Imeonekana kuwa mauaji ya watu wenye ulemavu wa ngozi na
suala mauaji yanahusishwa na imani za
kishirikina huchangiwa kwa asilimia kubwa na waganga wa kienyeji.
kauli hiyo imetolewa na mwinjilisti wa kimataifa andulile
mbile wakati akielezea kuhisiana na mganga
wa kienyeji ambaye alisalimisha vifaa vyake vya kiganga kwake katika mkutano wa
injili ambao ulifanyika katika viwanja vya kisopwa jijini dar es salaam ambapo
amesema kuwa kwa asilimia kuwa mauaji ya watu wenye ulemavu wa ngozi
yanahusishwa na wanganga hao.
Aidha ameiomba serikali kuwa makini hasa wakati wa kutoa
vibali kwa waganga wa kienyeji na pia alizungumzia suala la uchanguzi ambao
unategewa kufanyika octoba mwaka na kuwaondoa hofu wananchi kuwa kutakuwepo na
amani wakati wa uchaguzi maana wananchi wengi mpaka sasa wanawaza sana juu ya
uchaguzi kuwa itakuwaje.
hizi ndizo zana za kiganga ambazo zimesalimishwa kwa mwinjilisti Andulile.
Mwinjilisti Andulile akikagua hivyo zana na kuanza kuchoma.
Hapa zoezi a kuzichoma moto limeanzaa
Ubatizo unaanza
Naye bwana jackson hakanya ambaye alikuwa mganga wa kienyeji na ameamua kusalimisha vifaa vyake na kukubali kubatizwa alisema kuwa kwa asilimia kubwa wagan ga wa kienyeji wanadanganya wanadamu wenzao maana kwa asilimia kuwa dawa hizo hazileti mafanikio kama inavyosadikiwa na wengi na kaka kutatokea mafanikio badao ni ya muda mfupi sana,hata hivyo aliamua kubatizwa
Baadhi ya waumini ambao walimpokea bwana Yesu kama Bwana na Mwokozi wa maisha yao na kukubali kubatizwa hapa zoezi la ubatizo likiendelea katika bahari ya Hindi
Baadhi ya waumini ambao walishiriki katika mkutano.
Katika mkutano huo ambao umefanyika kisobwa watu wengi
wamefunguliwa kutoka kwenye matatizo mbali mbali na kuamini na wengi wao
walibatizo.
wasiliana nasi kwa namba 0682672828.
wasiliana nasi kwa namba 0682672828.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni