Kanisa Katoliki nchini Burundi
limejiondoa katika mchakato mzima wa uchunguzi na uongozi wa aina yoyote katika
uchaguzi huo.
Rais Nkurunziza anapania kuwania
tena kiti cha urais kwa muhula wa tatu.
Uamuzi huo umekuja wakati ikisalia
wiki moja tu uchaguzi wa wabunge na madiwani ufanyike nchini humo
Kanisa katoliki ni kiungo muhimu
katika suala la amani na demokrasia nchini Burundi tokea kuanzishwa mazungumzo
ya amani ya Arusha mnamo miaka ya tisini.
EU inasema kuwa uamuzi wao
umeafikiwa kwa sababu ya sheria kali dhidi ya vyombo vya habari na waandamanaji
Haya yamearifiwa wakati maandamano
dhidi muhula wa tatu wa rais wa Burundi Pierre Nkurunziza yanaendelea kufanyika
katika mitaa kadhaa ya mji mkuu Bujumbura kwa zaidi ya mwezi mmoja sasa.
Wakati huohuo, Jumuia ya bara ulaya
imesimamisha ujumbe wake uliokuwa usimamie uchaguzi mkuu nchini Burundi.
EU inasema kuwa uamuzi huo
umeafikiwa kwa sababu ya sheria kali dhidi ya vyombo vya habari, matumizi ya
nguvu dhidi ya waandamanaji, na mazingara mabaya ya vitisho kwa vyama vya
upinzani.
Makundi ya kutetea haki za binadamu,
yanasema kuwa zaidi ya watu 20 wamefariki wakati wa ghasia za maandamano,
tangu rais Pierre Nkurunziza
alipotangaza mwezi uliopita kuwa anapania kuwania tena kiti cha urais kwa
muhula wa tatu, kinyume na katiba ya Burundi.
Uchaguzi wa urais umepangiwa
kufanyika Juni tarehe tano, huku ule wa urais ukiwa mwishoni mwa mwezi huo wa
Juni.
Sasa kama hali ni hii ni vyema mataifa ya kiafrika wajifunze na kuachia ngazi pale wanapoona kuwa usalama unayumba kwa sababu yao ili kuwaponya wananchi wasio na hatia kutokana na mabaya,pia wananchi watumie busaran maana kura ndiyo mwamuzi wa mwisho.
chanzo BBC,kama una maoni habari wasiliana nasi kwa namba 0682672828,
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni