Mamlaka ya Nepal imeomba msaada zaidi wa helikopta kutoka kwa mataifa ya kigeni baada ya nchi hiyo kukumbwa na tetemeko baya la ardhi ambapo zaidi ya watu elfu sita waliuawa.
Serikali imesema inahitaji ndege
hizo kusafirisha misaada ya dharura katika maeneo ya vijiji hususan maeneo ya
milimani.
Pia ndege hizo zitasaidia
kuwasafirisha majeruhi ili kupokea matibabu.
Kumekua na makabiliano miongoni mwa
manusura wanaong'angania usafiri mdogo ambao unatolewa na serikali.
Serikali pia
imetaka maiti zote kuzikwa punde baada ya kutolewa ndani ya vivusi.
Waziri wa
fedha wa Nepal , Ram Sharan Mahat, amesema nchi yake inahitaji dola bilioni
mbili kukarabati nchi hiyo ambayo miundo msingi yake imeharibiwa vibaya.Chanzo BBC,
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni