani potofu ina uwezo wa kuwa na wafuasi wengi kwa sababu zimetokana na Shetani mwenyewe. Tena yapo na maandiko yatumikayo katika kusimamia dhana hii ua kwamba hata Yesu mwenyewe alitabiri juu ya manabii wa uongo ambayo watadanganya wengi. (Math…….) Maandiko mengine ni ya mitume akina Petro na Paulo yaliyolitahadharisha kanisa kwamba watakuwepo mitume na manabii wa uongo ambao watatengeneza wafuasi wengi kwa ushawishi na udanganyifu wao.
Kwanza kabisa, naomba kuthibitisha kwamba ni kweli imani potofu zinapata wafuasi wengi kwa sababu zimejaa udanganyifu wa Shetani. Tena naweza kuongezea uzito katika hoja hii kwa kusema kwamba, kinachofanya imani potofu kupata wafuasi wengi ni kwa sababu hazina masharti yenye maadili ya kiungu, na zimejaa uwashiwi unaohamasisha tamaa binafsi au wanaotafuta msaada binafsi.
Lakini, ninapenda kuzungumuzia udhaifu wa dhana hii. Sio kweli hata kidogo kwamba, imani sahihi haipati wafuasi wengi kwa sababu yenyewe ndiyo imetokana na Mungu wa kweli. Ingelikuwa hii ndiyo maana sahihi, basi Yesu Kristo mwenyewe, enzi za mwili wake duniani, asingefuatwa na makumi elfu ya wafuasi wengi! Maneno yake na mafundisho yake yalikuwa magumu na mifano mingi ilikuwa na mafumbo lakini bado umati mkubwa wa watu ulimfuata na kumsikiliza na kushuhudia kwamba huyu ni Mwalimu kweli kweli!
Kana kwamba hii haitoshi, baada ya kufufuka na kupaa kwake, mitume wake nao walitengeneza maelfu ya wafuasi na wanafunzi wengi kama ilivyokuwa nyakati za Yesu mwenyewe. Kanisa la kwanza lilianza kwa kishindo cha wafuasi 3000 kwa siku moja na katika muda wa miaka 40 mfululizo lilikuwa na wafuasi wasiopungua 30,000 wanaokusanyika kwa wiki jijini Yerusalemu!
Ni nini ninachotaka kusema hapa? Napenda kuweka bayana ukweli huu, kwamba hata “Imani sahihi katika Kristo”, kama kweli kweli ikihubiriwa kwa usahihi kama Yesu na mitume wake wa kwanza; kazi zile zile zilizofanyika enzi za karne ya kwanza pia zitatendeka hata sasa. Kwa matokeo hayo makumi elfu ya watu wataikimbilia imani hii kwa wingi kama ilivyokuwa karne ya kwanza.
 Pamoja na ukweli kwamba “Imani potofu” zina ushawishi wa kupata wafuasi wengi; lakini sio kwamba hao wafuasi wenyewe hutoka kwenye imani sahihi na kisha kuijunga na imani potofu! Wengi wao hawakuwahi hata kuijua “imani sahihi” tangu kuzaliwa kwao na ndio maana ni rahisi kwao kujiunga na imani nyingine potofu!
Kwanini imani potofu zimeruhusiwa
kuwepo sambamba na imani sahihi?

Kitu ambacho kinatatiza watu wengi na hasa wale ambao ni wapenzi wa imani sahihi, ni kuona jinsi ambavyo imani potofu zinaendelea kufumuka na kuendelea kupoteza wafuasi wengine wasioijua au kuwa na imani sahihi. Wengine wanafunga na kuomba wakijaribu kudhibiti ongezeko la imani potofu. Hata hivyo, ukweli halisi bado imani potofu zinaongezeka kila siku.

Ningependa kujibu swali hili gumu kwanza kwa kutahadharisha athari zitokanazo na shinikizo la kutumia nguvu za dola kudhibiti imani potofu. Kujaribu kudhibiti mfumuko wa imani potofu kupitia nguvu za Dola, kwanza ni kinyume cha katiba na tamko la haki za binadamu. Pili, kila itikadi katika dini inatafsriwa kuwa potofu na itikadi nyingine zinazotofautiana kiitikadi. Tatu nitalieleza kwa mujibu wa mafundisho ya Bwana Yesu Kristo. Kabla sijaanza kufafanua hebu tuyasome maneno ya Yesu kwa mfano alioutoa:


“Akawatolea mfano mwingine, akisema, ufalme wa mbinguni umefanana na mtu aliyepanda mbegu njema katika konde lake; lakini watu walipolala akaja adui yake akapanda magugu katikati ya ngano, akaenda zake. Baadaye majani ya ngano yalipomea na kuzaa, yakaonekana na magugu. Watumwa wa mwenye nyumba wakaenda wakamwambia, Bwana, hukupanda mbegu njema katika konde lako? Limepata wapi basi magugu? Akawaambia adui ndiye aliyetenda hivi. Watumwa wakamwambia, basi wataka twende tuyakusanye? Akasema la; msije mkakusanya magugu na kuzing’oa ngano pamoja nayo. Viacheni vyote vikue hata wakati wa mavuno; na wakati wa mavuno nitawaambia wavunao, yakusanyeni kwanza magugu, myafunge matita matita mkayachome; bali ngano ikusanyeni ghalani mwangu.” (Math.13:24-30)



KANISA LACHOMWA MARA TATU MARA TATU LIKIKARABATIWA HUCHOMWA TENA WAHUSIKA WADAIWA NI WAUMINI WA DINI YA KIISLAMU




Wakati serikali ikijitahidi kukabiliana na vitendo vya uchomaji moto makanisa nchini vinavyofanywa na baadhi ya wanaharakati wa Kiislamu, imebainika kuwa Kanisa la Salvation Ministry for all Nations (SMAN) lililoko Mbezi Juu Jijini Dar es Salaam, limechomwa moto zaidi ya mara tatu.
Uongozi wa Kanisa hilo umelimbia Gazeti hili kuwa licha ya matukio hayo ya hujuma wanazofanyiwa na waumini wa Kiislamu kutoka katika msikiti wa Al Mubarak ulioko jirani na Kanisa hilo, usiku wa Jumapili iliyopita ya Desemba 2, 2012 , waumini hao walilibomoa Kanisa hilo na kufanya jaribio jingine tena la kulichoma moto.
Kwa mujibu wa Mchungaji kiongozi wa Kanisa hilo la SMAN Freddy Mwamtembe na Msaidizi wake Mch. Eliya Sudi, matukio matano ya hujuma mbaya dhidi yao yameripotiwa katika vituo vya polisi Mbezi Juu na Kawe na kufunguliwa majalada   yanayoeleza jinsi hujuma hizo zilivyofanyika kwa muda na nyakati tofauti.
Hujuma ya kwanza ya uharibifu mali na uchomaji moto wa Kanisa hilo iliripotiwa katika akituo cha polisi Kawe Februari 25, 2012  na kufunguliwa jalada nambari KW/RB/1743/2012 la kuchoma moto  choo cha kanisa hilo, ambapo jalada la pili la siku hiyo hiyo lilifunguliwa katika kituo cha Polisi Mbezi Juu likiwa na nambari MBJ/RB/586/2012 likitaarifu juu ya tukio la kuchomwa moto Kanisa hilo na kuharibu mali majira ya saa saba usiku.
Jalada jingine lilifunguliwa Machi 10, 2012 katika kituo cha Polisi  Mbezi juu na kupewa nambari MBJ/RB/714/2012, likitoa taarifa juu ya hujuma ya kuchomwa moto kwa Kanisa hilo la SMAN.
Hujuma nyingine lililofanyiwa kanisa hilo imo katika jalada la kituo cha Polisi Kawe lenye nambari KW/RB/7974/2012 kama taarifa ya  tukio lililofanywa Agosti 12, 2012 na waumini 28  wa msikiti wa Al Mubarak kwa kuvamia ibada, kujeruhi waumini na kuharibu mali za Kanisa hilo, ambapo Mchungaji Msaidizi Eliya Sudi alijeruhiwa akiwa madhabahuni.
Aidha uongozi wa Kanisa hilo ulilikabidha gazeti hili waraka unaoelezea jinsi waumini wa msikiti huo wanavyoshirikiana na mama mmoja kulifanyia fujo kwa kufukia msingi wa jengo lake na kisha mama huyo kuchimba msingi na kuanza ujenzi wa nyuma yake katika kiwanja cha Kanisa hilo.
Uongozi huo wa Kanisa la SMAN  ulisema ulilifikisha suala hilo katika ofisi ya Serikali ya Mtaa wa  Ndumbwi kupitia mjumbe wa nyumba kumi shina namba 40  Mbezi Juu Bwana Bonifasi Matiku  kwa ajili ya utatuzi, lakini hawakupatiwa msaada wowote, hadi ikabidi wamwandike barua Afisa Mtendaji wa kata ya Mbezi Juu, kumtaarifu juu ya kiwanja cha kanisa lao kuvamia na mama huyo ambaye kwa sasa jina lake limehifadhiwa.
Mjumbe huyo alidhibitisha juu ya kuwepo kwa hujuma dhidi ya Kanisa hilo na hatua alizochukua,ambapo liitaka serikali kutumia sheria ili kukabiliana nazo na kuzikomesha.
“Nakumbuka siku nilipofika  ofisini kwa Mtendaji wa Kata ya Mbezi Juu,  niliishia kutukanwa na wajumbe niliowakuta pale (majina tumeyahifadhi kwa sasa), wakinieleza mbele ya Mtendaji huyo kwamba ni lazima mama huyo  atajenga katika eneo la kiwanja chetu cha Kanisa. Nilimtahadharisha Mtendaji juu ya matusi niliyotukanwa lakini akanitaka niondoke akidai atashughulikia suala hilo. Mwandishi  hadi leo hakuna kilichofanyika”, alisema Mchungaji Mwamtembe.
Alisema tayari amelifikisha suala la  hujuma za Waislamu dhidi ya Kanisa lake katika ofisi za Kamanda wa Mkoa wa Kipolisi wa Kinondoni alikoahidiwa kushughulikiwa haraka kwa mujibu wa sheria.
“Kwa kweli sisi Wakristo ni wavumilivu sana kwa vile tunapenda amani na utakatifu. Tunaiomba sana serikali iwashughulike watu hawa wachache wasiopenda amani na wanaochochea vurugu za kidini. Ugomvi wa kidini ni mbaya sana. Tunaomba serikali iwe makini katika hili”, alisema Mch. Mwamtembe.
Alisema waumini hao korofi wa Kiislamu wanaolihujumu Kanisa lake kwa kulichoma moto, kuharibu mali na kujeruhi  washirika ni watu wanaofahamika wazi na hufanya hujuma hizo wazi wazi, wakitamka wazi  kuwa hawataki Kanisa katika maeneo yao; jambo ambalo ni kinyume kabisa na Katiba ya nchi  inayoruhusu uhuru wa kuabudu kwa kila mtu
Mmoja wa Mashehe wa Msikiti  wa Al Mubarak Mbezi Juu aliyetajwa kuwa mstari wa mbele kuhamasisha waumini wake kulihujumu kanisa  la SMAN, hakuweza kupatikana kutokana na kutofika msikitini hapo kwa uwazi, akiogopa kukamatwa na Polisi wanaomsaka.  
Aidha juhudi za kumpata mama aliyetajwa kushirikiana na waumini wa msikiti wa Al Mubarak kulihujumu kanisa hilo hazikuzaa matunda,  kutokana na makazi yake kutojulikana.