Yesu alitoa mfano mmoja akasema Mtu
mmoja alipanda mbegu njema shambani mwake lakini watu walipolala akaja adui
yake akapanda magumu MATHAYO 13:24-28.
Mwana wa Mungu kuna mambo mengi ya kujifunza hapa lakini nataka leo
tuangalie moja tu la nguvu ya macho maandiko Yesu alisema pia kuwa macho ndiyo
taa ya Mwili sawa kabisa ni kweli macho ndiyo taa ya Mwili Neno linasema kwamba
Mtu aliyepanda mbegu njema shambani mwake sasa hili neno mtu linamaanisha ni
mmoja lakini alikuwa na wafanyakazi wengi ambao walimlimia shamba lake na
kupanda mbegu njema na hao watu ndiyo walikuwa walinzi wa lile shamba. Sasa
basi pamoja na kwamba haijawekwa wazi kuwa walikuwa wangapi lakini lakini
kutokana na sentensi inayotumika kuelezea tukio hilo inaonyesha wazi kwamba
walikuwa si chini ya watu kumi ndiyo maana ikaandikwa WATU WALIPOLALA mimi
naamini Kama wangepungua kumi ingekuwa rahisi kuandikwa watu watatu au watu
watano au watu tisa ingekuwa rahisi kuandikwa watu kumi. Lakini siyo rahisi
kuandikwa watu kumi na tano no hiyo ingekuwa shughuli ya ziada mimi naamini
ilikuwa ni zaidi ya kumi na kuendelea. Pamoja na wingi wao na umahiri wao wa
kuchapa kazi ya bosi wao lakini bado hawakujua nguvu zao usalama wao kuwa upo
katika macho yao akili zao ziliwadanganya kuwa usalama wa shamba lao upo kwenye
uwepo wao wa wao kutokaa mbali na eneo lile waliamini kuwa wakiwa eneo lile
hakuna kibaya kinachoweza kutokea waliamini uwepo wao utamtisha adui asiweze
kusogea karibu na eneo lile. Lakini kwa bahati mbaya adui yao Alikuwa na akili
sana alikuwa anajua kuwa nguvu zao wao Kama walinzi haipo kwenye silaha wala
nguvu walizonazo bali nguvu zao zimo katika macho yao, Unajua Mwana wa Mungu ni
kwamba hawa watu walikuwa na ajira mbili mchana kulima na usiku kulinda hivyo ni
wazi kwamba walikuwa na mishahara miwili yani mshahara wa kulima na mshahara wa
kulinda. Ajira yao hii ni sawa na ajira ya kanisa kulima ni kutumika kwa bidii
katika kuwaleta watu kwa Yesu na kulinda ni kuwa macho wakati wote katika
kuwaleta watu wachanga kiroho kusudi sije wakavamiwa na mafundisho ya uongo na
kutolewa Nje ya njia sahihi na ya kweli hivyo kila mtumishi anajira ya kuwavuta
watu kwa Yesu pamoja na kuhakikisha anawalinda kwa maombi na mafundisho ya
kuwajenga kusudi wasirudi nyuma Kama mimi ninavyofanya kwenye Group zangu zote
za Whtsapp ndiyo maana nikawakataza watu kula chakula cha kusheherekea sikukuu
ya Idd mubarck kwasababu ni ibada ya miungu ni sikukuu ya miungu na kuna
madhara makubwa kwa mkristo aliyeokoka kula chakula kilichotolewa sadaka kwa
miungu =HESABU 25:1-4 Walafi na vipofu wa kiroho wanatumia maandiko vibaya
kwaajili ya kuhalalisha kula chakula cha miungu lakini nikutokana na upofu wa
kiroho pia nikutokana na ulafi tu uleule uliyomponza Esau akauza haki yake ya
mzaliwa wa kwanza kwaajili ya chakula kimoja kitu ambacho Mungu anakiita ni
uasherati =WAEBRANIA 12:16. Hii inamaanisha kwamba kula chakula kinachokuvunjia
uhusiano wako na Mungu ni hakuna tofauti na vijana wanaochukua makahaba na
kwendanao Guest kufanya Uasherati. Najua kuna wengine nimewakwaza lakini
jitahidini tu kunipenda hata hata kulazimisha kusudi roho zenu ziponywe na
mafundisho yangu ya matengenezo. Sasa tunaendelea ni kwamba wale walinzi
walikuwa wengi lakini hakujua anachokiogopa adui yao hivyo walipomwona adui anakatiza
walinyanyua silaha zao kusudi aogope lakini adui yule macho yake hatakuwa
yanatazamia zile silaha no bali macho ya adui yalikuwa yanatazama macho yao tu
adui aliogopa macho yao tu lakini walinzi hawa hawakujua ni sawa na Wakristo
wengi wasivyojua kuwa Shetani haogopi silaha zao za jina la Yesu tu no bali
Shetani anaogopa macho yao maana nguvu ya silaha ipo kwenye macho ndiyo maana
wameshindwa vita nyingi pamoja na kulitaja jina la Yesu Sikiliza mwana wa Mungu
Wote waliyoshindwa si kwamba hawakuwa na silaha ya Jina la Yesu no walikuwanayo
lakini walifumba macho NGUVU YA MACHO Yesu alisema Watu walipolala angalia
vizuri hili neno WATU maana yake ni wengi na hawa wengi wote walilala Usingizi
maana yake walifumba na macho maana huwezi kulala bila kufumba macho. ok watu
walipolala akaja adui. Angalia tena hii sentensi inasema AKAJA ADUI siyo WAKAJA
MAADUI no bali ni AKAJA ADUI maana yake alikuwa mmoja tu yani adui amekuja
mmoja tu lakini waliyolala walikuwa weengi wengi na akawashinda kwa kufanikiwa
kupanda magugu katikati ya shamba kisha akaondoka akaendazake. Wao walipoamka
asubuhi hawakujua kuwa adui alikuja usiku na kuwapandia magugu sasa wao
waliendelea na kuwekea mbolea pamoja na kumwagilia maji ili mazao yakue lakini
kipindi wanamwagilia mazao hayo hawakujua kuwa wanamwagilia na magugu hivyo ni
sawa na lile somo alilofundisha Mtumishi Vailethy Peter akasema Magugu
anayapanda Shetani lakini Mkuuzaji ayeyakuuza ni mwenye shamba yani magugu
anakupandia shetani lakini kukuuza unayakuuza mwenyewe. Ni kweli Shetani huwa
anapanda tu mbegu ya magugu ya mafarakano kwenye ndoa lakini wakuuzaji wa hiyo
mbegu ni wanandoa wenyewe kwa kuendeleza mafarakano vinyongo kuchukiana hiyo
yote hutokana na kukosa macho ya kuona kuwa adui hapa siyo mke w siyo Mume
wangu bali adui yetu hapa ni Shetani. Watu wengi wanashindwa kwasababu
hawamwoni Shetani wao wanaonana wenyewe wenyewe ndiyo maadui na Siku zote
haiwezekani kushinda vita kabla ya kumjua adui na kumwona mbinu zake. Silaha
haisadii mahali ambapo macho yamefumba silaha kupita macho kwasababu macho
ndiyo yanamwonyesha mlinzi mahali sahihi pakupiga huwezi kupigana vita huku
umefumba macho utauawa hata Nchi zote haziajiri vipofu jeshini kwasababu kipofu
haoni pakupiga ndivyo ilivyo watu wa Mungu leo hawajui pakupiga kwasabu
wamefumba macho wamelala na hata wakijaribu kupigana wanapigia wao kwa wao
shetani wanamwacha pembeni kwa sababu hawaoni kibaya zaidi hata nyakati baadhi
ya Watumishi nao hawaoni pamoja na kujipachika majina Makubwa kwa ajili ya
kuwateka watu kisaikoloji lakini hawaoni wamebakia kuonyesha shoo tu Kama
kaburini flani hivi kakufurahisha macho na masikio ya watu. Kwasababu nao
wamelala hawana. Adui anajua nguvu za Macho na ndiyo maana haji kwa mtu
aliyemacho mtu ambaye yuko macho kwenye utakatifu kwenye utoaji kwenye maombi
kwenye kufunga kwenye kufanya kazi ya Mungu kwa mali zao watu hawa ambao wako
macho Shetani hawasogelei watu ambao Mungu akisema wanajua huyu ni Mungu
wanatii na Shetani akija kwa njia yoyote wanajua huyu ni Shetani hapa
hatumkubalii kupita kirahisi tumzuie, wanapatana na kumzuia Shetani wanashinda
lakini watu ambao wamelala shetani atawagalagaza atawapepeta Kama ngano
atazivunja ndoa zao atavunja undugu wao atavuruga huduma zao atawaweza kwa
kishindo kwasababu wamelala hawataki Kuamka hawataki kusameheana mke hataki
kumnyenyekea mumewe hataki kumtii mume hataki kumpenda mkewe hampi huduma hata
mke akichukua pesa kununulia malapa tu lazima iwe kesi mke akienda kujinunulia
vitu vidogo vidogo tu anasimangwa anaambiwa anatumia pesa vibaya yani mke hana
uhuru na mali za mumewe mtu wajinsi hii nikipofu haoni na kamwe hawezi
kuvishinda vita vya kiroho kadhalika mke mwenye kiburi hawezi kushinda vita
inayomkabili. Pia na Mtu mwingine yes ambaye amelala kamwe hawezi kushinda vita
walokole wengi wamevamiwa na roho za ajabu ajabu kutoka Kuzimu kutokana na
kutokuwa tayari kutii ili kuwa na macho. Usisahau kwamba adui mmoja tu anaweza
kuwaangamiza Wote iwe kanisa au familia familia hata taifa indepo tu watalala
Usingizi. Yapo mengi ya kufahamu juu ya hili lakini kwa leo naishia hapa Kwa
Ushauri Na Maswali Nitumie Masage Kwenye Whtsapp yangu 0767 503054
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni