YESU NI JIBU

Jumatano, 31 Oktoba 2018

KUMTAMBUA THAMANI YA YESU MWISHO WA MATATIZO


Kanisa likitambua thamani ya kristo Yesu haliwezi kuyumbisha na kitu chochote hata kama litapita katika changamoto litabaki na msimamo wa kumpenda yesu katika imani na kuvumilia mateso yote.
Amesema hayo mchungaji Isaac Mwanjabeki wa kanisa la T.A.G Gongo La Mboto Solomoni Temple jijini Dar es salaam kwamba kanisa la leo linatakiwa liwe na uvumilivu katika kumtumikia Mungu pia lijifunze  kupitia kanisa la simina katika kitabu cha ufunuo.
Mchungaji Mwanjabeki amewasihi watu wanaopitia nyakati ngumu za kimaisha kutokata tamaa na kuwa na subira kwa Mungu kwakuwa jaribu lina muda wake upo wakati litapita.
Mungu huwaangalia walio waaminifu na wavumilivu hasa pale unapopitia majaribu ni vyema kukaa karibu zaidi nae ili uone ukuu wake.


Jumatatu, 14 Mei 2018

UBALOZI WA MAREKANI KUHAMIA JERUSALEM NA WATU 37 WARIPOTIWA KUFARIKI DUNIA:

Mamia ya watu wamejeruhiwa, kwa mujibu wa maafisa wa Palestina


Haki miliki ya pichaAFP
Image captionMamia ya watu wamejeruhiwa, kwa mujibu wa maafisa wa Palestina

Raia 37 wa Palestina wameuawa na wengine 1,300 wamejeruhiwa na wanajeshi wa Israeli katika mapigano katika mpaka wa Gaza, maafisa wa Palestina wanasema.

Jumamosi, 3 Machi 2018

KUKOMBOA WAKATI SIO KWENDA NA WAKATI:


Na Stelius Sane,
Imebainika kuwa kila mmoja akikomboa wakati badala ya kwenda na wakati atafanikiwa katika maisha yake kiuchumi,kiafya,kisiasa na hata kiroho kutokana na kuwa katika wakati sahihi wa kile anachokifanya.

Jumatano, 21 Februari 2018

MWINJILISTI WA KIMATAIFA BILLY GRAHAM AFARIKI DUNIA AKIWA NA MIAKA 99:

Mwinjilisti wa kimataifa kutoka nchini Marekani, Billy Graham (William Franklin Graham) amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 99 nyumbani kwakwe, North Carolina.Kwa mujibu wa vyanzo mbalimbali vya habari ikiwemo Sky News, NBC, New York Times,

KULINDA MOYO NI KUPONYA ROHO NA MWILI:


Imebainishwa kuwa kulinda moyo ni ia mojawapo ya kuepukana na magonjwa yanayoweza kushambulia mwili sanjari ya kuepukana na vifo vinavyotokana na magonjwa ya moyo.
akifundisha somo la namna ya kulinda moyo na Bi Monica lawrent ambaye yupo chini ya huduma  ya mwana wa Adamu alikuja kutafuta na kuokoa kilichopetea  inayongozwa na mtumishi Saimon Jonath iliyopo mkoani Morogoro ambapo amesema kuwa ili kuepukana na magonywa yanayoshambulia moyo na kuonekana katika mwili na roho ni kulinda moyo kama biblia inavyosema.

Jumanne, 20 Februari 2018

WAUMINI WASHAURIWA KUHUBIRI JUU YA UFALME WA MUNGU:


Askofu mkuu wa kanisa la Faith Community Pentecoste Church (FCPC) lililopo Mbezi Maramba mawili jijini Dar es salaam,Barthelomeo Sheggah amewataka wakristo kuhibiri juu ya ufalme wa mbinguni ikiwa ni njia pekee ya kulijenga kanisa la Mungu kulingana na misingi ambayo Yesu alituwekea tangu mwanzo 

Akizungumza katika Ibada wiki iliyopita Askofu Sheggah ameuelezea kuwa ufalme huo ni katika ulimwengu ambao hauonekani kwa macho ya kawaida bali kanuni zake zipo na zinafundishika 

Ijumaa, 16 Februari 2018

TANGAZAJI NA MWIMBAJI WA NYIMB0 ZA INJILI AACHIA VIDEO MPYA YA VIWANGO VINGINE FULLY HD


Mtangazaji na mwimbaji wa nyimbo za injili Costantino Elia Pius ameamua kutoa  Video ya wimbo wake VIWANGO VINGINE ambayo unaweza kupata kwenye Youtube 

Jumatano, 7 Februari 2018

Jumatatu, 22 Januari 2018

MAOMBI YA VIONGOZI WA DINI HULETA MABADILIKO MAKUBWA KWA TAIFA.

Askofu Mkuu wa Nyumba ya Huduma ya Abundant Blessing Centre, Flaston Ndabila ambaye ndiye Mratibu wa maombi hayo akizungumza kwenye ibada ya maombi iliyofanyika leo jijini Dar es Salaam.
Askofu Mkuu wa Nyumba ya Huduma ya Abundant Blessing Centre, Flaston Ndabila, akimkaribisha Waziri wa HabariUtamaduni, Sanaa na Michezo, Dk. Harrison Mwakyembe kwenye ibada hiyo mara baada ya kuwasili.

Jumatano, 17 Januari 2018

BROFOA HUTOA ELIMU BORA KUWASAIDIA WALIOKATA TAMAA NA KUSHINDWA KUENDELEA NA ELIMU

Mkurugenzi wa Brothers Academy Ndugu Robart Rwezaura akizungumza jambo na waandishi wa habari.
 Na Stelius Sane,
Imebaishwa kuwa elimu ambayo hutolewa katika mfumo usio rasmi imekuwa msaada mkubwa sana Kwa wale ambao walishindwa kupata elimu katika mfumo rasmi kutokana Na matatizo mbalimbali ya kifamilia ama sababu zingine.
Kauli hiyo imetolewa Na mkurugenzi wa brothers font of academy ndugu Robart Rwezaura wakati akizungumza Na gazeti hili ambapo alisema kuwa mfumo usio rasmi umekuwa mkombozi wa kielimu Kwa wale watu walioshindwa kusoma Katika mfumo rasmi.