YESU NI JIBU

Jumanne, 28 Julai 2015

UJUMBE MAALUM KWA WATANZANIA WOTE BILA KUJALI DINI,DHEHEMU WALA KABILA NA RANGI WATUMISHI WANENA KATIKA STUDIO ZA WAPO REDIO.

ASKOFU SYLVESTER GAMANYWA,
Nafasi ya kanisa la Tanzania katika changamoto zinazolikabili taifa ambazo ni ya changamoto za kiuchumi,kijaami na kisiasa.

askofu mkuu wa WAPO Mission Internatinal Slyvester Gamanywa akizungumza katika studio za TIT Dar es salaam.
Kanisa la Tanzania nafasi yake ni ipi na mchango wake ni ulipi hizo ndiyo agenda na kuanzia tarehe 31 Ijumaa  na 1 jumamosi ukumbi wa mwalimu julias kambarere
Aidha askofu Gamanywa alisema kuwa maaskofu,wachungaji,mitume,manabii wanaalikwa kuhudhuria na wacha Mungu ambao wana taaluma mbalimbali ambao zitasaidia kanisa kusimama katika nafasi yake.
Aliongeza kuwa Roho mtakatifu anazungumza na watumishi wa Mungu katika nafasi mbalimbali na katika jumbe mbalimbali ambazo yeye anataka taifa lisikie.
Na Katika mkutano huo watumishi watapitia jumbe mbalimbali ambazo zilitolewa na watumishi mbalimbali na kinachotakiwa ni kutubu tu na kugeuka na kufanya kile ambacho Mungu yeye anataka maana
yeye sio wa malumbano wala sio maandamano.
Hata hivyo alisema kuwa Kadi kwa wale ambao watahudhuria katika kongamano hilo zimekabidhiwa kwa viongozi wa kanisa na madhehebu mbalimbali na pia mtu .
Kiashirio cha kutoweka kwa amani katika taifa la Tanzania vimeanza kuonekana na kiukweli hakuna amani kuna utulivu ndani ya nchi.
Hata hivyo askofu Gamanywa hakuchelea kuelezea nini kinachosababisha haya yote ambapo alisema kuna watu wanaonufaika na mazingira ya vita na fujo zinazotokea na wao wanaochangia na wapo ndani na nje ya nchi.

 Alisema pia vita vya kiraia na jeshi usiombe, nchii kuingia mikononi mwa jeshi sio jambo la kuliombea,na haya nasema sio kwa lengo la kuwatisha wananchi hapana nafahamu maana wakati wa vita vya Uganda na Tanzania limepigana nafahamu sana tu madhara ya vita. 
ASKOFU DEO LUBAMA AKIWA KATIKA STUDIO ZA TIT MIKOCHENI JIJINI DAR ES SALAAM.
Katika miaka ya hivi karibuni Mungu amekuwa akizungumza mambo mengi kuhusu kanisa na Taifa la Tanzania.
kuanzia Mwaka 2002 Mungu alizungumza na watumishi kuwa maaskofu,wachungaji na watumishi wake wengine,wakae pamoja ili kuomba  na kutafakari Neno lake katika umoja
Mwaka 2008 Julai Mungu alisema yupo karibu kuingia Tanzania.
Mwaka 2014 katika mkutano wa madhehebu mbalimbali uliofanyika DAR es salaam,Mungu alisema kuwa  endapo kanisa halitaingia katika  toba na maombi,amani iliyopo itatoweka na hali ya nchi itakuwa mbaya kuliko ile ya Somalia.
Mwaka 2015 kupitia watumishi mbalimbali wa ndani na nje ya nchi,Mungu anasema tena kanisa linahitajika kuinuka na kuchukua nafasi yake ya katika nchi.
kwa mawasiliano

0754507230 na 0784847070
MZEE GOFREY LEMA AKIELEZEA KWA MAKINI JUU YA KIONGOZI BORA NDANI YA STUDIO ZA TIT huku askofu Gamanywa akimsikiliza kwa makini na Mhe Kaduma kulia.
Kiongozi mzuri hasubiri mambo yaharibike ila anafanya kila jitihada kutafuta ufumbuzi mapema.
luka 19:41-43
Maneno ya manabii yanatimia maaana Mungu amekuwa akisema juu ya Taifa la Tanzania kwa muda mrefu sana,amekuwa kama anatubembeleza watanzania maana yeye anajua kilichopo mbele wakati sisi tunajua ya leo tu.
Mungu anataka kuingia Tanzania kufanya kile anachotaka kufanya na hawezi kufanya jambo bila kuwashirikisha watumishi wake.
Amosi 3:7

Wataalamu mbalimbali wanakaribishwa na wale wanasiasa wanaowania nafasi mbalimbali katika taifa hili ili wapate cha kuwaambia wapiga kura wao
Aidha Mzee Lema alisema kuwa mkutano huo hakuna kiingilio  na litanza saa tano kami asubuhi hadi jioni.
Hata hivyo alisema kuwa vyakula vitakuwepo ambavyo vitauzwa kwa bei ndogo sana kutakuwepo na kadi ya kutambulisha.
Hakukawia kuwataja wanenaji katika mkutano huo kuwa ni
Askofu Bernard Nwaka kutoka Tanzania na Emanuel Kure kutoka Marekani.

Hta hivyo alisema ujumbe juu ya Tanzania kwa itampata kiongozi anayetokana na Mungu 14 Agosti  2008 ulirudiwa na  Moris Cerullo 2008 Taifa hili litapata  Rais ambaye ni mteule kutoka kwa Mungu.
 IBRAHIMU KADUMA NDANI YA STUDIO ZA TIT.
Kauli ya mh. Ibrahim Kaduma ambaye ni mwenyekiti wa bodi ya wakurugenzi wa Kingdom Leadership Network Tanzania alisema kuwa julai 2008 unabii ulitolewa juu ya Tanzania sasa  ni vyema wateule waombe kwa bidii maana hatujui huyo mteule ni nani na unabii unapomkuja haubadiliki na anayetokana na Mungu atatenda kwa haki.
Askofu Deo Lubama
Ndugu msomaji wetu huu ni ujumbe juu ya Tanzania na sasa unaenda kutimia wewe unachukua hatua gani na unaweza kujiuliza kuwa walengwa katika mkutano huo ni viongozi wa makanisa hasa maskofu,wachungaji na watumishi wengine,wanasiasa,wafanyabiaashara na viongozi mbalimbali wa umma na sekta binafsi. 

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni