Askari
wa FFU Njombe wakifungua barabara kuu ya Njombe - Iringa iliyofungwa kwa
kuchomwa mataili na waandamanaji
Viongozi wa Chadema Njombe wakivutana na polisi eneo la Kibena
Mmoja
wa majeruhi ambaye amejeruhiwa katika vurugu za FFU na Raia.
ASKARI wa
kikosi cha kutuliza ghasia (FFU) Njombe watumia mabomu ya
machozi kuwatawanya wananchi waliotaka kuchukua mwili wa
mwenzao anayedaiwa kuuwawa na polisi kuupeleka kituo cha
polisi .
Wakizungumzia
mtandao huu wa www.matukiodaima.co.tz juu ya vurugu hizo
baadhi ya wananchi walisema kuwa jana majira ya
saa 3 usiku askari wawili wakiwa na slaha walivamia
kilabu cha pombe za kienyeji kilichopo
eneo la Zenge mtaa wa Kambarage na kuwakamata wananchi wote
zaidi ya 20 waliokuwemo klabuni hapo na kuwaweka chini
ya ulinzi .
Hata hivyo
baada ya wananchi hoa kukamatwa wakiwemo wahudumu
inadaiwa polisi hao wawili waliovalia kininja kwa
kuziba sura zao walianza kuwapiga raia
walioonyesha kukaidi agizo la kutaka kutoa pesa
walizonazo kama faini ya kunywa pombe usiku huo.
Hivyo
kutokana na baadhi yao kushindwa kulipa adhabu hiyo akiwemo
kijana mmoja aliyetambuliwa jina la Bashir Mwalongo ambae ni
fundi ujenzi katika mji huo wa Njombe aliyekuwa
akitaka kutoka mlangoni hapo ndipo alipopigwa na kitu
kinachosadikika kuwa ni risasi tumboni na kufa
papo hapo
Mmoja kati ya
rai waliokamatwa na askari hao kwa kunywa
pombe usiku Bi Veronica Ng'ara alisema askari
hao walifika eneo hilo huku marehemu huyo akiwa
mlangoni kutoka kutoka nje na ndipo alipozuiliwa na kulazimishwa
kuingia ndani ya klabu hicho .
"Kabla
ya kufyatuliwa risasi kijana huyo alikuwa
amesimama mlangoni akitaka kutoka na ndipo askari
mmoja kati ya watatu waliofika eneo hilo kumpiga na
risasi ..... hawa watu sisi hatujui kama ni askari ama majambazi
kwani walikuwa wamejifunika usoni .... walipoona raia
tunamsaidia aliyepitwa risasi ndipo walipoanza kufyatua
risasi ovyo na kuingia katika gari na kukimbia ....tulipiga simu
kwa mkuu wa polisi usiku huo na yeye alikataa kuwatuma askari
hao ambao walikuja kutaka posho usiku huo "
Alisema askari
hao walilazimika kufyatua risasi za moto
ovyo klabuni hapo ili kuokoa maisha yao baada ya
wananchi kutaka kuwazingira kwa kosa la mauwaji .
Kuwa
kutokana na vurugu hizo jana usiku kwa wananchi hao
kuupeleka mwili wamarehemu huyo Hospitali ya wilaya ya
Njombe pamoja na majeruhi mmoja asubuhi ndipo wananchi
walipoandamana kwenda Hospitali hapo kuchukua mwili
huo ili kuupeleka kituo cha polisi .
Alisema wananchi
waligoma kuzika mwili huo na kutaka kuuchukua ili
kuupeleka polisi ili wao askari waliooa ndio wakauzike
.
Majeruhi
Lupiana Mandera ambae amelazwa katika Hospitali ya
wilaya ya Njombe alisema kuwa wakati vurugu hizo
zikiendelea nje ya Hospitali ya wilaya ya Njombe
kwa polisi wa FFU kutumia mabomu ya machozi kuwatawanya raia
zaidi ya 1000 walikuwa wameziba barabara kuu ya Njombe
- Ruvuma kwa kuchoma moto katikati ya barabara ndipo askari
walipomvamia na kumshambulia kwa virungu .
Alisema
kuwa kwa upande wake alikuwa akiwaonya vijana
waliokuwa wakichoma moto mataili barabarani kuachana na zoezi
hilo ndipo polisi walipomvamia na kumpiga katika kichwa
chake kabla ya kumjeruhi vibaya kichwani na mkononi .
Mama mdogo
wa marehemu Mwalongo anayedaiwa kuuwawa kwa
kupigwa risasi na polisi katika klabu cha pombe
Bi Regina Msemwa alisema kuwa alipigiwa simu
usiku kujulishwa juu ya tukio la kifo cha mtoto wake
huyo mdogo na asubuhi alifuatwa na kundi la watu
wakiwemo viongozi wa vyama vya siasa kumtaka kwenda kuchukua mwili
Hospitali ya Kibena ili kuupeleka kituo cha
polisi.
Alisema kuwa
kimsingi yeye alikuwa bado katika mazungumzo na ndugu mbali mbali
waliopo nje ya Njombe ili kupanga taratibu za mazishi ila
alifika katika Hospitali hiyo ya Njombe baada ya
kutakiwa na viongozi na wananchi kuungana nao katika
maandamano hayo.
Mwenyekiti
wa mtaa wa Kambarage Ally Mhagama ( Chadema) ambae alikuwepo
katika vurugu hizo katika Hospitali ya wilaya ya Njombe
alisema kuwa vurugu hizo zimeanzishwa na polisi
wenyewe baada ya kuzuia mwili kutolewa kwenda
kupeleka polisi .
Kwani
alisema wao kama viongozi walitaka
majeruhi mmoja ambae alipigwa risasa sehemu zake za siri
kutolewa Hospitali hapo na kupelekwa Hospitali ya Rufaa Mbeya
ama Iringa kwa ajili ya matibabu ila hakuna kilichofanyika juu ya
majeruhi huyo ambae alipigwa risasi pamoja na Marehemu
Mwalongo .
Hata hivyo
alisema kuwa anashangazwa na hatua ya polisi hao
kutumia nguvu kubwa kuwakamata wanywaji wa pombe na
kuwaacha waarifu .
Mhagama
alisema kuwa wao kama chama wanapowapongeza
wananchi waandamanaji ambao walifika kupinga
vitendo vya kionevu vya polisi na hata wananchi
hao kumchangia majeruhi huyo .
HIvyo
alisema wanachoomba ili kumaliza vurugu hizo ni polisi
na serikali kumpeleka Hospitali kubwa ya Rufaa majeruhi
hao pamoja na kuueleza umma jinsi ambavyo maiti hiyo
itakavyozikwa .
Mwandishi wa
habari hizi alishuhudia polisi wa FFU wakilazimika kuwatawanya
waandamanaji hao ambao walitaka kuandamana kutoka Hospitali ya
wilaya kwenda ofisi ya mkuu wa mkoa wa Njombe Dr Rehema Nchimbi
ili kufikisha malalamiko yao kabla ya kutawanywa kwa
mabomu .
Pia shughuli
mbali mbali zikiwemo za usafiri wa kutoka na kuingia mjini
Njombe kwa wasafiri wa mikoa ya Ruvuma , Mbeya , Iringa na
Dar es Salaam wakikama kwa muda huku magari yao
yakipigwa mawe na maduka kufungwa kwa zaidi ya masaa 3 baada
ya vurugu kuhamia katikati ya mji wa Njombe .
Barabara
kuu ya Njombe - Ruvuma na Iringa ya Njombe - Iringa na Njombe
- Makete zilifungwa na waandamanaji hao ambao walichoma
mataili kila kona kabla ya jeshi la polisi
kutumia mbinu zaidi kufungua barabara hizo.
Huku watu
kadhaa wakijeruhiwa kwa kupigwa mawe na waandamanaji hao na
wengine kupigwa na polisi wakati wa vurugu hizo
na baadhi yao kukamatwa kwa kuhusika na vurugu hizo.
Majira ya saa 7
mchana kamanda wa polisi mkoa wa Njombe alitaka kuzungumza na
wanahabari kuelezea hali hiyo ila hakuweza kufanya
hivyo kutokana na hali kuchafuka tena na hivyo kulazimika
kikao chake na viongozi wa Chadema Njombe kukatishwa na
wote na viongozi hao wa Chadema kuongozana mitaani kutuliza vurugu
hizo.
Hata hivyo
kamanda wa polisi wa mkoa wa Njombe alisema hawezi kugumza na
wanahabari hao kwa madai bado hali si shwari .
source:www.matukiodaima.co.tz
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni