Kuwa na kiburi kutokana naulichonacho imeelezwa kuwa ni
mojawapo ya njia zinazobasabaisha mwaminini asiweze kupokea Baraka zake kutoka
kwa Mungu kwani kiburi kinamfanya mwamini kujiona kuwa bora kuliko mwingine.
Kauli hiyo ilitolewa
hivi karibuni na askofu mkuu wa WAPO Mission international askofu Silvester
Gamanya wakati akifundisha juu ya somo la kiburi kwenye mchesha uliofanyika
katika ukumbi wa BCIC Mbezi beach jijini Dar se saalam.
Kiburi ni tatizo kubwa linalowakabili waumini wengi kwenye
madhehebu yao na dini zao na suala hilo linasababisha uwepo wa Mungu kuwa na
mipaka ndani ya waumini,ni vyema kila mwamini kwa nafasi yake kukataa na
kupinga kwa juhudi zote juu ya tatizo hilo la kiburi lisiwepo ndani ya maisha
yake.
Mwanadamu anaweza kuwa na kiburi ya mali ,elimu aliyonayo
ama fedha na inasababisha mwanadamu huyo kujiona kuwa hakuna kinachoweza
kumkwamisha ama kumzuia katika maisha yake kufanya jambo ambalo kwa ukweli ni
kujidanganya katika maisha yake.
Alisema kuwa na elimu fedha na utajiri wa kila aina ni
vizuri kila mwanini ama mwanadamu asiwe na kiburi maana ni mbaya sana kiasi kwamba inasababisha hata pamoja na kuwa
na vitu hivyo kuonekana kuwa haufai mbele za Mungu na mbele za wanadamu.
Mkesha huo ni mfululizo ya mikesha ya urejesho ambayo
hufanyika kila mwisho wa mwenzi katika vituo vya BCIC Mbezi beach na BCIC
temeke na huwa maombi na maombezi hufanyika kwa wale wenye shida na matatizo
mbalimbali katika maisha yao na watu wengi hufunguliwa.
Kutokana na hayo askofu amekuwa akifundisha kwa umakini na
ufasaha zaidi juu mafundishao yanayohusu maisha ya wanadamu pamoja na kuwepo
kwa malalamiko ya waumini kulalamikia hali ngumu ya maisha basi njia pekee ya
kupata ufumbuzi ni kumwamini bwana Yesu.