YESU NI JIBU

Jumatano, 29 Julai 2015

"NI SAA YA USHINDI NA KUFUNGULIWA UNGANA NA MCHUNGAJI KATUNZI KATIKA KUENEZA INJILI KWA SADAKA YA INJILI”

·      Kanuni ya Mungu ni kupanda na kuvuna
            (Isaya 6:8)
 Katika mfululizo wa makala haya, tumekuwa tukijifunza umuhimu wa kujitolea muda wetu, mali zetu na akili zetu kumtumikia Mungu kama alivyotuagiza katika Neno lake. Leo Mtumishi wa Mungu, Mchungaji Florian Josephat Katunzi, anaeleza  kwa kina umuhimu wa kila aliyeokolewa kuamka na kwenda kumuokoa mwingine anayeangamia dhambini, kuzimu ikipanua mdomo kumdaka. Tafadhali ungana na Yonathan Landa katika makala haya...
Jukwaa ambalo mtumishi wa Mungu mch.Florian Josephat Katunzi analihitaji kwa ajili ya kazi ya MUNGU ya kueneza injili kwa watu wote.
Yapo maswali makuu anayouliza Bwana kwetu sisi tunaolicha jina lake. Maswali yenyewe ni haya; 1. Nimtume nani? Hapa Muumba wetu, akiisha kutuokoa kwa damu yake ya thamani atutaka tusikae chini na kufikiri tumefika. Laa anataka mtu wa kumtuma kuwaendea wale wengine ambvao bado wanamtumikia shetani.
Ni hapa swali libngine linapokuja kwetu, Je ni nani atakayekwenda kwa ajili yetu. Bwana anamtafuata mtu atakayemtuma kumletea wanakondoo wengine waliopotea. Anawahitaji zizini mwake.
Inatupasa hapa kukumbuka kuwa mtu huyu hatakwenda kwa niaba yuetu tu, bali atakwenda kwa ajili yetu. Mpango  wa injili wa miaka 20 unahitaji Mtu atakayekwenda  kuhubiri habari njema za ufalme wa Mungu, mtu huyu lazima aenda kwa niaba yetu. Hivyo basi, unaposhiriki kwa sadaka yako maana yake ni kuwa umemtuma mhubiri aende shambani mwa bwana kwa niaba yako na watoto wako.

Mimi nilipoupokea mpango huu nilikubalia kwenda kwa ajili yanu  kuhubiri pamoja nanyi katika mpango huu  wa miaka 20 ya safari ndefu za kuwakoa wale ambao bado hawajaokolewa ndabni na nje ya nchi yetu.

Mtumishi wa Mungu , Musaa alipokuwa kwenye misheni ya kuiokoa wana wa Israeli kutoka utumwani Misiri aliulizwa na Farao (mtawala wa Misri) “Utaenda na akina nani huko Jangwani kumtumikia huyo Mungu wako?”

Majibu ya maswali haya yanapatikana katika Biblia kitabu cha Kutoka 10:9, jibu lenyewe ni hili:
“Musa akamjibu; tutakwenda na vijana wetu na wazee wetu, na wana wetu, na binti zetu, tutakwenda nma kondoo zetu na ng’ombe zetu; kwa kuwa inatupasa kumfanyia Bwana siku kuu.”
Katika mpango huu wa wokovu inatupasa kumtumikia Mungu sisi na watoto wetu, tutakwenda na mali zetu (sadaka zetu). Malizetu lazima zitumike katika kazi ya Injili, tupate vyombo, gari na Jenereta. 
Ni muhimu sana watoto wetu wawe sehemu ya huduma, vijana wako wawe sehemu ya huduma ili kwa sadaka zako tuwe alama ya ukumbusho katika Ufalme wa Bwana wetu Yesu Kristo.
Leteni sadaka hizi, imje mbele zake katika utukufu  ili sifa zimuendee yeye, kama maandiko matakatifu katika zaburi  yasemavyo: “Mpeni Bwana utukufu wa jina lake, leteni sadaka mkazingie nyua zake.”
(Zaburi 96:8)
Sdaka yako ni kiunganishi na Mungu aliye hai kwa kuwa kupitia utoaji Yeye huuona unyofu wako kwake. Neno la Mungu linasema: “Ndipo ghala zako zitakapojazwa kwa wingi, na mashinikizo yako yatafurika divai mpya.” (Mithali 3:10). Sadaka yako ya Injili itakuondolea msiba  usiwe katika nyumba yako na raha siku ya mapito yako uwe na kitu cha kumkumbusha Mungu aliye hai jkama alivyofanya  Ezekia.
“Siku hizo Ezekia aliugua, akawa katika hatari ya kufa, na Isaya mwana wa aAmuzi, akaenda kwa Mfalme, akamwambia, Bwana asema hivi, tengeneza mambo ya nymba yako; maana utakufa, wala hutapona . basi Ezekia akajigeuiza akaelekeza uso wake ukutani akaomba Bwana, akasema, eeBwana, kumbuka haya, nakusihi, kwamba nimekwenda mbele zako katika kweli na kwa moyo mkamilifu, na kutenda yaliyomema machiini kwako. Ezekia akalia san asana. Ikawa neno la Bwana likamjia Isaya, kusema, enenda ukamwambie Ezekia, Bwana , Myungu wa daudi, baba yako, asema hivi, mimi nimeyasikia maombi yako, nimeyaona machozi yako; tazama nitaziongeza siku zako, kiasi cha miaka 15.” (Isaya 38:16).
Nakaribisha marafiki wa Injili tushirikiane ili kutimiza mpango huu ambao si wa kidhehebu wala haufungwi na kundi lolote; tunaalika watu 200 watakaojitoa kwa sadaka ya shilingi 1,000,000, kwa ajili ya maandalizi haya ya ununuzi wa vifaa vya Injili, watu 200 watakaojidhabihu kwa sadaka ya shilingi 500,000. Lakini pia tunawaalika wengine kuungana nasi kwa njia ya utoaji wa sadaka zao ili kukamilisha mpango huu mkubwa unaolenga kufika kila kijiji cha Tanzania kukabiliana na giza hili la kiroho.

Aina ya magari ambayo ndiyo yanahitajikwa kwa ajili ya kueneza injili kwa kusafirishia vyombo na jukwaa.
Mimi pamoja na wewe uliyepokea neema hii ya Injili hatuwezi kutulia wakati shetani akihubiri hadharani na kuchukua watoto wetu kila dakika wakijiunga na ibada za kishetani kwa tamaa ya kupata utajiri wa haraka haraka.
Nawaomba wana-injili watuunge mkono katika mpango huu mkubwa na maono haya, yenye lengo la kuwafikia wenzetu kokote waliko, ili tuweze kununua vyombo hivyo, jukwaa na gari kwa ajili ya safari za injili nchi nzima.
Unaweza kushirikiana nasi katika mpango huu wa ki-Mungu kwa kuchangia kupitia akaunti zetu zifuatazo:
Jina la Akaunti: Florian Josephat Katunzi
Benki: CRDB no. 01j1028426200
M-Pesa - 0754367826
Tigo Pesa: 0718-267171
Airtel money: 0784-367826
UKITAKA KUWASILIANA NASI WANABLOG HII WHATSAPP NI 0752834514.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni