Mamia na maelfu ya watu wanaendelea kufunguliwa kutoka
katika vifungo mbalimbali katika ibada 100 za operation vunja mafungo
zinazoendelea kufanyika katika kanisa la Eagt City Centre jijini DSM.
Akizungumza na blog hii ofisini kwake Temeke jijini DSM mchungaji
florian josephat katunzi ameeleza kuwa lengo kuu la ibada hizo ni kuwafungua
watu kutoka katika mafungo ya giza ,kuwaamisha na kuwaingiza katika ufalme wa
MUNGU.
Aidha mch.katunzi ameeleza kuwa katika ibada hizo
zinazoendelea kila kila siku za jumatano hadi jumapili zinasimamia maandiko ya
biblia kutoka katika kitabu cha wakolosai 1;13 na 1yohana 3;8 ,na kusisitiza
kuwa watu wahudhurie katika ibada hizo waone kuwa mungu yupo, anaponya
anafungua na haina haja ya kwenda kwa waganga wa kienyeji.
Hata hivyo ameongeza kuwa katika ibada hizo zilizo anza mwezi
January zinatarajiwa kumalizika mwishoni mwa mwezi may ambapo katika hitimisho la ibada hizo
kutakuwa na maombi maalum ya familia na kila familia itafunguliwa na kuinuliwa
kimadhabahu katika ufalme wa mungu.
Baadhi ya waumini wakiwa kanisani wakifuatilia kwa makini neno la Mungu na maombi katika ukumbi wa PTA jijini Dar es salaam,
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni