Somo la Roho mtakatifu ambalo limefundishwa na mtumishi wa Mungu mchungaji Peter Miagie kutoka Lengijave Arusha katika kanisa la T.A.G Sayuni Msakuzi linaloongozwa na mchungaji Editor Sylvester Kajuna jijini Dar es salaam.
Katika somo hilo ameelezea juu ya Roho mtakatifu kuwa ni nafsi ya tatu
ya Mungu na ni muhimu sana katika maisha ya kila mkristo maana anafanya kazi
mbalimbali ndani ya maisha ya mwamini na ndani ya kanisa kwa ujumla.
MCHUNGAJI PETER MIAGIE AKIWAOMBEA WAUMINI AMBAO WAMEHUDHURIA KATIKA SEMINA TAG MSAKUZI.
Kuna kazi mbalimbali ambazo Roho
Mtakatifu hutenda kwa kanisa na kwa mwamini mmoja mmoja,pia ana majina ambayo
mara nyingi hutumika.
1.Roho wa Kristo ,umoja na
uhusiano wa utatu mtakatifu.
2.Roho wa hukumu na kuchoma
Roho wa haki,sheria na taratibu
ambapo huondoa dhambi maana kwa hali ya kawaida hakuna mwanadamu ambaye
anamfahamu mwenzake ila Mungu pekee anafahamu na matendo ya kila mwanadamu
chini ya jua.
3.Roho wa neema na maombezi.
Hana mipaka na hawezi kuwekewa
maana yeye yupo popote,na ndiyo maana hata kama mtu yupo mbali anweza kuombewa
na kupokea uponyaji.
4.Roho wa hekima na ufunuo
Yeye huamua kwa haki na kila
mwamini ambaye yupo tayari kumtegemea humsaidia kuamua maamuzi mengi kwa
hekima.mfano Mfalme Suleimani aliweza kuamua kesi ambayo ilikuwa ngumu sana kwa
kutumia hekima ambayo aliomba kwa Mungu kabla.
5. Roho wa baba yenu.
kuna uhusiano wa karibu sana
ndiyo maana mara nyingi wakati wa maombi na maombezi huytajwa Mungu wa Ibrahimu
Isaka na Yakobo.
6.Roho wa kweli.
Ni nafsi ya tatu ya Mungu
anafahamu yote katika maisha ya kila siku ya mwamini.
7Ni Roho mtakatifu
Ni tabia yake utakatifu hivyo
imetupasa waumini kuwa watakatifu katika maisha ya kila siku
Zaburi 143:10.
8.Roho wa Uzima
Ni kazi yake ROho mtakatifu
kuwaombea watakatifu kutoka katika sheria ya dhambi
kolosai 1:13
warumi8:2
Maombi na maombezi yakiendelea baada ya neno ,waumini wengi walifika mbele kuombewa nguvu za Roho Mtakatifu ndani ya kanisa la TAG Sayuni Msakuzi
Waumini ambao walihudhuria semina wakiwa katika hali ya kuabudiu huku maombi yakiendelea.
Mchungaji kiongozi wa kanisa la TAG sayuni akiwaombea waumini katika semina ambayo imeendeshwa na mchungaji Peter Miagie kutoka kanisa la TAG Lengijave Arusha.
Maombi na maombezi yakiendelea baada ya neno ,waumini wengi walifika mbele kuombewa nguvu za Roho Mtakatifu ndani ya kanisa la TAG Sayuni Msakuzi
Waumini ambao walihudhuria semina wakiwa katika hali ya kuabudiu huku maombi yakiendelea.
Mchungaji kiongozi wa kanisa la TAG sayuni akiwaombea waumini katika semina ambayo imeendeshwa na mchungaji Peter Miagie kutoka kanisa la TAG Lengijave Arusha.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni