YESU NI JIBU

Ijumaa, 8 Mei 2015

MAMLAKA YA HALI YA HEWA TANZANIA TAM WAMETOA UTABIRI WA HALI YA HEWA YA MVUA KUENDELEA KUNYESHA HADI MWISHONI MWA MEI MWAKA HUU.



Mamalaka ya hali hewa nchini (TAM) imewatahadharisha wananchi kuchukua hatua za haraka kuondoka katika maeneo ya mabondeni kufuatia mvua zinazoendelea kunyesha.
 Dr Agnes Kijazi
Kauli hiyo imetolewa na mkurugenzi mamlaka hiyo Dr Agnes Kijazi amesema mvua hizo zinazoendelea kunyesha mfululizo licha ya kuwa zitapungua kidogo na kuwasihi wananchi kuendelea kufuatilia kwa makini taarifa zinazotolewa na mamlaka hiyo kila siku ili waweze kupata taadhari ili kuepukana na maafa na kuhamia maeneo ambayo ni salama.
Aidha mvua hizo zimesababisha madhara makubwa ambapo mpaka sasa Watu nane wamepoteza maisha na mamia kukosa makazi kutokana na mvua kubwa zinazoendelea kunyesha katika jiji la Dar es Salaam .












Hata hivyo  mvua hizo zimekuwa zikinyesha mfulullizo na kusababisha uharibifu mkubwa wa miundo mbinu pamoja baadhi na kusababisha  foleni kubwa ya magari jijini dare s salaam.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni