Mamia
wajipanga barabarani kustaajabu.
Zoezi la uzinduzi wa kanisa likifanywa na mchungaji kiongozi wa kanisa la EAGT City Center mchungaji Florian Katunzi.
“Nilikuwa nimesikia habari zako, kwa kusikia kwa masikio; bali sasa jicho langu linakuona.”
Kama ilivyokuwa kwa wana wa Israeli walipotwaa kila kilicho chao na kuongozwa na wingu la uwepo wa Bwana, kutoka Misri kuelekea Nchi ya ahadi (Kanaani) ndivyo ilivyokuwa Jumapili iliyopita wakati maelfu kwa maelfu ya wana- familia ya Kanisa la EAGT City Centre, chini Mchungaji kiongozi, Florian Josephat Katunzi, walipotwaa vilivyo vyao, na kuandamana toka eneo la Viwanja vya maonyesho ya Biashara, vya Mwl. Nyerere (Sabasaba) kuelekea “Nchi ya Ahadi” Mtoni Mtongani Relini, huku mamia ya wana wa jiji la Dar es Salam, bila kujali dini zao wakijipanga bara barani na wengine kuparamia mapaa ya nyumba kustaajabia maandamano hayo ya kihistoria yaliyofunga barabara ya Kilwa kwa muda.
Zoezi la uzinduzi wa kanisa likifanywa na mchungaji kiongozi wa kanisa la EAGT City Center mchungaji Florian Katunzi.
“Nilikuwa
nimesikia habari zako, kwa kusikia kwa
masikio; bali sasa jicho langu linakuona.” Maneno
hayo yalitamkwa na mchungaji kiongozi wa kansia la EAGT City Centre, Florian
Josephat Katunzi, Jumapili iliyopita mara baada ya kukanyaga katika ardhi
lilipojengwa Kanisa la kisasa kule Mtoni Mtongani Relini akinukuu maandiko ya
Biblia katika kitabu cha Ayubu 42:5.
Ilikuwa majira ya saa saba
mchana wakati anga likiwa angavu, Bendi ya Jeshi la Polisi wakiongoza
maandamano kwa wimbo usemao: “Mwambie
Farao nimeokoka sitarudi tena misri naelekea kaanani………”
Mbele Mchungaji kiongozi akiwa sambamba na mwimbaji wa nyimbo za Injili
Tumsifu Rutufu, aliyevalia majoho kama ya Mussa na kilemba kichwani, sambamba
na viongozi wa kanisa hilo walitembea kwa miguu kuelekea mtoni Mtongani, huku
maelf ya wana-familia ya EAGT, wakibeba viti vyao na kufunga kwa muda Barabara ya Kilwa.
Waandamanaji walipofika kwenye daraja la Reli (Mtoni Mtongani,
walikunja kona kuelekea upande wa kushoto na kuchora alama ya elo, iliyokuwa
kivutio kikubwa, kisha kuingia “Kanaani” eneo lilipojengwa jengo la kisasa,
lakini la muda lenye uwezo wa kuhimili watu 3000.
Akikata utepe kukanyaga eneo hilo, Mchungaji Katunzi alisema: “Sasa
Bwana ametupa eneo hili kuwa eneo la kumuabudu na kumpa utukufu unaomstahili.
Mahali hapa hapatakuwa eneo la wachawi na vinyamkera tena, bali ni mahala pa
ushindi na kufunguliwa.”
Huku akijawa na uwepo wa nguvu za Mungu, Mch. Katunzi aliinua mikono
juu na kuwaongoza maelfu kumshukuru Mungu kwa matendo makuu aliyolifanyia
kanisa lake, akawabariki wote waliokuwa kwenye maandamano hayo na kisha kuliombe Taifa, akimsihi Mungu
alivushe salama katika matukio muhimu yanayoenda kutokea mwaka huu ikiwa ni
pamoja na uchaguzi Mkuu.
Katika hotuba fupi ya kuhitimisha tukio hilo la kiibada, Mch. Katunzi
alisema; huu ni mwaka wa uchaguzi na kanisa limeingia kwenye maombi, wagombea
wanaotegemea makafara na uchawi hawatachaguliwa kamwe, bali wale wanaomtazama
Mungu na kutumainia maombi.
JINSI YA KUFIKA EAGT CITY
CENTRE, MTONI MTONGANI (RELINI)
Kanisa liko kandoni mwa Daraja la juu la Reli ya TAZARA eneo la Mtoni
mtongani, kama hatua 100 kutoka barabara
kuu.
Unaweza kuwasiliana nasi kwa simu:
0718-267171
0754367826
0784367826
0713803057
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni