Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Mhe.
Amos Makalla ameielekeza Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba TMDA kupatia ufumbuzi
tatizo la Wizi wa Dawa za Serikali na kutoa onyo kwa Maduka yanayonunua dawa za
Wizi.
Aidha aliwaagiza Wakaguzi wa Dawa kuzingatia Weledi na maadili ya kazi kwa kuhakikisha wanatanguliza uzalendo Kutokana na unyeji wa kazi hiyo ambayo inabeba dhamana ya Maisha na uhai wa Wananchi.
Hata hivyo RC Makalla ameielekeza Mamlaka hiyo Kudhibiti tatizo la Vishoka Wanaofanya ziara za ukaguzi kwenye Maduka huku akitaka kuwepo kwa usimamizi madhubuti wa Maduka ya dawa.
Pamoja na hayo RC Makalla ameitaka
Mamlaka hiyo kuweka utaratibu wa kufanya ziara za kustukiza kwenye Maduka ya
dawa ili kubaini wababaishaji na kutaka uwepo wa watoa huduma Wenye sifa na
Vigezo.