I YOHANA 3:8.Jina la Bwana lihimidiwe milele nataka
kusema neno nawe japo kwa ufupi. Ni hivi hakuna ushirika wowote kati ya Mungu
na dhambi hakuna hata kidogo haijawahi kupokea na kamwe hatowahi kutokea milele
pamoja na kwamba siku za leo dhambi imeonekana kuwa ni kitu cha kawaida sana
lakini ukweli ni kwamba hiyo kawaida ipo kwa wanadamu tu lakini kwa Mungu bado
msimamo uko pale pale.
DHAMBI NI NINI?
Dhambi ni uasi dhidi ya sharia za Mungu =1YOHANA 3:4 mtu anapotaka kuijua
dhambi hana haja ya kuuliza uliza kwa watu hana haja ya kuuliza uliza kwa
Mtumishi yoyote yule kwasabu hata mtumishi anaweza kudanganya akataja dhambi
zisizomgusa yeye lakini dhambi inajulikakana kwa kuzijua sharia za Mungu hivyo
basi ili kuweza kujua kuwa dhambi ni nini ni lazima kupima kwa kutumia mmsheria
za Mungu kwa hiyo kitendo chochote au maneno yoyote yale yanayopinzana na
sharia za Mungu hayo ni Dhambi tena nasema kwa msisitizo chochote kile ambacho
hakiendi sawa na maagizo ya Mungu ni dhambi haijalishi ni nani anakisema au
kukifanya haijalishi ni Mtume Nabii Mchungaji Mwalimu Mwijilisti hicho sio
kigezo hata kidogo kigezo vyeo hivyo sio kipimo hata kidogo bali kipimo ni neno
la Mungu. Sasa basi hili ni jambo la muhimu sana kulijua kila mtu anapaswa
kujua hii awe Mkristo au mpagani anapaswa kujua hili kwamba kipimo sio mtume
wala nabii kipimo ni neno sasa dhambi ni kuasi maagizo ya Mungu.
Mtu yeyote yule anayefanya mambo kinyume na maagizo
ya Mungu huyo mtu NI MALI YA SHETANI haijalishi ataitwa kwa cheogani cha kiroho
haijalishi bado huyo mtu ni mali ya shetani na kwa kuwa yeye ni mali ya Shetani
ni wazi kabisa na wote wanaomsikiliza nao ni hivyo hivyo ni mali ya Shetani kwa
sababu maandiko yanena wazi wazi kuwa Atendaye dhambi ni wa ibilisi. Kutokana
na sababu hiyo mtu wa ibilisi atafanya mashauri ya ibilisi. na moyoni mwake
hakutatoka mambo mzuri bali siku zote atafanya mambo mabaya kwasabu moyo wake
umejaa mawazo mabaya tu.
ALIYEZALIWA NA MUNGU HATENDI DHAMBI =1YOHANA 5:18.
Aliyezaliwa na Mungu hatendi dhambi kwa sababu uzao wa Mungu unakaa ndani yake.
Hapa kuna kitu kikubwa sana cha kujifunza nacho ni hiki Kuna kuzaliwa na Mungu
na kuna kuzaliwa na shetani kwasabu kama Roho anasema aliyezaliwa na Mungu hatendi
dhambi basi bila shaka kabisa wapo waliyozaliwa na shetani hivyo kama kuzaliwa
na Mungu kupo basi na kuzaliwa na ibilisi nako kupo na kama. Aliyezaliwa na
Mungu hatendi dhambi basi ni wazi kabisa kuwa anayetenda dhambi amezaliwa na
shetani kwa hiyo Mtu yeyote ambaye ni Mwongo,
Tapeli,Mzinzi, Mwasherati,Muuaji, Mchonganishi, Mshirikina, Msoma nyota, Aliyeachana
na mume au mkewe na kuoa au kuolewa tena, Asiyelipa madeni, Aliyedhurumu Mali
za mjane na yatima, Mwabudu sanamu, Anayevaa mavazi yasiyoipasa jinsia yake, Anayejikoboa
ili kuusahihisha uumbaji wa Mungu, Muuzaji mafuta na maji ya upako, Muuzaji
sabuni na vitambaa vya upako, Mtume na nabii wa uongo, Mchungaji na Mwalimu wa
uongo, Anayeombea watu kwa kutoza pesa, Anayenunua mafuta na kingine chochote
cha upako kinachouzwa,
Na mengineyo yote yafananayo na hayo yoote
wanaoyatenda hayo ni watoto wa ibilisi ni UZAO WA SHETANI, na wote wapo njiani
kuelekea motoni.
TENGENEZA NA MUNGU SASA HIVI
Kama wewe uliyekutana na ujumbe huu ni unazo tabia kama hizo ujue hakika kabisa
wewe ni Mwana wa ibilisi na unahitaji kutengeneza na Mungu neema ya Mungu bado
ipo mlango wa neema haujafungwa bado unayo nafasi ya kutengeneza sasa basi tubu
leo
Kama wewe ni Mtumishi unayetapeli watu unajijua
kabisa kuwa bado hajaokoka bado kabisa tena huna wito bali umeingia kwa tamaa
na umesababisha kanisa kutukanwa mimi nakwambai kuna kifo kibaya cha aibu
hakipo mbali na wewe kabisa kama hautatubu leo unaenda kuaibika vibaya sana na
mbaya zaidi moto wa jehanam unakungoja wale funza wa jehanam wanasubiri nyama
yako utaponea wapi tubu leo tubu leo tubu leo sasa hivi mara moja na Yesu
atakusamehe na kufungua ukurasa mpya wa maisha yako.
Na kwako wewe ambaye bado hajaokoka unajijua
mwenyewe pamoja na kuwa na dini yako Kubwa mnasali kwenye hekalu kubwa lakini
unadhambi mwenyewe unajijua sasa basi nafasi ipo leo hebu fwatisha maneno haya
hapa Chini
SALA YA TOBA
Eee Bwana Yesu nimetambua kuwa mimi mimi ni mtu ninayeishi na dhambi moyoni
mwangu nakuomba leo unisamehe dhambi zangu zote unisafishe kwa Damu yako niwe
safi dhamiri yangu nazitubu dhambi zangu zoote kwa kumaanisha kuziacha kabisa,
sitozitenda tena namkataa kabisa Shetani na kazi zake zote na laana zake zote
na matatizo yake yote. Kuanzia leo nafanya agano na wewe Yesu kwa Damu yako ya
agano la milele, Ahsante kwa kunisamehe amina.
BAADA YA KUOKOKA
Baada ya kuokoka sio vema kuishia hapo
Bali unapaswa sasa kutafuta mafundisho ya neno la Mungu ni lazima upate mwalimu
mzuri mwaminifu atakayekulea kiroho hadi kufikia hatua ya kuweza kusimama
mwenyewe kwa miguu yako na kama unapenda kuwasiliana nami kwaajili ya kukujenga
zaidi kiroho
Nitafute kwenye WhatsApp kwa no hii hapa 0767 503054
YESU NI JIBU
Jumapili, 13 Desemba 2015
ATENDAYE DHAMBI NI WA IBILISI KWA KWA IBILISI HUTENDA DHAMBI TANGU MWANZO:
Imechapishwa na
Amaninafuraha
kwa
12:16
Tuma Hii kwa Barua pepe
Blogu Hii!
Shiriki kwenye Twitter
Shiriki kwenye Facebook
Shiriki kwenye Pinterest
Lebo:
Dhambi
,
kuokoka
,
kutubu
,
mtumishi Likuta
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni