2. Onyesha mazingira ya makaribisho ya urafiki na upendo.
3. Ukarimu ni njia ya kawaida ya kuelezea uelewa na kujali
kwako kwa mshauriwa.
4. Ukarimu huwa huonyeshwa kwa vitendo kama vile:
• Ishara zako unavyo zionyesha kwa mshauriwa.
• Mwonekano wa mwili wako ulivyo.
• Kiimbo cha sauti (tone of voice) Ikiwa ya chini sana
mshauriwa anaweza kudhani hujafurahia ujio wake. Pia ikiwa
ya juu sana mshauriwa anaweza kukuogopa akadhani wewe ni mkali sana.
• Mguso wa mwili (unagusa wapi na unagusaje gusaje, kuna
wengine wakisalimia nikama wanakupangusa tu kiganja
hawakushiki vizuri ni kama wanakuona una kinyaa. Wengine
wanakandamiza mikono ni kama mkono umekanyangwa na
tairi ya trekta).
• Mapigo ya moyo yanakwendaje.
• Mwonekano wa uso ukoje. N.k
AFYA YA MSHAURI COUNSELING TRAINING!
1. Kuna uhusiano mkubwa kati ya ushauri na kuwa na afya njema kimwili kama mshauri.
2. Afya ya mshauri ni ya muhimu sana katika mwonekano wa mshauri hasa kwa mara ya kwanza anapokutana na mshauriwa.
3. Kama afya yako sio nzuri ni vema ukaahirisha ushauri ili ushughulikie matengenezo ya afya yako.
Mfano:
• Kushauri huku unakikoozi kikali inaweza kuwa kizuizi katrika kazi ya ushauri
• Kushauri huku unamafua makali inaweza kuwa kizuizi katrika kazi ya ushauri.
• Kushauri huku una tatizo la kuwashwa sehemu mbalimbali na hususani sehemu za siri na kwingineko inaweza kuwa kizuizi katrika kazi ya ushauri.
• Kushauri huku una homa au mareria kali unatetemeka.
• Kufanya huduam ya ushauri huku unajisikia mdhaifu na usiye na nguvu.
4. Kama mshauri jijengee mazoea ya kufanya mazoezi ya mwili mara kwa mara.
5. Ni hatari kufanya ushauri ukiwa na msongo wa mawazo (stress).
6. Ni hatari kufanya ushauri huku umetoka kuumizwa na mtu umejeruhiwa moyo.
7. Uimara wa afya ya kimwili ya mshauri inaweza kuchangia namna atakavyoongea na mshauriwa wake na namna ambavyo mshauriwa atakavyo muona mshauri.
5. Ni hatari kufanya ushauri ukiwa na msongo wa mawazo (stress).
6. Ni hatari kufanya ushauri huku umetoka kuumizwa na mtu umejeruhiwa moyo.
7. Uimara wa afya ya kimwili ya mshauri inaweza kuchangia namna atakavyoongea na mshauriwa wake na namna ambavyo mshauriwa atakavyo muona mshauri.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni