YESU NI JIBU

Jumatano, 27 Januari 2016

WAZIRI NAPE NAUYE ASEMA KUWA TELEVISHENI YA TAIFA TBC HAINA FEDHA YA KUJIENDESHA KURUSHA MATANGAZO YA BUNGE MOJA KWAMOJA (LIVE)

Posted by on Wednesday, January 27, 2016

Jumanne, 26 Januari 2016

MTUME NA NABII BETHANIA SIMON MWASISI NA MBEBA MAONO YA OPERATION NIBEBE NAMI NIKUBEBE UPOKEE YOTE.









Mtumishi wakweli wa Mungu hapaswi kuficha mafunuo yake,anapaswa kuyatangaza maana sio bangi bali ni habari njema kwa watu wote,labda wanao ficha hawayaamini mafunuo yao kuwa ni ya Mungu Yehova Bwana wangu,waweke wazi kama mimi hapa.
Ufunuo huu ni kama unaleta kichekesho,na kwa wale walio mwilini huenda wasinielewe kabisa,lakini ni ufunuo wenye maana kubwa sana kibibilia.
Nime anza operation nibebe na mimi nikubebe,au tubebane ili tufike,kama watu hawawezi kubebana basi maana yake ni kwamba mtasimama milele na hamtakuja kutembea ili mfike kule mtakako kwenda.
Tokea huu ufunuo uje kupitia mimi hapa,watu hufunguliwa pindi ninapo kuwa nahubiri huku nimebebwa dede juu kwa juu,kanisa limeanza kuongezeka kwa kasi kubwa,watu wanatoa shuhuda za ajabu sana.
Nashauri watumishi waumini na wa Tanzania wote muanze kubebana juu kwa juu,na tuweke wazi mafunuo yetu maana sio bangi wala meno ya tembo.
 Karibuni mezani Maana wa Tanzania wengi huongozwa na hofu badala ya kweli iliyo mioyoni mwao.





Waumini  wakiwa katika ibada

Jumatatu, 25 Januari 2016

RAIS MAGUFULI AMETENGUA UTEUZI WA BWANA DICKSON E. MAIMU, MKURUGENZI MKUU WA MAMLAKA YA VITAMBULISHO VYA TAIFA

 Rais Dk. John Magufuli ametengua uteuzi wa Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA), Dickson Maimu (pichani).

Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue akifafanua moja ya swali lililoulizwa kutoka kwa mmoja Waandishi wa habari (hayupo pichani) kuhusiana na suala zima la kusimamishwa kwa Mkurugenzi wa NIDA,katika mkutano na waandishi wa habari, uliofanyika Ikulu jijini Dar es Salaam mapema leo, kuhusu uamuzi wa Rais Magufuli kutengua uteuzi wa Mkurugenzi wa NIDA, Dickson Maimu.
 Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue akizungmza katika mkutano na waandishi wa habari, Ikulu Dar es Salaam leo, kuhusu uamuzi wa Rais Magufuli kutengua uteuzi wa Mkurugenzi wa NIDA, Dickson Maimu




1.1 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli, ametengua uteuzi wa Bwana Dickson E. MAIMU, Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa kuanzia leo, tarehe 25 Januari, 2016.

1.2 Aidha, baada ya utenguzi huo, Bwana Dickson E. MAIMUamesimamishwa kazi kupisha uchunguzi, pamoja na wafuatao:

1.2.1    Bwana Joseph MAKANI, Mkurugenzi wa TEHAMA
1.2.2.   Bi Rahel MAPANDE, Afisa Ugavi Mkuu
1.2.3    Bi Sabrina NYONI, Mkurugenzi wa Sheria
1.2.4    Bwana George NTALIMA, Afisa usafirishaji

1.3  Taarifa zilizomfikia Rais zinaonesha kuwa NIDA hadi sasa imetumia Sh.179.6 bilioni. Kiasi hiki ni kikubwa na Rais angependa ufanyike uchunguzi na ukaguzi jinsi fedha hizi zilivyotumika, maana Rais amekuwa akipokea malalamiko ya wananchi kuhusiana na kasi ndogo ya utoaji wa Vitambulisho vya Taifa.

1.4 Hivyo, Rais ameelekeza Mamlaka ya Udhibiti wa Manunuzi ya Umma (PPRA) wafanye ukaguzi maalum wa manunuzi yote yaliyofanywa na NIDA.

1.5 Rais pia ameelekeza Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali afanye ukaguzi maalum wa hesabu za NIDA, ikiwemo ukaguzi wa “value for money” baada ya kuthibitisha idadi halisi ya vitambulisho vilivyotolewa hadi sasa.

1.6 Rais vile vile ameelekeza Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa ifanye uchunguzi kujiridhisha kama kulikuwa na vitendo vya rushwa au la.

2.0  Wizara ya Mambo ya Nje, Afrika Mashariki na Ushirikiano wa Kikanda na Kimataifa

2.1 Aliyekuwa Naibu Waziri wa Mambo ya Nchi za Nje na Ushirikiano wa Kimataifa kwenye Serikali ya Awamu ya Nne, Mhe. Mahadhi Juma MAALIM ameteuliwa kuwa Balozi wa kwanza wa Tanzania nchini Kuwait, kufuatia uamuzi wa Serikali kufungua Ofisi ya Ubalozi katika nchi hiyo rafiki.

2.2  Rais ameagiza Wizara ya Mambo ya Nje, Afrika Mashariki na Ushirikiano wa Kianda na Kimataifa kuwarejesha nyumbani mara moja Mabalozi wawili ambao mikataba yao imeisha. Leo hii Mabalozi hao wanatakiwa kukabidhi kazi kwa Afisa Mkuu au Mwandamizi aliye chini yao. Mabalozi hao ni:

2.2.1    Bi Batilda Salha BURIANI, aliyeko Tokyo, Japan
2. 2.2   Dkt. James Alex MSEKELA, aliyeko Rome, Italia.

2.3 Rais amemrejesha nyumbani Balozi wa Tanzania aliyeko London, Uingereza, Bwana Peter Allan KALLAGHE. Anarejea Wizara ya Mambo ya Nje, Afrika Mashariki na Ushirikiano wa Kikanda na Kimataifa atakapopangiwa kazi nyingine.

2.4  Kwa maana hiyo, vituo vya Ubalozi vifuatavyo viko wazi:

2.4.1  London, kufuatia kurejea nchini kwa Balozi Peter A. KALLAGHE

2.4.2    Brussels, kufuatia aliyekuwa Balozi, Dkt. Deodorous KAMALAkuchaguliwa kuwa Mbunge.

2.4.3    Rome, Italia, kufuatia kuisha kwa mkataba wa Dkt. James Alex MSEKELA.

2.4.4    Tokyo, Japan, kufuatia kuisha kwa mkataba wa Bibi Batilda BURIANI

2.4.5    Kuala Lumpar, Malaysia, kufuatia aliyekuwa Balozi, Dkt. Aziz Ponray MLIMA, kuteuliwa kuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje, Afrika Mashariki na Ushirikiano wa Kikanda na Kimataifa.

2.4.6    Brasilia, Brazil, kufuatia kustaafu kwa aliyekuwa Balozi, Bwana Francis MALAMBUGI.

3.0   Tawala za Mikoa

3.1 Rais ametengua uteuzi wa Eng. Madeni Juma KIPANDE kabla hajathibitishwa kwenye cheo cha Katibu Tawala wa Mkoa wa Katavi kutokana na utendaji kazi usioridhisha.

4.0       Utumishi wa Umma

3.2  Nachukua nafasi hii kuwahimiza viongozi wote katika Utumishi wa Umma, na watumishi wote wa umma, kubadilika kwa dhati kwenye utendaji wao na uadilifu wao.

3.3 Napenda kusisitiza kuwa Rais na sisi tunaomsaidia hatuoni raha kuchukua hatua dhidi ya viongozi na watumishi wengine. Tungependa kila mtu mwenyewe ajirekebishe na kutomfikisha Rais mahali ambapo inabidi amchukulie hatua. Mambo yafuatayo ni muhimu:

4.2.1 Kila kiongozi na kila mamlaka ya nidhamu isipate kigugumizi kusimamia utendaji na maadili ya kazi.

4.2.2 Kila kiongozi na kila mamlaka ya nidhamu asipate kigugumizi kuchukua hatua za nidhamu, lakini afanye hivyo kwa kuzingatia kwa ukamilifu sheria, kanuni na taratibu katika Utumishi wa Umma.

4.2.3   Lazima uongozi na watumishi wa umma wawahudumie wananchi kwa haki, weledi, uadilifu na heshima. Kwa sababu hiyo:

a)  Kila ofisi ya Serikali iwe na dawati la kusikiliza shida za wananchi na kuzitafutia ufumbuzi.

b) Kwenye kila Ofisi ya Mkuu wa Mkoa na Ofisi ya Mkuu wa Wilaya wajenge uwezo wa kushughulikia shida za wananchi kwa ukamilifu na kwa wakati. Kwa muundo wa Serikali yetu hakuna sababu kwa mwananchi kufunga safari mpaka Ikulu Dar es Salaam kwa kuamini kuwa ni Rais tu anayeweza kumaliza matatizo yake, maana wawakilishi wa Rais wako kila pembe ya nchi yetu. Ikibidi wananchi wafike Ikulu ina maana hao wawakilishi wa Rais hawakutimiza wajibu wao.

c)  Kuanzia sasa watumishi wote wa umma wavae majina yao ili iwe rahisi kwa mwananchi kumtambua anayemhudumia na hivyo kumsifu mtumishi wa umma anayewahudumia kwa weledi, uaminifu na kwa wakati, na kumtolea taarifa yule anayefanya mambo ya hovyo.

d) Kila ofisi ya Serikali iwe na utaratibu wa kupokea maoni ya wananchi kuhusu huduma inayotolewa kwenye ofisi hizo, na kushughulikia haraka maeneo yote ambayo wananchi wataonesha kutoridhika na huduma.

                                                            
Gerson Msigwa
Kaimu Mkurugenzi wa Mawasiliano, IKULU

25 Januari, 2016








MHANDISI GEORGE SAMBALI ATEULIWA KUWA KAIMU MKURUGENZI MKUU WA MAMLAKA YA VIWANJA VYA NDEGE TANZANIA (TAA)

WAZIRI wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Mh. Profesa Makame Mbarawa amemteua aliyekuwa Mkurugenzi wa Kiwanja cha Ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA), Mhandisi George Sambali kukaimu nafasi ya Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), kufuatia kifo cha aliyekuwa Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka hiyo, Mhandisi Suleiman S. Suleiman.

Mhandisi Suleiman alifariki dunia tarehe 18 Januari, 2016 wakati akipelekwa katika hospitali ya Aga Khan, Dar es Salaam baada ya kuishiwa nguvu ghafla akiwa katika mazoezi ya kuogelea katika eneo la Feri, jijini Dar es Salaam.

Akitangaza uteuzi huo kwa niaba ya Waziri Mbarawa mbele ya Menejimenti ya TAA Jumatano tarehe 20 Januari, 2016 katika Ofisi za Makao Makuu ya Mamlaka hiyo kwa niaba ya Mh. Waziri, Katibu Mkuu Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Sekta ya Uchukuzi, Dkt. Leonard Chamuliho, alisema uteuzi wa Mhandisi Sambali umeanza rasmi tarehe 20 Januari, 2016.

Jumapili, 24 Januari 2016

WITO LIMEENDELEA KUTOLEWA NA BASATA KWA WAIMBAJI WA NYIMBO ZA INJILI KUJISAJILI KWA LENGO LA KUPATA STAHIKI ZAO.


BARAZA la Sanaa la Taifa (Basata) limezidi kutoa wito kwa Waimbaji wa muziki wa Injili kujisajili katika baraza hilo ili stahiki zao zitambulike inavyotakiwa.

Mkurugenzi wa ukuzaji Sanaa na Mtukio wa Basata, Maregesi Kwirujira Ng’oko alisema waimbaji wengi wa muziki wa Injili wa Tanzania kuzingatia hilo.

Ng’oko alisema kujisajili Basata kuna faida na fursa nyingi ambazo ni msaada ambao utasaidia kupata haki zao kupitia kazi zao.

Ng’oko alisema kwa kuwa wao ndio wasimamizi wa kazi za sanaa ni jukumu lao kuwakumbusha mara kwa mara wasanii kujisajili.

Aidha Ng’oko alisema wanatoa salamu hizo kwa wasanii pindi inapotokea mikinzano katika ufanikishaji wa kazi zao.

Naye Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya maandalizi ya Tamasha la Pasaka, Abihudi Mang’era alisema wanafikiria kuongeza msukumo kwa waimbaji wa muziki wa Injili kuhusu kujisajili Basata katika baadhi ya matukio.

Mang’era alisema wanafikiria kutoa elimu ya kujisajili Basata katika matamasha yao ama kusaka namna ya kufanikisha utambuzi wa waimbaji katika baraza hilo.


Jumamosi, 23 Januari 2016

,HUKO NCHI DEMOKRASIA YA CONGO MTU MMOJA AJIITA MUNGU KAMA YULE WA HUKO NCHINI KENYA AMBAYE ALIJIITA MUNGU NA BADO AMEFARIKI.


Unaweza ukawa na maswali mengi katika maisha yako ila kumbuka maandiko yanavyosema juu ya siku za mwisho,kuwa watatokea manabii wa uongo,na watawadanganya wengi.
Ndugu msomaji wa blog hii hili sasa ni tukio la pili la mwanadamu kujiita mungu mara baada ya yule raia wa Kenya ambaye naye alijiita mungu na hatimaye akafariki baada ya kuugua ila waumini wake walikataa na kusema hajafariki wakati ni tukio la kweli kuwa amefariki.
Sasa hapa ni nchini Demokrasia ya Congo huyu naye anajiita mungu,ila ikumbukwe kuwa na hata Tanzania alishawahi kutokea mtu mwingine naye alijiita Adamu wa pili ila naye alifariki na waumini wake yaani wafuasi nao walidai kuwa amepaa kwenda mbinguni jambo ambalo lilionekana kuwa sio la kweli.
Source ITV,
MSOMAJI WA BLOG HII TUPE MAONI YAKO,

HUKO NCHI DEMOKRASIA YA CONGO AJIITA MUNGU KAMA YULE WA HUKO NCHINI KENYA AMBAYE ALIJIITA MUNGU NA BADO AMEFARIKI.

Jumatatu, 11 Januari 2016

KANISA LA ANGLIKANA TANZANIA DAYOSISI YA VICTORIA NYANZA (DVN) LILILOPO JIJINI MWANZA, LIMEMTIMUA RASMI ASKOFU KANISA HILO, BONIFACE KWANGU, KUTOKANA NA UBADHILIFU WA wa MAMILIONI YA FEDHA.


 Mwenyekiti wa nyumba ya wahudumu wa kanisa la Anglikana Dayosisi ya Victoria Nyanza ,mchungaji Andrew Kashilimu akisoma tamko la wachungaji.
Askofu huyo ni wa pili kutimuliwa na uongozi wa kanisa hilo baada ya mwaka 2007 aliyekuwa Askofu wa dayosisi hiyo, John Changae na yeye kufukuzwa kutokana na matumizi mabaya ya madaraka kitendo ambacho kinaonesha taswira mbaya kwenye kanisa hilo.

Jumanne, 5 Januari 2016

WAUMINI WAMGEUZIA KIBAO MCHUNGAJI WAO BAADA YA KUGUNDUA ANACHEPUKA NA WAUMINI.



Vurugu kubwa zimeibuka katika ibada ya kanisa la Ebeneza la Kipentekoste wakimshusha mchungaji kiongozi wa kanisa hilo Musa Mlezi madhabahuni wakimtuhumu kuendesha kanisa hilo kinyume cha maadili na kuendekeza vitendo vya udharirishaji wa wanawake.
Chanzo ITV.

Jumapili, 3 Januari 2016

KILA MTANZANIA ATAKIWA KULIOMBE TAIFA AMANI ILI AMANI NA USALAMA UENDELEE KUDUMU NA WANANCHI WAINULIWE KIUCHUMI.

Watanzania wametakiwa kuliombea taifa amani ili liendelee kudumu katika hali ya utulivu upendo na mshikamano na kuepukana na machafuko yanayoweza  kutokana na viongozi kushindwa kuongoza kwa haki na hivyo kujenga chuki miongoni mwa wananchi wake.

Ijumaa, 1 Januari 2016

HOJA YA ASKOFU GAMANYWA JUU YA VITU AMBAVYO HAVINA MAANA YA KUMALIZA MWAKA


Kumaliza mwaka sio tu kubadilisha namba ya mwaka toka 2015 kwenda 2016. Kubadilisha namba hakuleti mabadiliko yoyote zaidi ya kubadili namba tu.

Na wala kumaliza mwaka hakuna maana ya kubadilika kwa mazingira toka kwenye uchakavu kwenda kwenye upya. Wala kubadili mwaka sio kuondoa changamoto za maisha ulizokuwa nazo na kuingia kwenye maisha raha bila masumbufu yoyote ya maisha.