Aidha katika mkutano huo wa siku nane
watu wengi walishuhudia kufunguliwa na wengine kupokea uponyaji kupitia wapo
redio ambyo imekuwa ikirusha matangazo hayo moja kwa moja kutoka katika viwanja
hivyo vilivyoko jijini Dar es salaam.
Mkutano huo umeandaliwa na umoja wa
makanisa ya Dar es salaam na kuhudhuriwa na waumini wa makanisa hayo pamoja na
wachungaji mbalimbali.
Watumishi mbalimbali walihudhuria na
kuhudumu katika mkutano huo ambao kila siku maombi na maombezi hufanyika kwa
ajili ya kuliombea amani Taifa na uchaguzi mkuu wa octoba mwaka huu.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni