Mwandishi
wa habari mkongwe Kyaloeichi Oko Kessy (62) amefariki usiku wa kuamkia jana
nyumbani kwake Pugu jijini Dar es Salaam.
Mpwa
wa marehemu Tumaini Msengi ,amesema leo kuwa marehemu alikuwa anasumbuliwa na
ugonjwa wa kisukari na shinikizo la damu kwa muda mrefu na amekuwa akitibiwa
katika hospitali mbalimbali za jijini Dar es Salaam hadi jana ambapo mauti
yalimkuta.
Kabla
hajaanza kuugua Kessy alikuwa mwandishi wa kujitegemea akiandika zaidi
uchambuzi na makala katika vyombo mbalimbali vya habari nchini yakiwemo
magazeti ya Motomoto,Shaba,Rai, na mengineyo mengi pia alikuwa ni mtunzi wa
vitabu vya aina mbalimbali.
Hata
hivyo Msengi ameeleza kuwa marehemu ameacha watoto wawili na mipango
ya mazishi inafanyika nyumbani kwa mdogo wake Chanika nje kidogo ya jiji na
mazishi yanatarajiwa kufanyika wiki ijayo ambapo Marehemu ni mzaliwa wa kijiji
cha Rosho Kilema mkoani Kilimanjaro.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni