YESU NI JIBU

Jumatano, 2 Agosti 2017

USHAURI KWA WAZAZI JUU YA WATOTO WAO WANAOSOMA SHULE ZA KULALA.

Wazazi wanatakiwa kuwa makini na watoto wao hasa wale ambao wanapenda kuwapeleka watoto shule za kulala (boarding)iwe ya wasichana wenyewe  ama ya wavulana wenyewe,ni vizuri kuwa makini na kuhakikisha kuwa kila unapompeleka shuleni akirudi hakikisha kuwa unamsikiliza na kukaa naye ili ufahamu kuwa amekutana na changamoto gani akiwa huko shuleni.
Wazazi wenzangu nimekaa na kutafakari sana juu ya watoto wanaopelekwa shule za kulala watoto maana hali ni mbaya katika shule hizo maarufu kama (boarding).

WAWAUMINI WASHAURIWA KUTUMIA FURSA ZILIZOPO ILI KUJIKWAMUA NA UMASKINI:

ASKOFU wa kanda ya kati kanisa la Pentecostal Holliness Association Mission (PHAM) Julias Bundala amewataka waumini wa  madhehebu ya dini kuhakikisha kuwa wanatumia fursa zinazojitokeza kwa wakati huu ambapo serikali imeamua kuhamishia makao yake makuu mkoani Dodoma.

Kiongozi huyo wa kanisa hilo ametoa ushauri huo wakati alipokuwa akizungumza na watumishi mbalimbali wakiwemo wachungaji,wainjilisti,wazee wa kanisa na mashemasi kwenye semina ya siku nne iliyoandaliwa na kanda ya kati iliyofanyika kijiji cha Chiwe wilaya ya Kongwa mkoani Dodoma.