Mgombea Ubunge wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo - CHADEMA katika Jimbo la Arusha, GODBLEES LEMA ameibuka mshindi na kutangazwa kuwa mbunge mteule wa jimbo hilo.
Katika uchaguzi huo
ulioshirikisha vyama vitano vya siasa, LEMA amepata kura 68 ,848
kati ya kura 104,353 zilizopigwa akifuatiwa na mgombea wa Chama cha
Mapinduzi, PHILEMON MOLLEL aliyepata kura 35 ,907.
Wagombea
wengine walioshiriki katika uchaguzi huo ni
pamoja na NAVO MOLLEL wa ACT Wazalendo aliyepata kura
342, ZUBERI MWINYI wa Chama cha Wananchi -CUF-
aliyepata kura 106 na MAKAMA RASHIDI wa NRA
aliyepata kura 43.
Kwa mujibu wa
Msimamizi wa Uchaguzi wa Jimbo la Arusha, JUMA
IDDY,wapiga kura walioandishwa ni 317 814, na waliojitokeza kupiga
kura ni 105, 800.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni