1.Kuabudu
maana yake ni nini?
Answer:Ni tendo linalogusa
akili,hisia,nafsi na utu wa mtu na mwili pia kwa kusujudu,kuanguka
kifudifudi,au uso kwa uso.
Mwanzo 17:3
Kuabudu katika Roho na Kweli kunaweza
kukafanywa wakati wowote na mahali popote mradi lengo ni kufanyia Mungu Ibada.
2.Kwa
nini malkia esta alimwaambia Mordekai
awakusanye wayahudi na wakufunga na kuomba bila kula wala kunywa kwa muda wa
siku tatu usiku na mchana kwa ajili yake,naye atafanya hivyo pamoja na wajakazi wake
Answer:
Kwa lengo la kuingia kwa mfalme
,kinyume cha sheria(maana Hamani amepanga wayahudi wote katika ufalme wa
Ahusero waangamizwe na kupanga kuwa hamani atundikwe Esta 3,4)esta 4:16-17.
3.Karama ya kupambanua Roho inatolewa
kwa lengo Gani?
Jawabu:
Jawabu:
1.
kutambua chanzo cha miujiza ,ishara
na maajabu matendo 8:4-13
2.
Kutambua mawakala wa ibilisi matendo
13:6-12
3.
Kutambua aina ya roho chafu
zinazotenda kazi matendo 16:16-18
4.
Kutambua vyanzo vya magonjwa na
udhaifu katika miili na nafsi za watu mathayo 12:22-23
5.
Kutambua mafundisho potofu au ya
uongo waebrania 1:1-2; 1thethalonike 4:13-17
4.Toa
maana sita za rafiki wa kweli kwa mfumo wa kiblia ni nani?
Jawabu:
1. Rafiki ni mtu anayekupenda
(yohana15:12)
2.ni mtu aliyetayari kujitoa maisha
kwa ajili ya marafiki zake(yohana 15 :13) Yesu pia alionesha hilo kwa kutufia
msalabani (rumi 5:8)
3.ni mtu ambaye yupo tayari
kukutendea lile jema utakalomwomba akutendee (yohana 15:14)
4. ni mtu anayehusika na kushirikiana
nawe(yohana15:15)
maombezi ,mafundisho na makemeo ya urafikiYesu
anainua ,kuponya na kuadibisha.
5.ni yule anayejitolea kwa hiari
kudumisha urafiki uliopo(yohana 16:16)
kujitoa kwa moyo wa hiari kulinda kudumisha uhusiano wa
kirafiki(yoh 7:17)
6.ni yule ambaye anaendelea kuchagua kuwa
rafiki wakati wengine wote wanajitenga na kukimbia kwa sababu
mbalimba(yoh15:17)