YESU NI JIBU

Alhamisi, 30 Mei 2013

WAZIRI MKUU MIZENGO PINDA ANATARAJIWA KUWA MGENI RASMI TAMASHA LA AMANI NA UPENDO JIJINI DSM


Waziri mkuu wa jamhuri ya muungano wa Tanzania Mh.Mizengo Pinda anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika tamasha la amani na upendo litakalofanyika jijini Dar es salaam, Agosti 28 mwaka huu.

Akizungumza na waandishi wa habri mwenyekiti wa kituo cha kulelea watoto yatima cha New Hope Family Bw. Omary Kombe amesema lengo la tamasha hilo ni kuenzi amani na upendo hapa nchini.

Aidha Bw. Kombe ameongeza kwamba kutokana nan chi nyingi za kiafrika kukumbwa na vita ya wenyewe kwa wenyewe wameamua kuratibu tamasha hilo kuihamasisha jamii ya watanzania kutunza amani na upendo sanjari na kuchangisha fedha kwa ajili ya kujengea kituo cha kulelea watoto yatima kiasi cha shilingi milioni 300.

Hata hivyo Bw.kombe amesema jamii inapaswa kuenzi amani hasa ngazi ya familia kwani kukosekana kwa amani katika ndoa ndio chanzo kikubwa cha kuongezeka watoto wa mitaani.
Amani inapotoweka kwenye familia hupelekea watoto na wazazi kuishi katika hali ngumu kiasi kwamba kila kukicha watoto wanaongezeka mitaani na wanaishi kwenye mazingira magumu.
Ni vema kuendelea kuenzi na kusimamia amani na upendo kwa juhudi zote ili kuweza kujenga taifa ambalo linaweza kustawi kiuchumi na kisiasa.  

  

REJOICE AND HOPE MINISTRIES RHM WATOA MATIBABU BURE JIJINI DAR ES SAALAM

Taasisi isiyo ya kiserikali inayoitwa,’Rejoice and Hope Ministries’, -RHM, yenye makao yake makuu nchini       Marekani, kwa kushirikiana na Madaktari nchini, watatoa matibabu ya bure  katika kituo cha Pentekostal Holy Mission maeneo ya Mbezi Jijini Dar es Salaam.
Mwasisi wa Taasisisi hiyo Dk.Rejoice Ndalima amesema kuwa, jopo la madaktari hao kutoka Marekani, watashirikiana na madaktari wa Tanzania na wauguzi kutoa  matibabu ya macho, uvimbe pamoja na magonjwa ya kawaida ambapo watapatiwa dawa bure baada ya kutibiwa.
Sanjari na matibabu hayo, RHM watatoa misaada kwa jamii kama vile wajane, yatima na watoto waishio katika mazingira magumu ambapo misaada hiyo itatolewa Jumamosi hii katika Kanisa la Pentekostal Holliness Ubungo Jijini Dar es Salaam.

Taasisi hiyo ya RHMI, hutoa misaada mara kwa mara kwa jamii ambapo mwaka jana walikuwa Mkoani Morogoro na walifanikiwa kuwahudumia bure wagonjwa mia tano.

VIJANA WATAKIWA KUJIKOMBOA KIUCHUMI KWA KUTUMIA FURSA ZIANAZOJITOKEZA

Wito umetolewa  kwa vijana nchini kutumia fursa  mbalimbali zinazojitokeza katika jamii ili kujikomboa  kiuchumi na kuliinua taifa  kwa ujumla.
Wito huo umetolewa na  Makamu wa Rais wa Vicoba Bibi  Scholastica  Kevela  alipokuwa akitoa msaada  kwa kikundi cha Jambo Africa Group kwa malengo  ya kuinua  Vijana Jijini Dar es Salaam.
Aidha Bibi Kevela  amesema  vijana ni  muhimu kupewa  kipaumbele  katika Nyanja  mbalimbali ili kumiliki uchumi na  kupunguza utegemezi katika jamii.

Naye Mwalimu wa Ujasiriamali wa Vicoba kitaifa, Bibi  Flora Masalu amesema kuwa, vijana wanapaswa kuachana na dhana ya kuajiriwa na kujiajiri kwa kufanya shughuli  za ujasiriamali.

MWANAFUNZI KIDATO CHA PILI KUJINYONGA

Mwanafunzi wa Shule ya Sekondari Keko Wilayani Temeke Jijini Dar es Salaam, Edson John mwenye umri wa miaka kumi na tatu aliyekuwa anasoma kidato cha pili, amekutwa amejinyonga kwa kutumia kamba ya katani aliyoitundika kwenye mti.
Kamanda wa Polisi mkoa wa kipolisi Mkoani Temeke, Engelbert Kiondo amedhibitisha kutokea kwa tukio hilo  maeneo ya makaburini Temeke na kijana huyo alikutwa na karatasi yenye ujumbe mfupi  kwamba ameamua kujinyonga kwa kusingiziwa maneno ya uongo.
Hata hivyo, Kamanda Kiondo  alieleza kuwa, sababu  za kujinyonga kwa kijana huyo bado hazijafahamika na mwili wake umehifadhiwa Hospitali ya Wilaya Temeke kwa uchunguzi zaidi.
Suala la watu kujinyonga katika jiji la Dar es saalam linaendelea kushika kasi kwani kila kukicha hutolewa taarifa za watu kujinga ama kujaribu kujiua hivyo ni nyema hatua na njia maususi zichukuliwe ili kudhibiti na kuondoa tatizo hilo.

Imeonekana kuwa shetani anasababisha watu kujiua kwa kusingizia vitu mbalimbali kama kuachwa na wapenzi wao wengine magonjwa,shida,kukataliwa jambo ambalo ukichunguza kwa undani sio la kweli ni hila za adui kuwaangamiza wanadamu bila kufikilia toba.

NGUVU ZA ROHO MTAKATIFU ZINAENDELEA KUONEKANA KATIKA MADHABAHU YA EAGT SINZA

Hakika moto wa Roho mtakatifu unaendelea kuwaka katika kanisa la EAGT Sinza kwa takribani wiki nzima ambapo mtumishi wa Mungu mchungaji Florian Katunzi ameendelea kufundisha kwa neno kufundisha neno la Mungu juu ya madhabahu.
Aidha Katunzi amewafanyia maombi na maombezi watu waliofika katika kongamano  hilo na watu wengi wamefunguliwa katika matatizo yao mbalimbali yanayowakabili katika maisha yao








Mchungaji wa kanisa la EAGT City Center kushoto mchungaji Florian Katunzi akisimama na mchungaji Emanuel mwasota katika madhabahu ya kanisa la EAGT Sinza.












 Baadhi ya viongozi wa WWI waimba wakiwa kwenye kongamano jimbo la Kinondoni












 Mwimbaji Christina Matai akiimba wimbo wake wa Raha jipe mwenyeweadiu zangu nimewasamehe bure












 Baadhi ya waimbaji wa kwaya ya Majestic singers wakiimba wimbo wao wa mifupa katika kanisa la Sinza




Mwimbaji wa nyimbo za injili Bitres Mwaipaja akiimba katika konga
mano la wana wake watumishi waenezao injili katika kanisa la EAGT Sinza

Jumanne, 28 Mei 2013

WIKI YA UAMSHO EAGT SINZA KWENYE KONGAMANO LA WWI JIMBO LA SINZA









Kiukweli neno la Mungu limeonekana kuleta mageuzi na mapinduzi makubwa katika ulimwengu wa roho kiasi kwamba watu wenye mataizo mbalimbali taabu shida sanjari na walioshuka kiimani wanainuliwa.

Hayo yamebainika baada ya mtumishi wa Mungu mwinjilisti ambaye pia ni mchungaji wa EAGT City Center mchungaji Florian Josephat Katunzi aliposimama na kuhubiri neno la Mungu katika kanisa la EAGT Sinza kwenye kongamano la Wanawake Waenezao injili jimbo la Kinondoni WWI ambapo alisema kuwa lazima kile ambacho adui amekiiba unaweza kurudishiwa maana lazima wenye magonjwa migogoro ya ndoa watafunguliwa.
Aidha mch.katunzi aliema kuwa ni lazima kufunguliwa katika jina la yesu haijalishi umekuwa katika matatizo mbalimbali hata kama umetumiwa majini mikosi wiki hii ni ya kufunguliwa .

Hata hivyo aliongeza kuwa kuokoka ni lazima na kuacha njia zako mbaya na kufunguliwa na kumfuata Hata hivyo aliongeza kuwa kuokoka ni lazima na kuacha njia zako mbaya na kufunguliwa na kumfuata Yesu.










Mchungaji Florian Katunzi akijiaandaa kusimama madhabahuni kwenye kongamano la WWI jimbo la Kinondoni












 Mkurugenzi wa WWI jimbo la kinondoni Sophymery Matingisa akiwa na mchungaji Katunzi














Mch.Katunzi akiwasha moto  katika kongamano la WWI




























Mchungaji Emanuel Mwasota akimsikiliza kwa makini mchungaji Katunzi akihubiri katika kanisa la EAGT Sinza














Wanawake wakishangilia katika kongamano la WWI wakati mchungaji Katunzi akihubiri












Wakinamama wakifuatilia kwa makini mafundisho ya neno la Mungu katika kongamano hilo

































 Wanawake wakimwabudu Mungu na kuomba katika kongamano hilo la WWI wakiongozwa na mchungaji Katunzi























Jumanne, 21 Mei 2013

UADUI MKUBWA WA UKRISTO SIO DINI NYINGINE ILA NI UKRISTO WA KIBAYOLOJIA



                             

Imeelezwa kuwa adui mkubwa wa ukristo si dini nyingine wala mamlaka za kisiasa, bali ni ukristo unaoenea kibaiolojia pasipokuwa na Roho Mtakatifu.

Hayo yameelezwa na Mwangalizi Mkuu wa Wapo Mission International, Askofu Sylivester Gamanywa wakati wa maadhimisho ya kilele cha  wiki kumi na saba za Ibada ya ujazo wa  Roho Mtakatifu iliyofanyika Jumapili iliyopita katika Ukumbi wa BCIC Mbezi Beach Jijini Dar es Salaam.

Aidha, Askofu Gamaywa amebainisha kuwa, ukristo usioambatana na Roho Mtakatifu ambaye ndiye anayefundisha, si ukristo halisi bali ni imani potofu na kwamba uzao wa kikristo hutokana na Mungu kinyume na uzao wa kibaiolojia.
Huku akishangiliwa na maelfu ya watu waliohudhuria maadhimisho hayo ambayo yameangukia Sikukuu ya Pentekoste, Askofu Gamanywa amesisitiza kwamba kama Mkristo hajaokoka, Mbinguni haingii kamwe hata kama amebatizwa.
Ameeleza kuwa, lengo la maombezi hayo ya ujazo wa Roho Mtakatifu, ni kumtambulisha Mungu katika utendaji wake wa nafsi tatu ambazo ni Baba, Mwana na Roho Mtakatifu na uzao wake wa kiroho.







Askofu Gamanywa akiwafundisha juu ya changamoto ama uadui wa dini ya kikristo






Askofu akiwaombea waumini ambao wamefika mbele ya madhabahu kwa le
ngo la kupata maombi na maombezi juu ya ujazo wa Roho Mtakatifu








Askofu akiwaongoza waumini  na kuongoza katika maombi  huku wakiinua mikono yao juu.


























Hapa maombi yamekolea uongozi wa Roho Mtakatifu ukichukua nafasi

























Mchungaji Amon Kilahiro anayepiga gitaa akiongoza
kikundi cha kusifu na kuabudu cha BCIC Mbezi beach katika ibada ya ujazo wa Roho mtakatifu.






Waimbaji wa kikundi cha kusifu na kuabudu cha BCIC wakibubujika katika ibada ya ujazo wa Roho mtakatifu.











muumini huyu akiomba kwa roho na kweli katika  ibada ya maombezi ya ujazo wa Roho mtakatifu







Waumini wakiomba ujazo wa Roho mtakatifu pamoja na kuombea mahitaji mengine mbalimbali katika ukumbi wa BCIC Mbezi beach.















































Hapa lazima kieleweke






































Jumatano, 15 Mei 2013



Hakika ni wiki kumi na tatu za urejesho ambayo ni maombi na maombezi na kila siku ya jumapili jioni kuanzia saa tisa mchna kutafanyika maombi kwa kila mmoja atakayewasili kaitka kanisa hilo.Na hayo yote yanafanyika katika chuo cha utalii na bandari Temeke Mwembe yanga,Je unateswa na dhambi,je unateswa na magonjwa,je umetupiwa mikosi,je unasumbuliwa na madeni,je ndoa yako imekuwa mwiba.
wahudumu wakiwaombea watu mbalimbali waliofika katika ukumbu wa utalii bandari kupata maombi na maombezi kutoka kwa mchungaji Florian J.Katunzi


















 hapa chini ni mwandishi wa habari wa gazeti la jibu la maisha gazzeti la kila wiki la kikristo akifanya mahojiano na baadhi ya watu waliofika kwenye ibada ya maombi na maombezi.