Askofu
wa Kanisa la Ufufuo na uzima ,Josephat Gwajima akihudumiwa na muuguzi
wa hospitali ya TMJ, Dar es Salaam baada ya kulazwa katika chumba cha wagonjwa wenye uangalizi maalum.
Picha na
Salim Shao,
Mtumishi wa Mungu na pia ni askofu wa huduma la Ufufuo na Uzima Josephat Gwajima amelazwa mara baada ya kuzimia wakati akihojiwa kwenye kituo kikuu cha kati kanda maalum jijini Dar es salaam inaendelea vizuri.
Akizungumza na waandishi wa habari daktari Fortunatus Mazingo wa hospitali ya TMJ amesema kuwa hali ya mgonjwa inaendelea vizuri kwa sasa pamoja na kuwa amelazwa kwenye chumba cha wagonjwa wenye uangalizi maalum. Aidhaa Dr Mazingo amesema kuwa hali ya mgonjwa inaendelea vizuri ila vipimo vyote bado havijakamilika ila anaendelea vizuri.
Askofu Gwajima akiwaelekea kituo cha polisi akiwa na watumishi wenzake.
wewe unamaoni gani juu ya tatizo hilo la ghafla kwa askofu Gamanywa,
YESU NI JIBU
Jumamosi, 28 Machi 2015
LEO NI SIKU NYINGINE AMBAYO TUNAKUTANA KWENYE ENEO LA IFAHAMU BIBLIA YAKO.
1.Ni mtu yupi ambaye Bwana Mungu alitaka
kumtumia katika nchi ya Benjamini kuwaonya watu makosa yao na hakuwa tayari
kutokana na umri wake na katika biblia inapatikana katika kitabu gani?
Jibu:Ni
Yeremia,
Kitabu
cha Yeremia 1:1-7
2.Mshauri wa ajabu,Mungu mwenye nguvu,Baba
wa milele,mfalme wa Amani;hayo yote ni majina ya nani na kwa ufafanuzi tunapate
wapi?
JIBU
ni Bwana YESU
Isaya
9:6
3.Katika wanafunzi wa Bwana Yesu
(Tenashara) ni yupi ambaye ameamua kumkana kwa sababu ya fedha bwana Yesu.
JIBU;Yuda
ambaye pia aliitwa Iskariote
luka
22:3-6,yohana13:2,27,Marko 14:10-11.
4.Ni mfalme yupi ambaye amemwomba Mungu juu
ya hekanu kwa kusema ikiwa mbingu zimefungwa hata hakuna mvua ,kwa sababu
wanadamu wamekukosea wewe Mungu ,wakiomba kwa kukabili hekaluni Mungu asikie
dua zao na na kuwa samehe dhambi yao.
JIBU:mfalme
Suleimani
1wafalme
8:35-40;
2
wafalme 7:12-15
5.Kwanini malkia Esta aliwaamuru wayahudi
waliokuwepo Shushani kufunga na kuomba kwa siku tatu bila kula mchana na usiku.
JIBU:Kwa
lengo la kuingia kwa mfalme kinyume cha sheria maana hamani bin hamedatha alipanga kuwaangamiza wayahudi wote.
esta
4:15-17,
6.Ni Sababu gani kuu ya wayahudi kuuuwawa
na hamadi nani alisababisha kutokea kwa kosa hilo la wayahudi kuuwawa.
JIBU:ni
kwa sababau mara baada ya kupandishwa cheo kuwa mkuu wa maakida wote alitaka
kuinamiwa na kusujudiwe na kila mtu,alipoona Mordekai hamsujudii aligadhibika
sana,
Esta
3:5(-10).
Ijumaa, 27 Machi 2015
MAENDELEO YA TEKNOLOGIA IMEONGEZEKA SANA DUNIANI MTU AWEKEWA MOYO WA MTU MWINGINE NA KUENDELEA KUISHI:
Madaktari wa upasuaji huko
Cambridgeshire wamefanya upandikizaji wa kwanza wa moyo barani Ulaya kwa
kutumia moyo mwengine uliosimama kufanya kazi.
Myoyo hiyo hupatikana kutoka kwa
watu waliokufa lakini ambao myoyo yao bado inafanya kazi.
Katika upasuaji huo,moyo huo ulitoka
kwa mtu ambaye mapafu yake na moyo wake ulikuwa haufanyi kazi.
Hospitali ya Papworth inasema kuwa
mbinu hiyo huenda ikaongeza idadi ya myoyo inayopatikana kwa asilimia 25.
Mgonjwa aliyewekwa moyo mpya kwa
jina Huseyin Ulucan, mwenye umri wa miaka 60, kutoka London,alikabiliwa na
shinikizo la moyo mwaka 2008.
Alisema:kabla ya upasuaji,sikuweza
kutembea na nilichoka sana,kwa hakika siku na maisha mazuri.
Lakini anasema kuwa amefurahishwa na
kuimarika kwa afya yake tangu upandikizaji huo.
Kwa sasa najisikia mwenye nguvu kila
siku,na nimetembea hadi haospitalini asubuhi hii bila tatizo.
Kumekuwa na visa 171 vya
upandikizaji wa myoyo katika kipindi cha miaka 12 iliopita nchini Uingereza.
Lakini mahitaji yanashinda myoyo
iliopo ,hivyobasi wagonjwa wengine hungoja kwa miaka mitatu kupata kiungo
kinachowafaa.
Wengi ya wagonjwa hao hufariki kabla
ya kiungo kupatikana.
Wewe unamaoni gani?kuhusu hili,
chanzo BBC,
Imechapishwa na
Amaninafuraha
kwa
15:04
Hakuna maoni
:
Tuma Hii kwa Barua pepe
Blogu Hii!
Shiriki kwenye Twitter
Shiriki kwenye Facebook
Shiriki kwenye Pinterest
Lebo:
Afya
,
Imani
,
Teknologia
Jumatano, 25 Machi 2015
WAIMBAJI WA INJILI MNAENDA MBINGU YA NANI SEHEMU YA PILI
NA MCHUNGAJI MWANGOMOLA,
Kijana mmoja alipotaka kuoa akaniambia “nataka kuoa
mwimbaji wa Nyimbo za Injili na huyo mwimbaji ni maarufu” nikwamuuliza swali
“unaoa umaarufu au unaoa mke”, akaniambia “vyote viwili yaani umaarufu na mke”.
Wapo rafiki zangu wengine wengi walioniambia muonye kijana wako, nilipomwambia
juu ya tahadhali hiyo na kwamba sio mimi tu ninayejaribu kushauri bali pia hata
rafiki zangu wanaokufahamu na kumfahamu huyo mwimbaji. Alikataa katakata
akisema hayo ni maneno ya mtu aliyekosa na mwenye wivu juu ya watu wanaopata
vitu vizuri kama yeye alivyompata mwimbaji huyo wa nyimbo za Injili.
Ndugu msomaji wangu leo hii napoandika makala haya,
Ndoa haipo tena maana baada ya kuoana ilikuwa timbwili timbwili ndani ya nyumba
haikuwepo amani kabisa. Mke aliondoka atakavyo akiulizwa anasema “mimi
nimealikwa kwenda kuimba huniambii kitu, siwezi kuacha kumtumikia Mungu kwa
sheria zako”, manjonjo, sifa, umaarufu aliokuwa akiuona madhabahuni vyote
vilipotea kabisa maana mke sio sifa za uimbaji mke ni utii alionao kwa mumuwe
hata angekuwa maarufu kiasi gani, hata angekuwa Raisi wa Nchi bado akiolewa
anakuwa mke wa mtu, Uraisi unabaki Ikulu, nyumbani ni mke wa mtu, mama wa
nyumbani. Basi sasa hayo waimbaji wa nyimbo za Injili kwao hayako wakiolewa
hawataki kutii na wanaona wewe umeoa umaarufu na uimbaji wake, utamweleza nini
yeye nafahamika kuliko wewe na ndio maana hata wakiolewa hawatumii majina ya
waume zao, wanatumika ya kwao maana ndio wayayojulikana, labda awe aliolewa
kabla hajawa maarufu hapo atatumia jina la mumewe maana umaarufu umemkuta na
jina hilo, vinginevyo kila mtu ataitwa kivyake.
Katika dunia hii tuliyonayo hakuna watu wagumu kuwachunga
kama waimbaji wa nyimbo za Injili, hawashiriki Ibada wao ni mialiko tu. Januari
mpaka Desemba hawasikilizi Neno la Mungu hawana muda huo, ni kuimba tu.
Mwimbaji wa nyimbo za Injili anaweza akakaa mwaka mzima hajashiriki Ibada kwa
ukamilifu zaidi ya kuimba kwenye mialiko na kuondoka, yaani akimaliza tu kuimba
anaishia anaenda kuimba Kanisa lingine, nalo akimaliza anasepa kwenda Kanisa
lingine, yaani wako kawa njiwa anayerukia mti huu kisha mwingine, jamani
waimbaji mnaboa sana. Na Mitume wanawapa vichwa sana wakiwemo na baadhi ya
wachungaji wanaowaalika kila mara mwende mkaimbe kwenye makanisa yao na
mikutano yao, huku wakiwapa Utukufu uliopitiliza kwamba mwimbaji fulani
atakuwepo usikose, wanainuliwa kuliko Bwana Yesu, matangazo yanatangazwa kwamba
mwimbaji fulani atakuwepo na sio Bwana Yesu tena, hivyo mmewaongezea kifo.
Hawana Neno la Mungu ndani yao maana hawasomi Biblia hawana muda wa kukaa
kwenye viti wahubiriwe, wao ni kuimba tu wakimaliza hao huwaoni tena. Ndio maana
nyimbo zao hazina Upako tena zaidi ya kelele na hazina ujumbe maana ujumbe unapatikana kwenye Neno la Mungu
sasa wao hawana Neno, watapata wapi ujumbe.
Utanimbia mbona nyimbo zao zinapendwa na watu, waangalie
hao watu wanaozipenda hizo nyimbo zao uone ni watu wa namna gani, nyimbo zao
siku hizi zinapigwa mpaka bar, nyimbo za zamani thubutu! Huwezi kupiga kwenye
bar kwa sababu nyimbo zile zilikuwa na maonyo na ujumbe ambao umebeba Injili ya
kweli na toba, wimbo unamwonya mlevi kwamba asipotubu anaenda jehanamu au ulevi
ni dhambi nani atakayepiga kwenye bar wimbo huo.
Lakini ukiimbwa nibebe, kila mtu mvivu anataka
kubebwa au ukiimba mizaha (comedy) kila mtu atataka apige wimbo huo. Kwa sababu
watu wengi sana siku hizi wanapenda mizaha, ndio maana siku hizi watu wanaingia
na simu kanisani na huku wakila chingamu na mchungaji nae ana maji ya kunywa
madhabahuni, mizaha mitupu, hao lazima watapenda nyimbo kama hizo, zinazokutajia
Baraka kila siku.
Lakini kwa watu wa Rohoni nyimbo hizo haziwasaidii
lolote zaidi ya kuwa makelele masikioni mwao. Tunataka nyimbo zenye ujumbe,
zenye kumfanya mtu atubu, zenye Upako si vinginevyo. Zamani wimbo ukipigwa
machozi yatakutoka utafarijiwa, utakuletwa kwenye kumtafakari Mungu. Kama
umeokoka na kama bado unaokoka, watu wengi waliookoka kupitia nyimbo zile za
zamani, watu hao wapo na wanandelea na wengine wamemaliza mwendo (wamelala)
nawafahamu.
Waimbaji wa siku zile walikuwa watu wa rohoni
walituliwa miguuni pa wachungaji wao pamoja na kuwa na adabu nzuri na
kusikiliza maonyo za si kusikiliza tu maonya bali kuyashika (kuyatendea kazi).
Ndio maana walidumu na nyimbo zao zina upako mpaka leo, japo nyombo vya habari
hawazipigi mara kwa mara nyimbo hizo. Mambo yalianza kuharibika baada ya kuanza
kuimba kila mtu kivyake kwa lengo la kupata pesa na sio kumtumikia Mungu, hapo
mambo yakawa mabaya sana, hata maadili yanapotea, waimbaji wa nyimbo za Injli
hawana maadili (Ethics) ndio maana hata nyumba (Ndoa) zenu zinashida tupu kila
mtu anajuta, hakuna Amani katika ndoa zenu, ndio maana mnaamua kwenda huko
kwenye vyombo vya habari kufichua mkidhani huko mtapata majibu, majibu yako kwa
Bwana Yesu aliyewapa vipawa hivyo, waimbaji mmemwaibisha Kristo kiasi cha
kutosha sasa rudini kundini mkamtumikie Mungu kwa Moyo na Utakatifu ambao
hapana mtu atayemwona asipokuwa nao EB. 12:14 si vinginevyo ili pia mpate amani
katika ndoa zenu zinazowaka moto. Kila mtu akiomba kimoyo moyo mwenzi wake afe
ili awe huru. Na hakuna anayekufa wote mko hai muonje joto la jiwe maana
hamsikii maonyo kama yule kijana wangu ambaye aliniambia anataka kuoa umaarufu
wa mkewe, alinilalamikia juu ya ndoa yake sijibu neno namtizama tu. Biblia
inasema Mithali 29:1 “Aonywaye mara nyingi akishupaza shingo, atavunjika
ghafula wala hapati dawa”.
Kwa hiyo mnapoonywa mara nyingi jaribuni kusikia na
kuacha yale mabaya ambayo kwayo mnaonywa, Biblia inaonya juu ya kushupaza
shingo (kutosikiliza maonyo) kuwa mtu wa namna hiyo atavunjika ghafula na wala
hapana dawa. Sasa wewe mwimbaji wa nyimbo za Injili kwa nini uvunjike shingo
wakati dawa ipo. Kazi yako ni kusikia na kujirekebisha na kuacha kabisa.
Mimi hapa ni mwonyaji wala msinichukie mna hiari, kama
nilivyokwisha tangulia kusema kwenye makala ya mwanzo kabisa, kwamba unaweza
kuyachukua maonyo haya au ukayaacha lakini katika umilele mtakuja kukumbuka
siku moja kwamba tulionywa katika njia zetu hatukusikia, mimi leo nawaonya waimbaji wote, wote kila anayejiona ni
mwimbaji apokee ujumbe huu uwe maarufu au unayeanza kuimba maana na wewe
unaelekea huko, pata dawa mapema ili usije ukavunjika shingo.
ITAENDELEA WIKI IJAYO!!!!!!!!
JIFUNZE BIBLIA YAKO KILA ITWAPO LEO.
1.Ni watoto wangapi wa mfalme Sauli
waliuwawa na wafilisti katika mlima Gilboa
Jibu;Ni
Yonathani,Abinadabu na Malkishua
1Nyakati
10:1-2
2.mfalme Sauli aliuwawa na nani?
Alijiua
mwenyewe
1Nyakati
10:4-6
3.Ni mtu yupi alikuwa anatumia uchawi na
watu wengi walimogopa sana na yeye kusema kuwa ni mtu mkubwa?
Simoni
matendo
8:9-13
4.Roho mtakatifu anatusaidia katika sehemu
mbalimbali ama nyingi ila katika suala la maombi hutusaidia kufanya nini na
katika biblia ibapatikana wapi?
Hutusaidia
katika udhaifu wetu
Warumi
8:26-27
5. Ni nani alifundisha neno la Mungu kwa
nguvu sana na kuwaonya watu kutenda mabaya wapinge Roho Mtakatifu badala yake
walimpiga kwa mawe hadi kufa.
Stefano
matendo
7:51-60