YESU NI JIBU

Jumatano, 9 Machi 2022

RAIS SAMIA AKUTANA NA KUFANYA MAZUNGUMZA NA MKURUGENZI WA UN WOMEN DK.MAXIME HOUINATO IKULU TUNGUU ZANZIBAR

    

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Mkurugenzi wa UN Women Ukanda wa Afrika Mashariki na Kusini Dkt. Maxime Houinato alipofika Ikulu Tunguu Zanzibar

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa katika picha ya pamoja na Mkurugenzi wa UN Women Ukanda wa Afrika Mashariki na Kusini Dkt. Maxime Houinato na Ujumbe wake mara baada ya kumalizika mazungumzo yao Ikulu Tunguu Zanzibar

 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Mke wa aliyekuwa Rais wa Kwanza wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Mama Fatma Karume alipomtembelea kumjulia hali nyumbani kwake Bumbwini Mkoa wa Kaskazini Unguja 

 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi CCM Zanzibar Dkt. Abdallah Sadala Mabodi na Familia yake, alipomtembelea nyumbani kwake Chukwani Mkoa wa Mjini Magharibi  Unguja leo tarehe 09 Machi, 2022 kwa ajili ya kumfariji kutokana na kupotelewa na Mtoto wake  kwenye ajali ya Ndege.

 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Naibu Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi CCM Zanzibar Dkt. Abdallah Sadala Mabodi na Familia yake, alipomtembelea nyumbani kwake Chukwani Mkoa wa Mjini Magharibi  Unguja leo tarehe 09 Machi, 2022 kwa ajili ya kumfariji kutokana na kupotelewa na Mtoto wake  kwenye ajali ya Ndege.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na Familia ya Waziri wa Afya wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Mhe. Ahmed Nassor Mazrui alipowatembelea nyumbani kwao Mbweni Mkoa wa Mjini Magharibi  Unguja leo tarehe 09 Machi, 2022 kwa ajili ya kuwafariji kutokana na kupotelewa na Mtoto wao  kwenye ajali ya Ndege.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Familia ya Waziri wa Afya wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Mhe. Ahmed Nassor Mazrui alipowatembelea nyumbani kwao Mbweni Mkoa wa Mjini Magharibi  Unguja leo tarehe 09 Machi, 2022 kwa ajili ya kuwafariji kutokana na kupotelewa na Mtoto wao  kwenye ajali ya Ndege.

Jumanne, 8 Machi 2022

MKEMIA MKUU AHIMIZA MATUMIZI SALAMA YA KEMIKALI.

 


Mkemia Mkuu wa Serikali Dkt. Fidelice Mafumiko amewahimiza wajasiriamali kuzingatia matumizi salama ya kemikali wanazotumia katika uzalishaji wa bidhaa zao ili kulinda afya za binadamu na mazingira.

Dkt. Mafumiko ameyasema hayo jana jijini Dar es Salaam alipotembelea maonesho ya wanawake wajasiriamali yaliyoandaliwa na Chama cha Wanawake Wafanyabiashara Tanzania (TWCC) ambayo yanafanyika kwenye viwanja vya Mnazi Mmoja.

Aliwaeleza wajasiriamali hao kuwa Mamlaka ya Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali (GCLA) katika utekelezaji wa majukumu yake imekuwa ikitoa mafunzo kuhusu matumizi salama ya kemikali kwa wadau wake mbalimbali wanaotumia kemikali wakiwemo wajasiriamali ili kuwapa elimu ya matumizi salama ya kemikali pamoja na namna bora ya kuhifadhi bidhaa zao.

“Kwa nafasi yetu kama wasimamizi wa sheria ya kemikali tuna jukumu la kuhakikisha watumiaji wa kemikali kama vile watengeneza batiki na wanaosindika bidhaa za vyakula pamoja na dawa asili wanazingatia taratibu za kiusalama, hivyo tunawaahidi kuendelea kutoa elimu zaidi kwa wadau hao,” alisisitiza Dkt. Mafumiko.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa TWCC, Mercy Sila alisema kuwa katika zoezi la kuwafikia wajasiriamali, taasisi yake inapata ushirikiano mzuri kutoka GCLA kwenye kuwaelimisha wajasiriamali hao namna bora na salama ya kutumia kemikali katika uzalishaji wa bidhaa.

Aidha, baadhi ya wajasiriamali waliowahi kupata mafunzo ya matumizi salama ya kemikali kutoka GCLA walieleza kuwa elimu waliyoipata imewasaidia kuboresha bidhaa zao na kulinda afya zao bila kuchafua mazingira.

Naye mjasiriamali kutoka Zanzibar, Salma Othman ameiomba GCLA iendelee kutoa elimu kwa wadau wengi zaidi kupitia njia mbalimbali ili kuhakikisha jamii ya Watanzania inazingatia usalama wa afya za watu na mazingira.

Maonesho hayo ya pili ya wajasiriamali wanawake yaliyoandaliwa na TWCC yalianza Machi 3 mwaka huu na yanatarajiwa kukamilika Machi 8, 2022 ambayo ni Siku ya Wanawake Duniani.



MKAKATI WA MKOA WA DAR ES SALAAM NI KUONGEZA MAPATO BAJETI 2022/23

 


Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe. Amos Makalla leo ameongoza kikao Cha Kamati ya ushauri ya Mkoa RCC kuhusu mapendekezo ya bajeti ya Mkoa huo kwa Mwaka wa fedha 2022-2023 ambapo Mkoa huo umeomba kupatiwa kiasi Cha Shilingi bilioni 650.97 kwaajili ya utekelezaji wa Shughuli mbalimbali ikiwa ni ongezeko la Shilingi Bilioni 88.7 kwa Mwaka 2021/2022.


Akizungumza wakati wa kikao hicho, RC Makalla amesema kiasi hicho kinajumuisha Mishaha Shilingi Bilioni 338.2, Miradi ya maendeleo Shilingi Bilioni 77.7 na Matumizi mengine kiasi Cha Shilingi bilioni 10.8 ambapo upande wa makusanyo Mkoa umelenga kukusanya Shilingi Bilioni 224.

Aidha RC Makalla amesema miongoni mwa vipaombele vitakavyozingatiwa ni pamoja na kudumisha amani, ulinzi na usalama,  Ujenzi wa jengo la ofisi ya Mkuu wa Mkoa, kuboresha Elimu, Afya, Mazingira Bora ya Biashara, miradi ya kimkakati, ustawi wa jamii, kudhibiti na Kupunguza Majanga.

Ili kuhakikisha Serikali inaendelea kutoa huduma bora kwa wananchi, RC Makalla ametoa wito kwa Halmashauri kuhakikisha zinasimamia kikamilifu *makusanyo ya mapato na kubuni vyanzo vipya vya mapato.

Kikao hicho pia kwa kauli moja kimeazimia kumpongeza na kumshukuru Rais Samia Suluhu Hassan kwa utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo jijini humo pamoja na kutoa fedha kwa wakati jambo linalosababisha miradi kutekelezeka kwa wakati pasipo usumbufu wowote.