YESU NI JIBU

Alhamisi, 2 Aprili 2015

WAKRISTO WAITAADHARISHA SERIKALI KUTOWATENGANISHA AMA KUWAGAWA WATANZANIA KWA KULETA VITU VINAVYOWEZA KUWATENGANISA.





Waumini wa dini ya kikristo katika mkoa wa mtwara wameitaadharisha serikali isiwe chanzo cha kuleta mpasuko kwa wananchi wanaowatawala kwa kulazimisha mambo yanayoweza kuleta mpasuko dhidi yao.
Kauli hiyo imetolewa na baadhi ya waumini wa kanisa la Anglikana baada ya tamko la jukwaa la wakristoTanzania kuhusu katiba inayopendekezwa, mahakama ya kadhi na hali ya usalama nchini kusomwa katika ibada maalumu ya siku ya matawi hali iliyofanya baadhi ya waumini kupaza sauti zao na kutaka serikali kuwa sehemu ya kusimamia amani na si vinginevyo.

Wakizungumza na ITV baadhi ya waumini wa kanisa hilo wameendelea kupinga mahakama ya kadhi kuingizwa kwenye katiba ya nchi na wengine wakiizungumzia katiba pendekezwa.

Akisomesha ibada maalumu ya siku ya matawi askofu mkuu wa dayosisi ya Newala Oscar Mnung’a ambaye pia ni makamu mwenyekiti wa askofu mkuu wa kanisa la AngAlikana Tanzania  amesema jukwaa hilo mara kadhaa limeishauri serikali lakini matokeo yake ni haya.

Akiwa mgeni rasmi katika mkutano wa kamati ya amani ya mkoa wa Dar es salaam uliyoshirikisha viongozi wa dini ya kikristo na kiislamu amesema msimamo wa jukwaa la wakristo Tanzania la kuipigia kura ya hapana katiba inayopendekezwa ni hasira zisizo kuwa na tija kwa maendeleo ya taifa.




Hakuna maoni :

Chapisha Maoni