YESU NI JIBU

Jumapili, 20 Mei 2012

WAZIRI MKUU MSTAAFU MHE. EDWARD LOWASA ANATARAJIWA KUWA MGENI MAALUM TAMASHA LA WEZESHA UPENDO RADIO

 Waziri mkuu mstaafu mheshimiwa Edward Ngoyaine Lowasa anatarajiwa kuwa mgeni maalum katika tamasha la wezesha Upendo redio linalolenga kukusanya pesa za kitanzania zaidi ya milioni 220 kwa ajili ya ununuzi wa vifaa vya kuboreshea na kuongeza usikivu wa matangazo ya redio hiyo litakalofanyika Mei 27 mwaka huu katika ukumbi wa Diamond Jubilee jijini Dar es salaam.

Akizungumzia juu ya tamasha hilo msaidizi wa askofu wa dayosisi ya mashariki na Pwani (DMP) wa  kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) mchungaji George Fupe amesema kanisa hilo limemtumia mwaliko mheshimiwa Lowasa kuwa mgeni maalum katika tamasha hilo kwani yeye ni mmoja wa washarika wa kanisa hilo.

Aidha mchungaji Fupe alisema  tayari wameshawatumia baadhi ya mawaziri,wabunge,wafanyabiashara,watu mashuhuri na viongozi mbalimbali wa serikali pamoja na wakuu wa dini na madhehebu mbalimbali waweze kushiriki baraka hizo.
"Tunawakaribisha si kwa sababu wamekuwa na nyasfa kubwa serikalini bali tumeangalia unyenyekevu wao kwa Mungu na kwa jamii"alisema mchungaji Fupe.

Aliongeza kuwa kwa taratibu za KKKT askofu wa dayosisi hiyo na ambaye pia ni askofu mkuu wa kanisa hilo hapa nchini Dr Alex Malasusa ndiye atakuwa mgeni rasmi katika tamasha hilo.

Alisema kuwa licha ya upendo redio kumilikiwa na kanisa hilo na hata kurusha vipindi vya dini pia imekuwa ikitangaza vipindi vingi vya kijamii kama vile vya ujasiriamali,wanawake na matumaini, walemavu,vijana,watoto,wazee,upendo mseto na hali halisi ambavyo vimekuwa msaada kwa jamii.

Tamasha hilo la aina yake litapambwa na vikundi mbalimbali vya kwaya pamoja na waimbaji  binafsi wa ndani na nje ya nchi  kama vile Faraja Ntaboba kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) na Sara Kimani kutoka nchini Kenya.

Wengine ni Jackson bent kutoka jijini  Arusha,Jennifa Mgendi kutoka jijini Dar es salaam na kwaya mbalimbali za KKKT Dayosisi ya Mashariki na Pwani (DMP).

Upendo redio Fm inayosikika katika masafa ya FM 107.7 Mhz ilianzishwa mwaka 2004 ikiwa chini ya DMP na inasikika mikoa saba hapa nchini ambayo ni Dar es salaam,Pwani,Morogoro,Tanga,Zanzibar na baadhi ya sehemu za mkoa wa Kilimanjaro lengo lake ni kutaka isikie ndani na nje ya nje.

Ijumaa, 18 Mei 2012

WATANZANIA WATAKIWA KUTUBU DHAMBI NA KUACHA UOVU WAMGEUKIE MUNGU


Watanzania wametakiwa kuacha dhambi na kumgeukia Mungu kabla Mungu hajashusha ghadhabu kali katika taifa.

Kauli hiyo imetolewa na askofu wa kanisa la end time ministry askofu Frank Kilavatitu wakati akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es salaam ambapo amesema Mungu amemtumwa kuwaambai watanzania watubu dhambi na kuziacha zao.

Askofu Kilavatitu amesema kuwa katika maono yake Mungu amesema amechukizwa na uovu wa Tanzania ambao umekidhiri na watanzania wasipotubu ghadhabu itafuatia ambayo ni maji ya mvua yatakayosababisha maafa makubwa kwa muda wa siku saba.

Akifafanua juu ya dhambi na uovu ambao umekidhiri juu ya taifa la Tanzania ni baadhi ya viongozi wa dini kutoa kafara ya damu na wengine kujiunga na dini ambazo zinakwenda kinyume na maadili za MunguAkifafanua juu ya dhambi na

Hata hivyo ameongeza kuwa baada ya siku saba za toba wakikaidi atapiga taifa kwa maji kama ilivyotokea kwa siku za Nuhu na watu watdhani kuwa ni kiama kumbe ni fimbo ya Mungu kwa watanzania.

Alhamisi, 3 Mei 2012

MKESHA ULIOFANYIKA BCIC MBEZI BEACH WA KUWAOMBEA MAKUNDI MAKUU MATANO

 Askofu mkuu na mwangalizi wa WAPO MISSION INTERNATIONAL askofu Silverster Gamanywa akifundisha katika mkesha uliofanyika katika kanisa la BCIC Mbezi beach .
Katika mkesha huo askofu Gamanya aliwafanyia maombi na maombezi makundi makuu matano,ambapo makundi hayo ni
  1. kundi la watu waliompokea Yesu katika maisha yao.
  2. watu waliokuwa na matatizo mbalimbali ikiwepo magonjwa.
  3. kundi la wanandoa ili Mungu awasaidie katika ndoa zao.
  4. kundi la vijana wa kike ambao hawajaolewa wala hawana wachumba.
  5. kundi la mwisho la vijana wa kiume ambao hawajaoa wala hawana wachumba.
Hata hivyo kabla askofu hajawaombea makundi hayo aliweza kuwafundi neno la Mungu nakuwashauri  baada ya hapo ndipo anawafanyia maombi na maombezi.Aliongeza kusema kuwa ni vyema kukaa chini ya uongozi wa Mungu na kutafuta kuwa mtakatifu wakati wote maana Mungu ni mwaminifu hata kuacha bila kukubariki na kukutana na mahitaji yako.
Pia amewaonya wazazi kukaa na kuwalea watoto wao na vijana wao katika njia zinazompendeza Mungu.


Askofu anatoa maelekezo kabla ya kuanza kufanya maombi.



 Hawa ni baadhi ya watu waliofika kwenye mkesha na kuombewa sala ya toba na askofu Gamanywa.




Hawa ni wanandoa waliokuwa wakiombewa kwenye mkesha mafanikio katika ndoa zao

 Hawa ni baadhi ya wasichana waliofika kwenye mkesha wanafanyiwa maombezi na wanasikiliza kwa makini maelekezo kabla hawajaanza kuombewa.






  Hawa ni waimbaji wa DGC wakitoa huduma ya uimbaji katika mkesha katika kanisa la BCIC Mbezi beach.


 Askofu Gamanywa akiwaongoza wachungaji wa BCIC katika kuombea salada iliyotolewa kanisani hapo wakati wa mkesha





Hivi ndivyo waumini walivyokuwa wakionekana wakimsikiliza kwa makini askofu Gamanya ambaye hayupo pichani wakati akifundisha neno la Mungu.






Waumini wakimwabudu Mungu katika mkesha.




 Waimbaji wa BCIC Mbezi beach wakiimba katika mkesha


Hivi ndivyo madhabahu ya BCIC inavyoonekana.







Jumatano, 2 Mei 2012

Chanzo cha nguvu ya Mungu na uwepo wa Roho mtakatifu ndani ya kanisa ni pale tu kanisa ulimwengu walipojitoa katika kushirikiana na taifa la Israeli.

Kauli hiyo imetolewa na Askofu mkuu wa huduma ya maombi na ushauri wa kibiblia (BCIC) na pia ni msimamisi mkuu wa WAPO MISSION INTERNATIONAl Askofu Silverster Gamanywa katika mkesha uliofanyika katika kanisa hilo siku ya ijumaa ya tarehe 27 april.

Amesema hayo wakati akielezea lengo la ziara ya kuwaongoza waumini mbalimbali katika safari ya kutembelea taifa la Israel ambapo ziara hiyo itakuwa mwezi wa saba mwaka huu.

Baraka za Mungu zimetoweka katika mataifa mengi kutokana na waumini kutoshirikiana na taifa la Israeli  kusema kuwa kuna baraka za Mungu ambazo bado zinaandamana na wana wa Israeli likiwepo baraka ya kubariki taifa hilo nawe utabarikiwa na ukilaani taifa hilo utalaaniwa.

Kwa mkiristo halisi lazima aunganishwe na baraka za taifa hilo maana ni makosa kutengana na taifa hilo maana ukienda kinyume nawe wewe ni adui wa taifa hilo

Aidha Askofu Gamanywa amesema kuwa umaskini wa taifa la Tanzania limetokana na kutokuwepo kwa muunganiko na taifa hilo

Akielezea juu ya gharama za kuchangia ni dola za kimarekani elfu mbinu na mia tisa ambayo ni gharama ya tiketi ya ndege,hoteli ,chakula pamoja na nauli za usafiri za ndani wakati wote wa ziara.

Hata hivyo ameongeza kuwa ataongoza maombi na maombezi katika taifa hilo na kuahidi kuwa endapo watu watakubali kutembelea taifa la Israeli watakuwa wameungana na baraka za baba wa imani Ibrahimu.

Njia ya kuweza kufanya ni kurejesha uhusiano na taifa  hilo pili utainuka kiuchumi maana hoteli utakazolala ni za taifa hilo na vyakula na usafiri utakaotumika ni ya waisraeli hivyo utakuwa umechangia katika pato la taifa hilo na kuunganishwa na baraka za taifa.