YESU NI JIBU

Ijumaa, 30 Oktoba 2015

SHEREHE YA KUMKABIDHI HATI YA USHINDI YA URAIS DR JOHN POMBE MAGUFULI NA MGOMBEA MWENZA SAMIA SULUHU KATIKA UKUMBI WA DIAMOND JUBILEE JIJINI DAR ES SALAAM.

Zoezi la kukabidi hati ya  ushindi kwa mshindi wa chama cha mapinduzi ccm ndugu John pombe magufuli na mgombea mwenza limefanyika katika ukumbi wa Diamond Jubilee jijini DSM ambapo mwenyekiti wa tume ya uchaguzi NEC jaji mstaafu wa mahakama ya Rufaa Damian Lubuva amesema kuwa katiba ya tanzania inampa tume kibali ya kutangaza mgombea ambaye amekuwa na kura nyingi kuliko wagombea wenzake.
  Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), Jaji mstaafu Damian Lubuva (kulia), akimkabidhi hati ya ushindi ya Urais, Rais Mteule wa Tanzania Dk.John Magufuli katika hafla iliyofanyika Ukumbi wa Diamond Jubilee Dar es Salaam leo. Kushoto ni Makamu wa Rais Mteule, Samia Hassan Suluhu.
  Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), Jaji mstaafu Damian Lubuva (kulia), akimkabidhi cheti cha Makamu wa Rais, Samia Hassan Suluhu katika hafla hiyo.
Rais Mteule wa Tanzania, Dk. John Magufuli (kulia), akiwapungia mkono wananchi wakati wa hafla hiyo ya kukabidhiwa cheti cha urais. Kutoka  kushoto ni mgombea urais kupitia Chama cha ACT-Wazalendo, Anna Mghwira na mgombea nafasi hiyo kupitia Chama cha ADC, Chief Lutalosa Yemba.
  Viongozi mbalimbali wakiwa kwenye hafla hiyo.
   Rais Mteule wa Tanzania, Dk.Magufuli akimuonesha Rais Jakaya Kikwete hati ya ushindi.
 Rais Mteule wa Tanzania, Dk.Makufuli akiwa katika picha ya pamoja na wagombea urais wenzake wa vyama vingine.
  Waziri Mkuu, Mizengo Pinda akimpongeza Mwenyekiti wa
Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), Jaji mstaafu Damian 
Lubuva kwa kusimamia vizuri uchaguzi mkuu wa 2015.
Rais Jakaya Kikwete na Rais Mteule Dk.John Pombe Magufuli wakiwa katika picha ya pamoja na wake zao kwenye hafla hiyo.

Rais mstaafu Ali Hassan Mwinyi (kushoto), akimpongeza 
Rais Mteule wa Tanzania Dk. John Magufuli baada ya kuchaguliwa kuwa rais.
Makada wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), wakishangilia wakati Rais Mteule wa Tanzania Dk.John Magufuli alipokuwa akitoka Ukumbi wa Diamond Jubilee kukabidhiwa cheti cha urais. 
picha kwa hisa mtandao wa www.habari za jamii.com-simu namba 0712-727062

Alhamisi, 29 Oktoba 2015

BAADA YA MATOKEO KAULI MBALIMBALI ZIMEANZA KUTOLEWA SASA SWALI LANGU NI JE?WATANZANIA WALIO JUU YA NINI KAMA SIO AMANI.

Mara bada ya matokeo kutangazo baadhi ya watumishi 
wmekuwa na kauli mbalimbali kwenye mitandao ya kijamii na
 hapa tunakiutana na mtumishi Peter LUkuta ambaye
 amesema haya
SASA NIMETAMBUA KUMBE WATUMISHI WENGI 
WANAONGOZWA NA MIZIMU
Najaribu kuvuta picha kama ndiyo mimi niliyetabiri kuwa 
fulani ndiye atakuwa raisi dooh leo sijui ningeuficha wapi uso
 wangu dah aibu gani hii
Najiuliza maswali sijui Jumapili wanaanza anzaje makanisani
 mwao maana Biblia Yangu inaniambia Mtu akitoa unabii na 
usipotimia atakuwa Nabii wa uongo tena apigwe mawe na 
mimi leo napiga nawe manabii wa uongo =KUMBUKUMBU
 LA TORATI 18:20-22./
2WAKORINTHO 11:13-15.7

2 PETRO 2:1-3./

Hapa sina shaka tena juu wa watumishi ambao Wapo mwilini kupita hata Shetani mwenyewe hawa wamezidi kumbe 
walitoa unabii sijui kwa akili zao wakamsingizia Mungu watu 
hawa kama hawaogopi kumsingizia Mungu bila shaka hata 
kuzini hawataogopa Duh napata shida juu ya sadaka
zinazotolewa kwenye madhabahu zao sijui zinaenda kwa
 mungugani hii aibu ni kubwa kuzidi hata Ile ya Escrow
 kumbe ndiyo sababu hata waumini wao kila ninapo kutana
 nao huwa nakuta roho zingine za tofauti nashukuru sana 
Mungu mimi sikutabiri pamoja na wengi kunifwata inbox
 kutoka nitoe unabii juu ya Rasi anaye lakini sikufanya hivyo 
maana ningekuwa nimetabiri kwa kutumwa na watu kama
 walivyofanya hao wengine na sio Mungu wa kweli
Acha nisiseme sana sije wakajitoa fb nikashindwa kuwaponya

Jumanne, 27 Oktoba 2015

MWENYEKITI WA TUME YA UCHAGUZI WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIAJAJI DAMIAN LUBUVA AKITANGAZA MATOKEO YA URAIS


Tunawaletea matokeo rasmi kwa nafasi ya Urais kwa mujibu wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi, NEC kama yanavyotangazwa.
 October 27, 2015 - Saa 8.40 Mchana

Jimbo  la  Fuoni-Mjini Magharibi

Magufuli (CCM): 956
Lowassa (CHADEMA):420

Jimbo  la  Kikwajuni-Mjini Magharibi

Magufuli (CCM):6,317
Lowassa (CHADEMA): 3669

 Jimbo  la  Mpanda Vijijini-Katavi

Magufuli (CCM):37,321
Lowassa (CHADEMA): 12,791

Jimbo  la  Mchinga-Lindi

Magufuli (CCM):13,948
Lowassa (CHADEMA):12,936

Jimbo  la  Mwela-Mjini Magharibi

Magufuli (CCM):6430
Lowassa (CHADEMA):5865

Jimbo  la Nkasi  Kaskazini-Rukwa

Magufuli (CCM):25,837
Lowassa (CHADEMA):19,891

Jimbo  la  Nkasi Kusini-Rukwa

Magufuli (CCM): 21,572
Lowassa (CHADEMA): 13,550


Jimbo  la  Nkenge-Kagera

Magufuli (CCM): 42,568
Lowassa (CHADEMA): 25,840

Jimbo  la  Amani-Kusini Magharibi

Magufuli (CCM):4,322
Lowassa (CHADEMA):3,157

Jimbo  la  Bumbwini

Magufuli (CCM):2503
Lowassa (CHADEMA): 2822

Jimbo  la  Nungwi- Mkoa wa Kaskazini Unguja

Magufuli (CCM):4135
Lowassa (CHADEMA): 4853

Jimbo  la Uzini

Magufuli (CCM):6537
Lowassa (CHADEMA):1864

Jimbo  la  Chwaka

Magufuli (CCM):6537
Lowassa (CHADEMA): 1864

Jimbo  la Mtama-Lindi

Magufuli (CCM):29,625
Lowassa (CHADEMA):20,841

Jimbo  la Tunguu-Kusini Unguja

Magufuli (CCM): 8,519
Lowassa (CHADEMA): 2,923

Jimbo  la Biharamuro-Kagera 

Magufuli (CCM):44,943
Lowassa (CHADEMA):28,576

Jimbo  la Arusha Mjini-Arusha 

Magufuli (CCM): 65,107
Lowassa (CHADEMA): 150,786

Jimbo  la Chake Chake

Magufuli (CCM):1253
Lowassa (CHADEMA):5209

Jimbo  la Kibaha Vijijini-Pwani 

Magufuli (CCM):20,805
Lowassa (CHADEMA):11,344

Jimbo  la Mwanakwereke

Magufuli (CCM): 4206
Lowassa (CHADEMA):4606

Jimbo  la Nachingwea-Lindi

Magufuli (CCM):46,485
Lowassa (CHADEMA):30,252

Jimbo  la Mafya- Pwani

Magufuli (CCM): 11,153
Lowassa (CHADEMA):9,363

Jimbo  la Mkuranga- Pwani

Magufuli (CCM):45,710
Lowassa (CHADEMA): 36,478

Jimbo  la Welezo

Magufuli (CCM):2615
Lowassa (CHADEMA):2582

Jimbo  la Magomeni-Kusini Magharibi

Magufuli (CCM): 5716
Lowassa (CHADEMA):3711
  == =================================== 
October 27, 2015 - Saa 3 Asubuhi  
  
Jimbo  la  Chalinze

Magufuli (CCM):52,212
Lowassa (CHADEMA):21380

Jimbo  la  Chonga

Magufuli (CCM):1740
Lowassa (CHADEMA):3800
  
Jimbo  la  Chumbuni

Magufuli (CCM): 5096
Lowassa (CHADEMA): 4450

Jimbo  la Ileje

Magufuli (CCM):26,368
Lowassa (CHADEMA): 15,651

Jimbo  la Kijini

Magufuli (CCM): 2703
Lowassa (CHADEMA): 3351

Jimbo  la Kilindi-Tanga

Magufuli (CCM): 33,942
Lowassa (CHADEMA):12,123
  
Jimbo  la Korogwe Mjini-Tanga

Magufuli (CCM): 17,168
Lowassa (CHADEMA): 9034

Jimbo  la Kohani-Mjini Magharibi

Magufuli (CCM):6,245
Lowassa (CHADEMA): 2689


Jimbo  la Lupembe-Njombe

Magufuli (CCM): 23,061
Lowassa (CHADEMA): 7,466

Jimbo  la Madaba-Ruvuma

Magufuli (CCM): 13,949
Lowassa (CHADEMA):4,735

Jimbo  la Masasi Mjini-Mtwara

Magufuli (CCM): 24,637
Lowassa (CHADEMA):16,778

Jimbo  la Mbeya Vijijini-Mbeya

Magufuli (CCM):62,662
Lowassa (CHADEMA):47,038

Jimbo  la Mkwajuni-Kaskazini Unguja

Magufuli (CCM): 4,686
Lowassa (CHADEMA): 3,314

Jimbo  la Momba- Mbeya

Magufuli (CCM): 28,978
Lowassa (CHADEMA):24,418

Jimbo  la Monduli-Arusha

Magufuli (CCM):11,355
Lowassa (CHADEMA): 49,675

Jimbo  la Mpendae- Mjini Magharibi

Magufuli (CCM):4,192
Lowassa (CHADEMA): 4,048

Jimbo  la Mwanga-Kilimanjaro

Magufuli (CCM): 25,738
Lowassa (CHADEMA):15,148

Jimbo  la Namtumbo-Ruvuma

Magufuli (CCM):44,061
Lowassa (CHADEMA): 23,039

Jimbo  la Newala Mjini-Mtwara

Magufuli (CCM): 21,269
Lowassa (CHADEMA):16,980

Jimbo  la Newala Vijijini-Mtwara

Magufuli (CCM): 29,799
Lowassa (CHADEMA): 13,958

Jimbo  la Siha-Kilimanjaro

Magufuli (CCM): 18,252
Lowassa (CHADEMA):22,572

Jimbo  la Solwa-Shinyanga

Magufuli (CCM): 66,096
Lowassa (CHADEMA): 23,510

Jimbo  la Tandahimba

Magufuli (CCM): 49,098
Lowassa (CHADEMA):46,288
  
Jimbo  la Tumbatu-Kaskazini Unguja

Magufuli (CCM): 5,720
Lowassa (CHADEMA):  3,967

Jimbo  la Igalula-Tabora

Magufuli (CCM): 28,747
Lowassa (CHADEMA): 8,393

Jimbo  la Ulanga-Morogoro

Magufuli (CCM):32,297
Lowassa (CHADEMA):20,489

Jimbo  la Wawi-Kusini Pemba

Magufuli (CCM): 1,748
Lowassa (CHADEMA): 5,216

Jimbo  la Ziwani-Kusini Pemba

Magufuli (CCM): 592
Lowassa (CHADEMA):6,067

Jimbo  la Ole-Kusini Pemba

Magufuli (CCM):681
Lowassa (CHADEMA):5,251
  
Jimbo  la .....-Kaskazini Unguja

Magufuli (CCM): 5,592
Lowassa (CHADEMA): 1,019

Jimbo  la Tabora Kaskazini-Tabora 

Magufuli (CCM): 38,050
Lowassa (CHADEMA): 12,410

Jimbo  la Ruangwa 

Magufuli (CCM): 34,516
Lowassa (CHADEMA): 26,827

Jimbo  la Malindi-Mjini Magharibi 

Magufuli (CCM): 2,581
Lowassa (CHADEMA): 5,662

Jimbo  la Jang'ombe-Mjini Magharibi 

Magufuli (CCM): 6,567
Lowassa (CHADEMA):2,839

Jimbo  la Mhambwe-Kigoma 

Magufuli (CCM): 37,746
Lowassa (CHADEMA): 22,804

=============================== 
Oktoba 26, 2015 - Saa 4 asubuhi:

Jimbo la Makunduchi:

Magufuli (CCM): 8,406
Lowassa (CHADEMA): 1,769

Jimbo la Paje:

Magufuli (CCM): 6,035
Lowassa (CHADEMA): 1,899

Jimbo la Lulindi:

Magufuli (CCM): 31,603
Lowassa (CHADEMA): 11,543

October 26, 2015 - Saa 11 Jioni
Jimbo la Mkoani:

Magufuli (CCM): 3341
Lowassa (CHADEMA): 7368

Jimbo la Ndanda:

Magufuli (CCM): 33699
Lowassa (CHADEMA): 19017

Jimbo la Kiwengwa:

Magufuli (CCM): 3317
Lowassa (CHADEMA): 1104

Jimbo la Nsimbo:

Magufuli (CCM): 31413
Lowassa (CHADEMA): 6042

Jimbo la Mtambile:

Magufuli (CCM): 902
Lowassa (CHADEMA): 5875

Jimbo la Donge:

Magufuli (CCM): 5592
Lowassa (CHADEMA): 1019

Jimbo la Kiwani:

Magufuli (CCM): 1661
Lowassa (CHADEMA): 4229

Jimbo la Chambani:

Magufuli (CCM): 818
Lowassa (CHADEMA): 5319

Jimbo la Kibaha Mjini:

Magufuli (CCM): 34604
Lowassa (CHADEMA): 25448

Jimbo la Bumbuli:
Magufuli (CCM): 35310
Lowassa (CHADEMA): 7928

October 26, 2015 - Saa 2 Usiku
Jimbo la Gando:

Magufuli (CCM): 881
Lowassa (CHADEMA): 5903

Jimbo la Kisarawe:

Magufuli (CCM): 24086
Lowassa (CHADEMA): 13093

Jimbo la Kojani:

Magufuli (CCM): 1561
Lowassa (CHADEMA): 9982

Jimbo la Mbinga Mjini:

Magufuli (CCM): 29295
Lowassa (CHADEMA): 11695

Jimbo la Mgogoni:

Magufuli (CCM): 710
Lowassa (CHADEMA): 6506

Jimbo la Mkinga:

Magufuli (CCM): 23798
Lowassa (CHADEMA): 15142

Jimbo la Moshi Mjini:

Magufuli (CCM): 28909
Lowassa (CHADEMA): 49379

Jimbo la Mtambwe:

Magufuli (CCM): 428
Lowassa (CHADEMA): 6937

Jimbo la Nanyamba:

Magufuli (CCM): 24904
Lowassa (CHADEMA): 16992

Jimbo la Peramiho:

Magufuli (CCM): 32505
Lowassa (CHADEMA): 11291

Jimbo la Wete:
Magufuli (CCM): 958
Lowassa (CHADEMA): 5119

Jimbo la Singida Mjini

Kura: 56,558 

Magufuli (CCM): 36,035 

Edward Lowassa (Chadema): 19,007

Jimbo la Lindi Mjini 
Kura: 38,992
Magufuli (CCM): 21,088
Edward Lowassa(Chadema): 17,607
 
Jimbo la Njombe Mjini 
Kura: 55,772
Magufuli (CCM): 33,626
Edward Lowassa(Chadema):20,368

Jumapili, 4 Oktoba 2015

MCHUNGAJI MTIKIA AFARIKI DUNIA KWENYE AJALI KATIKA KIJIJI CHA MSOLWA.

Mwanasiasa mkongwe na mwenyekiti wa chama cha Democratic Party DP mchungaji Christopher Mtikila amefariki dunia kwenye ajali ya gari  iliyotokea katika kijiji cha Msolwa Chalinze mkoani pwani
Akithibitisha kutokea kwa ajali hiyo kamanda wa polisi mkoa wa Pwani kamandaJaffar Mohamed amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo,ambapo amesema mchungaji Mtikila alikuwa akitokea mkoani Morogoro kwenda Dar es salaam akiwa na watu wengine watatu ambao wamejeruhiwa kwenye ajali hiyo.

Ameongeza kuwa chanzo cha ajali hakijafahamika inaendelea kuchunguzwa.

Ijumaa, 2 Oktoba 2015

KAULI TATA MAARUFU ZENYE KUKINZANA NA NENO LA MUNGU.

Hoja ya leo nimeona niwasilishe baadhi ya “kauli tata” ambazo ni maarufu sana kwa waumini wa madhehebu ya dini kwa kudhaniwa kwamba ni “maneno ya Mungu.”! Sababu ya kuamua kuzichambua ni kwa sababu, zimekubalika kama ni “Neno la Mungu wakati zinakinzana na Neno la Mungu”! Nia ni kuweka waziwazi uongo wa Ibilisi uliojificha kwenye kauli hizo tata ili aliyekuwa amedanganyika afunguliwe fahamu na kuwekwa huru kwa kuijua kweli. 
Kauli tata ya “Sisi
sote ni watoto wa Mungu”

Ni kweli kwamba kwa asili binadamu wote tunatokana na watu wawili ambao ni binadamu wa kwanza walioumbwa na Mungu. Na binadamu hawa waliishi miaka mingi isiyojulikana mpaka wakati walipoasi amri ya Mungu wakaanguka katika dhambi. Kuanzia wakati huo mpaka hivi leo, vizazi vilivyofuata viliathiriwa na dhambi na kujulikana kama watumwa wa Ibilisi kwa sababu hiyo.

Kwa sababu ya upendo wa Mungu, almtuma Mwana wake pekee Yesu Kristo ilia je kutukomboa katika utumwa wa Ibilisi. Tangu ujio wa Kristo duniani, ndipo ukaanzishwa uzao mpya wa kiroho ambayo unatoa fursa kwa kila binadamu mwenyedhambi kuimpokea Yesu na kisha kupata uwezo wa kufanyika mtoto wa Mungu. Kwa hiyo, tangu Yesu alipokufa na kufufuka katika wafu, tuna makundi ya aina mbili ya binadamu hapa duniani. Kundi la “watoto wa Mungu”, na kundi la “watoto wa Ibilisi”.

“Katika hili watoto wa Mungu ni dhahiri, na watoto wa Ibilisi nao. Mtu ye yote asiyetenda haki hatokani na Mungu, wala yeye asiyempenda ndugu yake.” (1 YOH. 3:10)

Kwa hiyo si kweli kwamba, kila binadamu aliye hai hapa duniani ni “mtoto wa Mungu.”! Haijalishi aina ya tofauti za madhehebu ya dini na wasio na dini kabisa. Wote ni “watu wa Mungu” kwa maana tu viumbe wake Mungu kwa asili. Lakini sio wote ni watoto wa Mungu ati kwa sababu ni binadamu. Kuwa mtoto wa Mungu ni uchaguzi binafsi ambao unafanywa na mtu mwenyewe.

“Wote waliompokea, aliwapa uwezo wa kufanyika “watoto wa Mungu”, ndio waliaminio jina lake.” (YH.1:12)

Jambo jema na kutia hamasa ni kwamba walio “watoto wa Mungu” sio kwamba tunajiaminisha tu kwa akili zetu wenyewe. Yesu mwenyewe ametusaidia kwa kumtuma Roho Mtakatifu ambaye amekuja kufanya makao ndani yetu. Na tunapompokea Roho Mtakatifu akiisha kujaa kwa wingi ndani yetu, yeye ndiye hufanya kazi ya kututhibitishia na kutushuhudia kwamba sisi ni watoto wa Mungu:

“Kwa kuwa hamkupokea tena roho wa utumwa iletayo hofu; bali mlipokea roho ya kufanywa wana, ambayo kwa hiyo twalia, Aba, yaani, Baba.  Roho mwenyewe hushuhudia pamoja na roho zetu, ya kuwa sisi tu watoto wa Mungu;” (RUM. 8:15-16)

Je wewe mwenzagu una hakika kwamba ni “mtoto wa Mungu”? Unaamini hivyo kwa sababu ya kauli ya mazoea kwamba “binadamu wote ni watoto wa Mungu”; au ni uchaguzi wako binafsi ulioufanya wa kumpokea Yesu Kristo ili akupe uwezo wake wa kufanyika mtoto wa Mungu? 
Kauli tata ya “Sisi sote
tunamwabudu Mungu mmoja”

Kauli tata nyingine inayokizana na Neno la Mungu lakini imeshika akili za watu wengine ni dhana ya kudai kwamba “Sisi sote tunamwabudu Mungu mmoja”! Ati pamoja na tofuati zetu za kimadhehebu na mitindo mbli mbli ya kuabudu; bado tunamwamubu Mungu mmoja tu iwe kwa kujua au kutokujua!

Tatizo kubwa linaanzia hapo hapo kwenye tofuati ya itikadi na mitindo ya kuabudu. Angelikuwa ni Mungu mmoja yule yule kwanini aabudiwe kwa njia na mitindo tofauti?  Wachiliana mbali tofauti za kiitikadi na kimitindo ya kuwabudu, mbona tunashawishiana na kuvutiana kila upande unafanya juhudi za kupata wafuasi wa itikadi nyingine wajiunge na itikadi yao? Majibu ya maswali yataonesha dhahiri kwamba hata kama yupo Mungu mmoja anayestahili kuabudiwa na sisi sote; lakini sio itikadi zinamwabudu Mungu mmoja.

Baada ya kusema yaliyotangulia, nije kwenye maandiko yasemavyo kwa habari ya Mungu anayestahili kuabudiwa na wote na jinsi ya kumwabudu. Kitabu cha Matendo ya Mitume kinatupa ukweli kama ifuatavyo:

“….jueni ninyi nyote na watu wote wa Israeli ya kuwa kwa jina la Yesu Kristo wa Nazareti, ambaye ninyi mlimsulibisha, na Mungu akamfufua katika wafu, kwa jina hilo mtu huyu anasimama ali mzima mbele yenu.  Yeye ndiye jiwe lile lililodharauliwa na ninyi waashi, nalo limewekwa kuwa jiwe kuu la pembeni.  Wala hakuna wokovu katika mwingine awaye yote, kwa maana hapana jina jingine chini ya mbingu walilopewa wanadamu litupasalo sisi kuokolewa kwalo.” (MDO 4:10-12)

Unaona? Kisa cha Mungu kumtuma Mwanawe licha ya kutukomboa toka utumwa wa Ibilisi, lakini pia kutuwezesha kumwabudu Mungu Baba kwa njia ya Yesu Kristo ambaye ni mlango wa kuingilia patakatifu pa patakatifu pa Mbinguni.

Kwa mantiki hii, hakuna mtu mwingine awaye yote chini ya mbingu ambaye inatupasa kuokolewa isipokuwa Yesu Kristo mwenyewe. Msingi wa maandiko haya ni kukanusha uvumi na itikadi za dini nyingine zote zisizomtambua Yesu Kristo kuwa ndiye peke ambaye anatupeleka kwa Mungu wa kweli kwa sababu Mungu huyo ni Baba yake halisi. Kwa hiyo, dhana kwamba sisi sote tunamwabudu Mungu mmoja si kweli. Kila dini ina Mungu wake ambaye wafuasi wake wanamwabudu. Hata kama majina yanaweza kufanana lakini, kigezo cha kumwabudu Mungu wa kweli ni kupitia Yesu Kristo peke yake.
Kauli tata kwamba “sisi sote
twaenda sehemu moja baada ya kufa”

Kauli tata ambayo imeshika hisia na akili za wengi kwamba ni Neno la Mungu, ni dhana hii inayodai kwamba, “sisi sote tukifa tunaenda kumoja, yaani kukaa na Mungu milele.” Ati “SISI SOTE KAMA BINADAMU TUNAELEKEA SEHEMU MOJA BAADA YA KUFA.” Dhana hii inadai kwamba bila kujali maisha ya mtu anayoishi hapa duniani, yawe machafu au masafi kulingana na dhamiri yake kwa itikadi ya dini yake akifa lazima anaenda sehemu moja ile ile ambayo binadamu wanapokufa wanakwenda kuishi na Mungu milele.

Tena wengine wanachanganya zege zaidi, kwamba tofauti za madhehebu ya dini ni sawa na njia nyingi tofauti lakini zinaishia na kuunganika kwa Mungu mmoja baada ya kufa. Ni kweli kwamba, kila anayekufanya atakutana na Mungu siku ya kiyama. Lakini inategemea unakutana na Mungu kwa kupitia NJIA ipi. ZIko njia mbili kuu hapa duniani. Kuna njia iendayo upotevuni, na kuna njia iendayo uzimani aliko Mungu baba.

Kana kwamba hii haitoshi, siku hizi kuna kauli tata za nyongeza zinazotoa faraja kwa wafiwa zinazosema; “Mungu amempenda zaidi.”! Ninatambua sana umuhimu, ya kwamba, wakati wa msiba wafiwa wanahitaji faraja za karibu ili kutuliza huzuni na maumivu yatokanayo na kuondokewa na mpendwa wao. Pamoja na juhudi na huruma za kuwafariji wafiwa, haifai kabisa kutoa kauli ambazo sio Neno la Mungu kwa sababu kwanza zinazidi kushindilia uongo wa kiimani na wengi wanazidi kupotea kwa uongo huo.

Jamani kama ingelikuwa ni rahisi kwamba kila mtu anayekufa anakwenda kukaa kwa Mungu na kupumzika moja kwa moja, pasingelikuwepo haja ya kuwahubiriwa watu Injili ya wokovu wa Yesu Kristo ili watubu na kuzaliwa upya kiroho! (MK.16:16)

Yesu alisema kwamba, “Ingieni kwa kupitia mlango ulio mwembamba; maana mlango ni mpana, na njia ni pana iendnayo upotevuni, nao ni wengi waingiao kwa mlango huo.” (MT.7:13-14)

Mfani mwingine unaoshuhudia kwamba sio kweli kwamba watu wote wanapokufa wanaenda sehemu moja, ni mfano vifo vya “Tajiri Lazaro na maskini” kama ilivyosimuliwa katika Injili ya Luka. (Lk.16:19-26) Humo tunasoma Tajiri alipokufa alikwenda mahali pa mateso na maskini alipokuwa alikwenda kifuani pa Ibrahimu mahali pa mapumziko. Hizi ni sehemu mbili tofauti na kila anayekufa huenda upande wake kulingana na aina ya njia aliyoichagua tangu alipokuwa angali hai.
Somo ambalo Askofu Gamanywa amefundisha,
wasiliana nasi kwa 0682672828.