Licha ya wadau mbali mbali wakiwemo
wadau wa Mambo ya Habari,wanasiasa pamoja na wanaharakati kumtaka Rais Jakaya
Kikwete asiusaini Mswaada wa Uhalifu wa Mitandao nchini wa Mwaka
2015 Hatimaye Rais Kikwete amesaini Rasmi Mswaada huo.
Akithibitisha kusainiwa kwa Mswaada
huo na kuwa sheria Rasmi Waziri
wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia, Prof. Makame Mbarawa leo jijini Dar es Salaam, Wakati wa
Mkutano na Waandishi wa Habari ambapo amesema Baada ya Mswaada huo kupitia
sehemu mbalimbali na kuonekana hauna Tatizo lolote ndio ukamfanya Rais Kikwete
kusiani Mswaada huo.
Waziri Mbarawa alisema Sheria hiyo
itasaidia kupunguza makosa mbali mbali ya watu wanaofanya kwa makusudi
kwenye mtandao jambo ambalo anadai italiweka taifa salama na kuondokana na
tabia iliyojijengeka kwa baadhi ya watu kuandika habari na kusambaza taarifa za
upotoshaji kwenye mitandao ya kijamii.
Pamoja na hayo Waziri Mbarawa
amesema kwa sasa baada ya Rais Kikwete kusaini hatua inayofuata ni kazi ya Wizara
hiyo kuwaelimishwa wananchi kuijua sheria hiyo ili kuanza kutimika Rasmi.
Aidha,waziri huyo amesema kwa wale
wadau mbali mbali wa masuala ya habari na wanasiasa pamoja na wanaharakati
ambao walikuwa wanaubeza mswaada huo,wanatakiwa kuwasilisha hoja zao kwenye
wizara yake ili hatua zichukuliwe kwenye vipengele ambavyo wizara hiyo itaviona
labda vitakuwa na utata .
vilevile akawataka watanzania
kuipokea sheria hiyo kwa manufaa makubwa kutokana na uharifu wa mitandao
hivi sasa ambao ulikuwa unawasumbua.
Kusainiwa kwa msaada kunatafsiriwa
na wadau mbali mbali wa masuala ya habari nchini ni kama umeendelea kunyonga
uhuru wa habari nchini kutokana na sheria hiyo kuwepo na vifungu kandamizi kwa
watu wanaotoa taarifa kwa umma kwa njia ya mitandao.
Wadau mbali mbali wa masuala ya
habari waliokutana tarehe 2 ya mwezi huu mkoani morogoro siku ya vyombo vya
habari duniani walimtaka rais Kikwete kutosaini mswaada huo kwani utaiweka njia
panda taifa na wakadai uhuru wa habari unazidi wambwa msalabani kutokana
na vipengele vilivyopo kwenye sheria hiyo mpya.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni