Maadhimisho ya miaka 54 ya Tanzania bara yameadhimishwa kwa kufanya usafi katika maeneo mbalimbali nchini yakiongozwa na rais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt John Pombe Magufuli ambapo alishiriki kufanya usafi katika maeneo ya Ferry na kuzungumza na wavuvi.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akiwa pamoja na Mama Janeth Magufuli wakielekea eneo la ufukwe wa Ferry kufanya usafi katika maadhimisho ya Siku ya Uhuru tarehe 9 Desemba.Rais Dkt. John Pombe Magufuli akiweka taka taka kwenye dastibin wakati akifanya zoezi la kufanya usafi
Rais Dkt. John Pombe Magufuli akiokota takataka
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli akizungumza na Wavuvi wa ferry huku akiwa ndani ya Mtumbwi. Rais Magufuli alizisikiliza kero zao na kuahidi kuzitatua ndani ya muda mfupi.
Rais Magufuli akifanya usafi pamoja na wavuvi wa eneo la
ferry waliojitokeza kuunga mkono zoezi hilo. Rais Magufuli amewataka Watanzania
kuwa na Utamaduni wa kufanya Usafi kila wakati ili kuweka mazingira katika hali
nzuri. PICHA ZOTE NA IKULU
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni