ASKOFU Msaidizi wa Kanisa
Katoliki Jimbo la Bukoba, Mhashamu, Methodius Kilaini amewataka wanandoa nchini
kuwekeza katika ndoa zao ili kuweza kujenga familia imara.
Askofu
Kilaini alisema hayo katika misa ya pili iliyofanyika katika Kanisa Katoliki mjini
Bukoba ambapo alisema kuwa bila wanandoa kuwekeza katika ndoa zao, kamwe
hawawezi kujenga familia imara.
Alisema
Wakristo wanapaswa kujenga tabia ya uvumilivu, upendo, amani, kuthaminiana,
kuheshimiana katika familia pamoja na kuombana msamaha kila inapotokea nyufa
miongoni mwao.
“Katika
suala zima la ndoa inahitaji uvumilivu wa hali ya juu, muwe watu wa kuombana
msamaha pindi mmoja wenu anapokosea neno samahani, pole na aksante
inapokosekana katika familia zetu, familia haiwezi kuwa imara kwani kila mmoja
ataonekana ni mbabe,”alisema.
Alisema
ili baba aonekane ni mwenye nyumba anapaswa kufuata utaratibu na kuachana na
maisha ya mwanamume ambaye hajaoa kama vile kuwahi kurudi nyumbani si
kila siku kurejea nyumbani kuanzia saa moja hadi usiku wa manane.
“Ukimuoa
mwanamke si kwamba ni golikipa tu, iko siku atafungwa goli, kwani mlinda goli
hafungwi…. Kuna watu watakufunga tu, … naye ni binadamu hivyo si vizuri
baba mwenye nyumba kurudi kila siku usiku nyumbani,”alisema Askofu Kilaini.
Askofu
pia aliwaasa wanawake walioolewa kuwa na adabu kama wake za watu na si kuishi
kama wasichana ambao hawajaolewa.
“Katika
miaka ya nyuma ilikuwa rahisi kumtofautisha mwanamke aliyeolewa na msichana
ambaye bado anatafuta mchumba, lakini siku hizi kuna ugumu fulani, hivyo wanawake
mnapaswa kuishi kama mwanamke aliyeolewa pamoja na mavazi yenu,”alisema.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni