Kumaliza mwaka sio tu kubadilisha namba
ya mwaka toka 2015 kwenda 2016. Kubadilisha namba hakuleti mabadiliko yoyote
zaidi ya kubadili namba tu.
Na wala kumaliza mwaka hakuna maana ya kubadilika
kwa mazingira toka kwenye uchakavu kwenda kwenye upya. Wala kubadili mwaka sio
kuondoa changamoto za maisha ulizokuwa nazo na kuingia kwenye maisha raha bila
masumbufu yoyote ya maisha.
Kimsingi, kumaliza mwaka kwa maneno tu
kwamba tumemaliza mwaka hakuna mabadiliko yoyote yenyewe kuhusiana na
mabadiliko ya mwaka. Tena unaweza kushangaa kwamba, unamaliza mwaka ukiwa
katika hali nzuri na unapoanza mwaka mpya unauanza kwa mabalaa na majanga
utadhani ni mwaka ndio una nuksi.
Kama haya yote hayana maana ya kumaliza
mwaka, je ni kwanini suala la kumaliza mwaka linagusa sana hisia za watu wengi
kila mahali duniani? Kwanini kumaliza mwaka kunasherehekewa kana kwamba kuna
kitu watu wanapata wanaposherehekea? Kusema kweli ziko sababu mbali mbali zinazowasukuma
watu kutoa uzito kwa sualala kumaliza mwaka nitazitajaa baadhi hapa chini.
Uzito
wa kumaliza mwaka
uko
kwenye sababu za kiibada
Ushahidi wa kihistoria unaonesha kwamba
suala zima la kuadhimisha kumaliza mwaka na kuanza mwaka mpya zimebeba uzito wa
shughuli za kiibada iwe kwa Mungu wa kweli au miungu/mizimu ya ukoo. Ndiyo
maana waabudu mashetani/mizimu lazima waende makwao kutambika.
Kundi la watu waabuduo mashetani na
mizimu wanapomaliza mwaka ibada zao kwa mashetani pasipo wao kujua huwapunguzia
umri wa kuishi na kujiweka tayari kwa maisha ya nuksi na laana ya maisha ya
kipindi cha miezi 12 ya mwaka unaofuata.
“..Yaliyokuwako ndiyo yatakayokuwako;
na yaliyotendeka ndiyo yatakayotendeka; wala jambo jipya hakuna chini ya jua.
Je! Kuna jambo lo lote ambalo watu husema juu yake, tazama ni jambo jipya?
Limekwisha kuwako, tangu zamani za kale zilizokuwa kabla yetu sisi” (MH.1:9)
Kwa kadri mtu asiyemcha Mungu
anavyozidi kuishi duniani mwelekeo wake ni kumaliza vibaya na kuishi kwenye
uangamivu wa kutisha kwa sababu ya maisha ya uovu aliyotumikia akiwa hai
duniani:“Ndivyo ulivyo mwisho wa hao wamsahauo Mungu; na matumaini yake
huyo mbaya huangamia.” (Ayb.8:13)
Kumaliza mwaka pamoja
na
Mungu huzalisha jambo
jipya
Kama
tulivyokwisha kupitia hapo juu ya kwamba, kutokumcha Mungu kunazalisha balaa
zaidi, na hakuna jambo jipya kwa wasiomcha Mungu! Sasa tunapokuja kwenye kundi
la wachaji Mungu mambo ni tofauti kabisa. Hapa tofauti tena haiko tu kwenye
kumaliza mwaka mmoja na kuingia katika mwaka mwingine; bali ni jinsi
tunavyomaliza mwaka tukiwa na mahusiano chanya na Mungu kiimani.
Hii ni kwa
sababu Mungu mwenyewe ndiye mwenye kufanya jambo jipya kwa hao wamchao ili
kudhihirisha kwamba wao pia ni watu tofauti chini ya jua. “Tazama
nitatenda eno jipya; sasa litachipuka; je hamtalijua sasa? Nitafanya njia hata jangwani, na mito ya maji nyikani.”
(Isa.43:19)
Kimsingi, kwa wachaji Mungu kwao
kumaliza mwaka ni kufikia kilele cha utumishi kwa Mungu na wanawajibika kufanya
ibada kwa fursa waliyopewa na Mungu kumtukuza katika maisha mafupi hapa
duniani. Na wanapofanya ibada ya shukrani ya kumaliza mwaka wanajiweka wakfu
kwa fursa nyingine ya kipindi cha miezi 12 ya utumishi mpya.“Tazama
nitatenda neno jipya; sasa litachipuka; je hamtalijua sasa? Nitafanya njia hata
jangwani, na mito ya maji nyikani.”
(Isa.43:19)
Mwisho wake mchaji Mungu ni tofauti
kabisa. Maandiko yanasimulia kwamba, Mungu anamuwazia amani na tumaini afikiapo
mwisho wa kuwepo kwake duniani.“Ninajua mawazo ninayo wawazia ninyi,
asema BWANA ni mawazo ya amani wala si ya mabaya, kuwapa ninyi tumaini siku
zenu za mwisho.” (29:11)
Vitu ambavyo havina
maana ya kumaliza mwaka
Kumaliza mwaka sio tu kubadilisha namba
ya mwaka toka 2015 kwenda 2016. Kubadilisha namba hakuleti mabadiliko yoyote
zaidi ya kubadili namba tu.
Na wala kumaliza mwaka hakuna maana ya
kubadilika kwa mazingira toka kwenye uchakavu kwenda kwenye upya. Wala kubadili mwaka
sio kuondoa changamoto za maisha ulizokuwa nazo na kuingia kwenye maisha raha
bila masumbufu yoyote ya maisha.
Kimsingi, kumaliza mwaka kwa maneno tu
kwamba tumemaliza mwaka hakuna mabadiliko yoyote yenyewe kuhusiana na
mabadiliko ya mwaka. Tena unaweza kushangaa kwamba, unamaliza mwaka ukiwa
katika hali nzuri na unapoanza mwaka mpya unauanza kwa mabalaa na majanga
utadhani ni mwaka ndio una nuksi.
Kama haya yote hayana maana ya kumaliza
mwaka, je ni kwanini suala la kumaliza mwaka linagusa sana hisia za watu wengi
kila mahali duniani? Kwanini kumaliza mwaka kunasherehekewa kana kwamba kuna
kitu watu wanapata wanaposherehekea? Kusema kweli ziko sababu mbali mbali
zinazowasukuma watu kutoa uzito kwa sualala kumaliza mwaka nitazitajaa baadhi
hapa chini.
Uzito wa
kumaliza mwaka
uko kwenye
sababu za kiibada
Ushahidi wa kihistoria unaonesha kwamba
suala zima la kuadhimisha kumaliza mwaka na kuanza mwaka mpya zimebeba uzito wa
shughuli za kiibada iwe kwa Mungu wa kweli au miungu/mizimu ya ukoo. Ndiyo
maana waabudu mashetani/mizimu lazima waende makwao kutambika.
Kundi la watu waabuduo mashetani na
mizimu wanapomaliza mwaka ibada zao kwa mashetani pasipo wao kujua huwapunguzia
umri wa kuishi na kujiweka tayari kwa maisha ya nuksi na laana ya maisha ya
kipindi cha miezi 12 ya mwaka unaofuata.
“..Yaliyokuwako ndiyo yatakayokuwako;
na yaliyotendeka ndiyo yatakayotendeka; wala jambo jipya hakuna chini ya jua.
Je! Kuna jambo lo lote ambalo watu husema juu yake, tazama ni jambo jipya?
Limekwisha kuwako, tangu zamani za kale zilizokuwa kabla yetu sisi” (MH.1:9)
Kwa kadri mtu asiyemcha Mungu
anavyozidi kuishi duniani mwelekeo wake ni kumaliza vibaya na kuishi kwenye
uangamivu wa kutisha kwa sababu ya maisha ya uovu aliyotumikia akiwa hai
duniani:“Ndivyo ulivyo mwisho wa hao wamsahauo Mungu; na matumaini yake
huyo mbaya huangamia.” (Ayb.8:13)
Kumaliza mwaka pamoja na
Mungu huzalisha jambo jipya
Kama
tulivyokwisha kupitia hapo juu ya kwamba, kutokumcha Mungu kunazalisha balaa
zaidi, na hakuna jambo jipya kwa wasiomcha Mungu! Sasa tunapokuja kwenye kundi
la wachaji Mungu mambo ni tofauti kabisa. Hapa tofauti tena haiko tu kwenye
kumaliza mwaka mmoja na kuingia katika mwaka mwingine; bali ni jinsi tunavyomaliza
mwaka tukiwa na mahusiano chanya na Mungu kiimani.
Hii ni kwa
sababu Mungu mwenyewe ndiye mwenye kufanya jambo jipya kwa hao wamchao ili
kudhihirisha kwamba wao pia ni watu tofauti chini ya jua. “Tazama
nitatenda eno jipya; sasa litachipuka; je hamtalijua sasa? Nitafanya njia hata jangwani, na mito ya maji nyikani.”
(Isa.43:19)
Kimsingi, kwa wachaji Mungu kwao
kumaliza mwaka ni kufikia kilele cha utumishi kwa Mungu na wanawajibika kufanya
ibada kwa fursa waliyopewa na Mungu kumtukuza katika maisha mafupi hapa
duniani. Na wanapofanya ibada ya shukrani ya kumaliza mwaka wanajiweka wakfu
kwa fursa nyingine ya kipindi cha miezi 12 ya utumishi mpya.“Tazama
nitatenda neno jipya; sasa litachipuka; je hamtalijua sasa? Nitafanya njia hata
jangwani, na mito ya maji nyikani.”
(Isa.43:19)
Mwisho wake mchaji Mungu ni tofauti
kabisa. Maandiko yanasimulia kwamba, Mungu anamuwazia amani na tumaini afikiapo
mwisho wa kuwepo kwake duniani.“Ninajua mawazo ninayo wawazia ninyi,
asema BWANA ni mawazo ya amani wala si ya mabaya, kuwapa ninyi tumaini siku
zenu za mwisho.” (29:11)
mwisho
- See more at: http://www.gospelkitaa.co.tz/2015/12/hoja-nini-maana-ya-kumaliza-mwaka.html#sthash.PsFuMNz4.dpuf
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni