YESU NI JIBU

Ijumaa, 8 Mei 2015

KATIBU MKUU KIONGOZI OMBENI SEFUE AKITHIBITISHA MBELE YA WAANDISHI WA HABARI KUSAINIWA KWA SHERIA TISA NA RAIS JAKAYA MRISHO KIKWETE KATIKA VIWANJA VYA IKULU JIJINI DAR ES SALAAM.



Licha ya wadau mbali mbali wakiwemo wadau wa Mambo ya Habari,wanasiasa pamoja na wanaharakati kumtaka Rais Jakaya Kikwete  asiusaini Mswaada wa Uhalifu wa Mitandao nchini wa Mwaka 2015  Hatimaye  Rais Kikwete amesaini Rasmi Mswaada huo. 
Akithibitisha kusainiwa kwa Mswaada huo na kuwa sheria rasmi   Sefue wakati wa mkutano na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, katibu mkuu kiongozi Ombeni amesema kuwa mswaada ukishatoka bungeni kwenda kwa rais tayari ni sheria akisaini inayofuta ni utekelezaji.
Aidha amesema kuwa rais ametia saini sheria ya tisa ambayo ni sheria ya ajira kwa watu ambao sio raia,sheria ya silaha, sheria ya marekebisho ya sheria ya risiti ghalani,sheria ya mfumo wa malipo nchini.
Hata hivyo ameongeza kuwa sheria nyingine ni Sheria ya marekebisho ya sheria ya tume ya ukimwi,sheria ya takwimu ,sheria ya baraza la vijana,sheria ya makosa ya kwenye mtandao na sheria ya miamala ya kielektroniki.

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni