Hatimaye naibu wa rais wa Kenya William Ruto amefanikiwa kusalimiana na rais wa Marekani Barrack Obama baada ya kukosekana hapo jana katika ujumbe uliomkaribisha rais huyo alipowasili katika uwanja wa Ndege wa Jomo Kenyatta jijini Nairobi. William Ruto anakabiliwa na mashtaka ya uhalifu wa kivita katika mahakama ya ICC mjini the Hague.
Ikulu ya Nairobi kenya
Ikulu
Mkutano wa kibiashara kati ya mataifa
ya kenya na Marekani umeanza katika ikulu ya rais nchini Kenya.Rais Barrack
Obama na mwenzake wa Kenya Uhuru Kenyatta wanawaongoza wajumbe kutoka mataifa
hayo mawili katika mkutano huo.Swala la ugaidi ni miongoni mwa maswala tata
yanayotarajiwa kujadiliwa katika kikao hicho.
Rais Obama pia anatarajiwa kutia
sahihi ya mikataba ya kibiashara na mwenyeji wake rais Kenyatta katika ikulu ya
Nairobi
Rais Barrack Obama kukutana na
makamu wa rais wa kenya William Ruto ambaye anakabiliwa na mashataka ya uhalifu
wa kivita katika mahakama ya kimataifa ya ICC katika mazungumzo ya kibiashara
kati ya Kenya na Marekani yatakayoandaliwa katika ikulu ya rais.
13.50pm:Rais Obama akiweka mauaObama
Rais Barrack Obama akiweka shada la
maua katika eneo la kumbukumbu ya mauaji ya kigaidi katika uliokuwa ubalozi wa
Marekani katikati ya jiji la Nairobi
Memorial Park
Rais Obama na Uhuru Kenyatta
wawasili katika eneo la shambulizi la kigaidi katika uliokuwa ubalozi wa Marekani
katikati ya jiji la Nairobi.Baadhi ya barabara katika jiji la Nairobi zimebakia
kuwa mahame
Manusura 1998,
Raia Walionusurika shambulizi la
1998 kenya wabeba mabango wakidai kwamba hawakufidiwa.Wanamtaka rais Obama
kutowatupa na badala yake kuangalia maslahi yao.
Wachezaji densi Nairobi
Wachezaji densi ya kimasai
wakisubiri kumtumbuiza rais Barrack Obama aliyetarajiwa kuwatembelea katikati
ya jiji la Nairobi
M-kopa M-kopa
Rais Obama kwa sasa ametembelea
maonyesho ya uvumbuzi jijini Nairobi ambapo alikutana na June Muli afisa
anayesimamia maslahi ya wateja M-Kopa ambao hutoa huduma ya kawi ya jua ya 'pay
as you go' katika makaazi.
Obama-uhuru Memorial Park
Obama na Uhuru sasa waelekea katika eneo
la shambulizi la kigaidi la mwaka 1998 jijini Nairobi
Obama amaliza hotuba yake
BBC hewani moja kwa moja
Runinga ya BBC inapeperusha moja kwa
moja kongamano hilo hewa
Obama
Kenya inaongoza katika teknolojia za
kibiashara.Kwa mfano utumizi wa Mpesa-ni vyema kwamba teknolojia hiyo ilianza
hapa Kenya
Obama 'Tutazindua mfuko wa kudhamini
biashara zinazoanzishwa na wanawake
Kina mama ndio injini ya maendeleo
barani Afrika.
Vituo vitatu vitafunguliwa
Mali,Kenya na Zambia barani Afrika ili kuwasaidia wanawake wajasiriamali
Rais Obama
Rais Obama awasalimia wakenya kwa
neno 'niaje' na
Hawayuni na kusema kuwa familia yake
inatoka nchini kenya.
Lengo la mkutano huu aliouzindua
miaka mitano iliopita mjini Washington ni kuwapiga jeki wafanyibiashara
duniani.
Amesema kuwa kuna umuhimu wa
kukabiliana na ufisadi ili biashara kushamiri.
Kenya ilikumbwa na chanagamoto
chungu nzima ikiwemo majanga lakini imesimama imara na kusonga mbele.
Bara la Afrika haliwezi kutegemea
mataifa ya magharibi .
Taifa la kenya ni chimbuko la
makabila tofauti.
Mkutano wa wajasiriamali umeanza
katika makao makuu ya Umoja wa Mataifa jijini Nairobi huku Rais wa Kenya Uhuru
Kenyatta akihutubia mkutano
Msafara wa Rais Uhuru
Kenyatta Ges tweet
Msafara wa Rais Uhuru Kenyatta ukiwa
tayari umewasili katika eneo la mkutano wa wajisiriamali unaotarajiwa
kufunguliwa na raia wa marekani Barrack Obama
Waandishi habari Waandishi
Waandishi wa habari wakijiandaa
kuliangazia kongamano la kibiashara la wajasiriamali katika eneo la Gigiri jini
Nairobi.
Vifaa vya waandishi hao vimepekuliwa na maafisa wa usalama wa Marekani.
Ndege za kijeshi
Ndege za kijeshi za Marekani
zimeanza kuzunguka katika anga ya jiji la Nairobi kuimarisha usalama.
Barabara za Jijini Nairobi:
Barabara nyingi za mji wa Nairobi
zimeonekana kuwa bila watu na magari kufuatia kuwasili kwa rais Obama.Mapema
leo maafisa wa polisi walionekana katika barabara zinazoelekea katika eneo la
Gigiri ambapo rais Obama atafungua rasmi kongamano la kibiashara.
Obama na familia yake Sara Obama,Barrack Obama na Daktari
Auma
Mama Sarah Obama,Rais Obama na
dadaake Daktari Auma Obama wakijumuika katika chakula cha jioni katika hoteli
moja jijini Nairobi.
Chanzo ni BBC.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni