Tanzania ni miongoni mwa nchi zinazotegemewa kushiriki mbio za Kigali Marathon zitakazofanyika May 23-24, ambapo nchi kadhaa zikialikwa kushiriki.
Michuano hiyo itakuwa ni ya wazi ya
kimataifa, kama yalivyo ya Kilimanjaro Marathon yanayofanyika kila mwaka nchini
Tanzania huku wakimbiaji kutoka nchi mbalimbali kama vile Kenya wakishiriki.
Kwa mujibu wa waandaaji, chama cha
riadha nchini Rwanda (RAF), mbio hizo za Kigali pia zitakuwa na msisitizo wa
kudumisha amani kupitia michezo.wakimbiaji watashindana katika mbio ndefu
(kilometa 42) na half marathon (kilometa 21) kwa upande wa wanawake na wanaume.
Mbio hizo zitaanza uwanja wa Amahoro.
Wanariadha wengi kwa sasa wapo
katika matayarisho na mashindano mbalimbali yakiwemo ya Olimpiki
yatakayofanyika Rio de Janeiro, Brazil mwaka 2016.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni