Mahakama ya juu zaidi Korea Kaskazini
imemhukumu mhubiri kutoka Canada kifungo cha maisha jela na kazi ngumu.
Hyeon Soo Lim, 60, aliyekamatwa mjini
Pyongyang baada ya kuzuru taifa hilo Januari kwa kazi ya kibinadamu amehukumiwa
kwa makosa ya “uhalifu dhidi ya dola.”
Bw Lim, ambaye ni kiongozi wa Light
Korean Presbyterian Church, alikuwa ameenda kusaidia kituo cha kutunza
wagonjwa, kituo cha kuwatunza watoto na kituo cha kutunza mayatima.
Mhubiri huyo kutoka Korea, anadaiwa
kukiri kuhusika katika njama ya kupanga kupindua serikali na kuunda taifa la
kidini.
Shughuli zozote za kidini ni marufuku
nchini Korea Kaskazini.
Taifa hilo mara kwa mara huwakamata na
kuwazuia wageni wanaoenda huko kwa shughuli za kidini au kimishenari.
Bw Lim alihukumiwa baada ya kesi yake
kuendeshwa kwa muda mfupi na mahakama ya juu ya Korea Kaskazini.
Inadaiwa mhubiri huyo amekiri kutoa
mihadhara na kusema “Korea Kaskazini inafaa kusambaratishwa na mapenzi ya
Mungu”, na kusaidia Marekani na Korea Kusini kutoa usaidizi kwa wanaotoroka
Korea Kaskazini.
Chanzo BBC,
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni