YESU NI JIBU

Jumatano, 23 Novemba 2016

MUNGU WA KWELI NI WA MATAIFA YOTE,BILA KUJALI DINI KABILA RANGI,NDIYO MAANA YEYE ANATENDA MAKUU.

Ni katika ibada na kipindi cha maombe na maombezi ambapo nguvu za Roho Mtakatifu zilishuka kwa namna ya tofauti na wengi kunena kwa lugha.
Hapa ni ndani ya ibada maombe na maombezi yakiendelea.

Ijumaa, 18 Novemba 2016

KUWA NA MTAZAMO SAHIHI KWA MUNGU WAKO NAWE UTAMTUMIKIA KWA UAMINIFU:


 Mchungaji kiongozi na pia ni askofu Geoffrey Masawe akifanya maombi madhabahuni.

MWANAMKE AFARIKI AKIOMBEWA KWA ‘NABII’ JIJINI ARUSHA ANYOLEWA NYWELE NA NYUSI.

Kamanda wa Polisi wa Mkoa, Charles Mkumbo
Mwanamke  mkazi wa Unga-Limited jijini Arusha , Lightness Kivuyo ameripotiwa kufa wakati akifanyiwa maombi nyumbani kwa mchungaji aliyejulikana kama ‘Nabii Rajabu’ eneo la Kwa-Mrombo pia jijini Arusha.

CITY HAVERSTY INTERNATIONAL CHURCH YAWASIMIKA VIONGOZI WANANE TAYARI KWA HUDUMA.

 Mchungaji Kiongozi wa Kanisa la City Haversty International Apostle Dr Livistone Banjagala wakati akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake wakati ajiandaa kuwasimika wachungaji wa kanisa lake.

Jumamosi, 5 Novemba 2016

MAHAKAMA KUU YAZUIA KUFUKUZWA MAKAMU ASKOFU WA EAGT

Mapanga yatumika kulinda Kanisa alipozikwa Ask.Kulola,
Miaka mitatu na siku 50 hivi, tangu Askofu Mkuu na Mwanzilishi wa kanisa la Evangelistic Assemblies of God Tanzania (EAGT) DK. Moses Kulola kumaliza kazi hapa duniani, (kufariki) hali si shwari ndani ya kansia aliloacha, baada ya Makamu Askofu Mkuu, John Maene kufukuzwa katika uongozi na uchungaji katika kanisa la Bungando, Mwanza, lilipo kaburi la mwanainjili huyo na kuzua kiza kinene katika mustakabali wa kiroho.
Habari za ndani toka ndani ya kanisa hilo zinaeleza kuwa tangu kutwaliwa kwa kiongozi huyo, ilizuka hali ya sintofahamu kwa kile kilichodaiwa kuwa ni kutoelewana baina ya wale wanaoelezwa kuwa ni “wa Kulola” yaani wafuasi wake  sugu na wale wa kizazi kipya kinachotaka kubadili mambo na kujenga himaya mpya.
Ni katika hali hiyo, hivi karibuni aliyekuwa Makamu Askofu Mkuu wa Kanisa hilo, John Maene, alifukuzwa uongozi na uchungaji kwa kile kilichodaiwa kuwa alipatikana na tuhuma za ukiukaji wa kimaadili, lakini akapinga tuhuma mbele ya Halmashauri ya kanisa na kasha kufungua Kesi katika mahakama Kuu kanda ya Mwanza.