YESU NI JIBU

Ijumaa, 29 Julai 2016

WENGI WAFUNGULIWA NA KUWEKWA HURU WAKATI WA UBATIZO:

 Hirizi ambazo zilitapikwa na mmoja wa watu waiofika kanisani na kuanza kuombewa na mara baada ya kutapika alianza kufunguliwa.

JIMBO LA TEMEKE LIMEONYWA KUWA MAKINI NA MGOGORO UNAOENDELEA AMBAO TAYARI UPO UMEFIKISHWA MAHAKAMANI:

Mwenyekiti wa Bodi ya wadhamini wa kansia la EAGT, Mzee Henri Mfuko, ameonya kuwa kansia hilo linakabiliwa na hatari ya kugawanyika kufuatia mgogoro ulioibuka baina ya uongozi wa kanda na ule wa Jimbo la temeke ambao umesababisha kufunguliwa kwa kesi ya madai mahakamani na kusimamishwa kwa viongozi wa Jimbo. Huku ikielezwa kuwa kivuli cha Hayati Askofu Dk. Moses Kulola ndicho kinacholityesa kanisa hilo.
Aidha imeelezwa kuwa  Wothia alioandika kulola Kabla ya kufariki dunia unaompa Katunzi kijititi cha kuhubiri Injili, kukua kwa kasi kwa kansia la EAGT City Centre na mpango wa kujenga majengo ya kisasa ya Jimbo la Temeke viliibua upinzani mkubwa  uliopelekea kuvuliwa  madaraka  na kugawanywa kwa Jimbo bila kufuata taratibu.
Ni kwa sababu hiyo, Askofu Katunzi na wenzake waliamua kufungua shauri la madai Mahakamani na ikatolewa amri ya kuzuia mkutano lakini  haikuheshimiwa na badala yake  mkutano ukafanyika na viongozi wa muda wakateuliwa.

Alhamisi, 28 Julai 2016

PAPA FRANCIS AANGUKA GHAFLA AKIONGOZA MISA POLAND

 
Kiongozi wa Kanisa Katoliki duniani, Papa Francis amepata ajali ya kuanguka ghafla alipokuwa akitembea kuelekea kwenye jukwaa lililoandaliwa kwa ajili ya kuendesha ibada, Czestochowa nchini Poland.

Jumanne, 26 Julai 2016

MCHUNGAJI ANTHONY LUSEKELO ANENA MAZITO KUHUSU LOWASSA

Mchungaji wa Kanisa la Maombezi (GRC) la Ubungo jijini Dar es Salaam, Anthony Lusekelo maarufu ‘Mzee wa Upako’ amesema kitendo cha viongozi wa CCM kulitaja zaidi jina la Edward Lowassa katika Mkutano Mkuu Maalumu wa chama hicho ni ishara kuwa Waziri Mkuu huyo wa zamani ni tishio.

Jumamosi, 16 Julai 2016

RAIS MAGUFULI AFANYA UTEUZI WA VIONGOZI NA WATENDAJI WA TAASISI ZA SERIKALI NA AWAPANDISHA VYEO MAAFISA WA POLISI



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli kwa mamlaka aliyopewa amefanya uteuzi wa viongozi na watendaji wa taasisi mbalimbali za Serikali, na pia amewapandisha vyeo maafisa wa Jeshi la Polisi Tanzania.
Uteuzi huo ni kama ifuatavyo;

1.   Mhe. Augustino Lyatonga Mrema.
·        Ameteuliwa kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Taifa ya Parole kwa kipindi cha miaka mitatu, kuanzia leo tarehe 16 Julai, 2016.

·        Mhe. Augustino Lyatonga Mrema anachukua nafasi iliyoachwa wazi na Jaji Mstaafu Mhe. Eusebia Nicholaus Munuo ambaye muda wake umemalizika.

2.   Prof. William R. Mahalu
·        Ameteuliwa kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete. Uteuzi huu umeanza leo tarehe 16 Julai, 2016.

3.   Prof. Mohamed Janabi
·        Ameteuliwa kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete. Uteuzi huu umeanza tarehe 15 Julai, 2016.

4.   Prof. Angelo Mtitu Mapunda
·        Ameteuliwa kuwa Kamishna wa Tume ya Utumishi wa Mahakama kwa kipindi cha miaka mitatu. Uteuzi huu umeanza tarehe 15 Julai, 2016.

5.   Bi. Sengiro Mulebya
·        Ameteuliwa kuwa Kamishna wa Tume ya Utumishi wa Mahakama kwa kipindi cha miaka mitatu. Uteuzi huu umeanza tarehe 15 Julai, 2016.

6.   Bw. Oliva Joseph Mhaiki
·        Ameteuliwa kuwa Mwenyekiti wa Tume ya Utumishi wa Walimu (TSC). Uteuzi huu umeanza tarehe 15 Julai, 2016.

7.   Mwl. Winifrida Gaspar Rutaindurwa
·        Ameteuliwa kuwa Katibu wa Tume ya Utumishi wa Walimu (TSC). Uteuzi huu umeanza tarehe 15 Julai, 2016.

8.   Dkt. Charles Rukiko Majinge
·        Ameteuliwa kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya wadhamini ya Hospitali ya Taifa Muhimbili. Uteuzi huu umeanza leo tarehe 16 Julai, 2016.

9.   Dkt. Julius David Mwaiselage
·        Ameteuliwa kuwa Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taasisi ya Saratani ya Ocean Road. Uteuzi huu umeanza tarehe 15 Julai, 2016.

DK. KIGWANGALLA- “TUTATATUA MGOGORO WA WANAKIJIJI NA HIFADHI YA MSITU WA IPALA KWA MAZUNGUMZO”

Mbunge wa Nzega Vijijini ambaye pia ni Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mhe. Dk. Hamisi Kigwangalla akiwasili kwenye kijiji cha Ipala huku akipokelewa na baadhi ya wananchi wa vijiji hivyo.Msululu wa wananchi wakiwa wamempokea Dk. Kigwangalla wakati akiwasili kwenye kijiji cha Ipala.

Ijumaa, 1 Julai 2016

MARUFUKU WANANCHI KUKATWA ASILIMIA 18 YA VAT KATIKA HUDUMA MBALIMBALI ZA TAASISI ZA FEDHA NA SIMU


Kamishina Mkuu wa Mamalaka ya Mapato Nchini (TRA ), Alphayo Kidata akizungumza na waandishi habari juu zuio la taasisi za fedha na kampuni za simu kukata miamala ya kodi ya ongezeko la thamani VAT leo jijini Dar es Salaam, Kulia ni Kamishina wa Mapato ya Ndani wa TRA, Elijah Mwandumbya. 

RAIS KAGAME AWASILI NCHINI-APOKEWA NA MWENYEJI WAKE RAIS DKT. MAGUFULI


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akisalimiana na Rais wa Rwanda Paul Kagame mara baada ya kuwasili katika uwanja wa ndege wa kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere jijini Dar es Salaam.