YESU NI JIBU

Ijumaa, 24 Agosti 2012

Fundi akijaribu kutafuta ufumbuzi wa umeme ambao umejitokeza wakati wa mahubiri ya neno la Mungu katika mkutano ulikuwa ukiendelea huko kwembe mbezi wilaya ya Kinondoni jijini Dar es salaam
 Waumini wakinyoosha mikono juu wakati wa maombi na maombezi

Mwinjilisti wa Kimataifa Andulile Bwile akiwa jukwaani akihubiri neno la Mungu katika viwanja vya CCM kwembe Mbezi jijini Dar es saalam


Imeelezwa kuwa ni vyema waumini wa dini zote kusimamia na kufuata sheria bila shuruti kwa lengo la kudumisha amani na usalama katika taifa la Tanzania sambamba na kuachana na uovu kwani wanaotenda maovu kwa asilimia kubwa ni watu wa dini.

Kauli hiyo imetolewa na mwinjilisti wa kimataifa Andulile Bwile jijini Dar es saalam katika mkutano wa injili ambao umeandaliwa na kanisa la EAGT kwembe ambapo amesema kuwa kuna watu wanafanya kazi ambazo hazipendezi mbele za Mungu na bado hawapendi kuitwa kwa majina ya kazi wanazozifanya.

Aidha mwinjilisti Bwile amesema kuwa unamkuta mtu ni mwasherati ni mzinzi,mlevi,mchawi,fisadi mwizi,muuaji lakini hapendi kutajwa kwa jina la kazi anazo fanya maana mtu hutajwa kwa kazi anazofanya kama ni fundi huitwa fundi mwandishi huitwa kwa jina la kazi yake kwanini wewe ukatae na unafanya hayo yote.

Kwa sasa asilimia kubwa ya watu wanaofanya makosa na uovu ni watu wenye dini,na dini zimekuwepo kwa muda mrefu lakini zimeshindwa kumbadilisha mwanadamu maana hawana huruma Yesu pekee ndiye mwenyeupendo kwa mwanadamu na ndiyo maana amekuja kwa lengo la kumkomboa mwanadamu ili kuacha uovu wake.

Kutokana na hayo ni vema basi waumini wote kuwa makini na kumfuata Yesu maana yeye ndiye mwenye uwezo wa kuokoa na kusamehe dhambi pamoja na kuponya magonjwa yanayowakabili wanadamu bila kujadi dini na hapo mabadiliko yanaweza kutokea na uponyaji wa taifa kwa ujumla