Rais Uhuru Kenyatta aliwaandikia barua kila familia iliyopoteza mpendwa wao.
Wote walioathirika walipewa shilingi laki moja za Kenya,Jeneza na gari la kusafirishia maiti hadi kwao.
Familia za wanafunzi 142 kati ya watu 148 waliouawa katika shambulizi la kundi la wapiganaji wa Kiislamu Al Shabaab katika chuo kikuu cha Garissa wameruhusiwa kuchukua miili ya wapendwa wao.
Familia zimeanza harakati za safari
ya mwisho ya wapendwa wao baada ya serikali ya Kenya kuwaruhusu kuzichukua
miili kutoka kwenye hifadhi ya maiti ya Chiromo jijini Nairobi.
Misa ya wafu huko Garissa
Shambulizi lilipokuwa likiendelea,
Takriban wanamgambo 5 wa kundi la
wapiganaji wa Kiislamu Al Shabaab washambulia chuo kikuu cha Garissa alfajiri.
Waliwapata wanafunzi wakiwa
wamelala.
Waliingia chuoni baada ya kuua
walinzi wawili langoni.
Walionusurika wanasema kuwa wavamizi
hao waliwabagua wanafunzi waislamu na kuwaua wakristo.
Waziri wa usalama wa taifa generali
mstaafu Joseph Nkaissery alitangaza idadi ya waliouawa kuwa ni 148 na kusema
kuwa operesheni ilikuwa imekamilika.
Wanafunzi 500 wameokolewa na maafisa
wa usalama
Rais Uhuru Kenyatta ahutubia taifa
na kutuma risala za rambirambi kwa wale waliouawa.
Serikali ilionyesha hadharani miili
ya wanamgambo waliouawa na kuonyesha picha ya raia mmoja kutoka Tanzania
aliyekamatwa.
Jamaa ya walioathirika,
Rais Uhuru Kenyatta atangaza kuwa
Serikali yake itachukua hatua kali dhidi ya wakenya wanaolisaidia Al Shabaab.
Serikali yakiri kuwa mmoja kati ya
washambuliaji hao alikuwa ni mwanawe Chifu wa kata ya Mandera.
Chifu huyo yamkini alikuwa ameripoti
kwa polisi kuhusu kutoweka kwake mwaka uliopita.
Maswali yaibuka kuhusu hatua
zilizochukuliwa na polisi baada ya kuarifiwa kuhusu shambulizi hilo.
Wananchi waizomea serikali kwa
kutumia ndege kuwasafirisha waziri wa usalama wa taifa Joseph Nkaissery na
Inspekta mkuu wa polisi Joseph Boinett
huku kikosi maalum cha kupambana na
magaidi al maarufu (RECCE) kikilazimika kusafiri kwa gari kwa zaidi ya saa
saba.
Wanafunzi walionusurika,
Kikosi hicho kilitumia chini ya
dakika 15 pekee kukamilisha operesheni hiyo.
Raia wa Kenya Mohamed Kuno kwa jina
jingine Mohamed Dulyadin,atajwa kuwa ndiye mshukiwa mkuu.
Serikali ya Kenya imetoa ruzuku ya
shilingi milioni 20 za Kenya yaani dola $215,000 za kimarekani.
Kuno aliwahi kuwa mwalimu katika
eneo la Garissa kabla ya kustaafu na kujiunga na kundi hilo.
Mwengine aliyetajwa ni wakili
Abdirahim Abdullahi aliyeongoza uvamizi huo.
Manusura waliopatikana wamelala,
Maiti ya wahanga wa mauaji hayo
yaletwa mjini Nairobi kwa ndege za kijeshi.
Wale walionusurika pia wasafirishwa
kwa msafara wa mabasi hadi mjini Nairobi.
Kituo cha kuwapokea waathiriwa wa
mauaji hayo na jamaa zao kinaundwa katika uwanja wa michezo wa Nyayo mjini
Nairobi.
Wale walionusurika pia wasafirishwa
kwa msafara wa mabasi hadi mjini Nairobi
Orodha ya wanafunzi waliouawa na
wale waliojeruhiwa inapachikwa katika lango la uwanja wa Nyayo.
Serikali yatangaza orodha
ya mashirika kumi na tatu na akaunti za watu binafsi wapatao 86 wanaoshukiwa
kuhusika na ufadhili wa kundi la kigaidi la Al Shabaab Garissa.
Akaunti za watu hao ambao
zimesitishwa ni baadhi ya watu waliokuwa katika orodha ya serikali ya Kenya
ambao walikuwa wakifuatiliwa mienendo yao.
kampuni 13 za ubadilishaji na
usafirishaji wa fedha nazo zimefungwa.
Maafisa wa Polisi wakishika doria,
Jamii ya wasomali yalalamikia hatua
hiyo ikisema ni mtego ambao umenasa waliokuwemo na wasiokuwemo.
Shughuli ya utambuaji wa maiti
yaanza huku familia nyingi zikitatizika kutambua miili ya wapendwa wao kufuatia
kuharibiwa kabisa kwa miili.
Mmoja wa wanandugu ambaye amefika kutambua mwili akilia kwa uchungu.
Serikali ya Kenya yalazimika kutumia
mashine maalum ya kutambua chembechembe za damu za DNA ili kuharakisha utambuzi
wa miili.
Dukuduku zaibuka kuhusiana na kuwepo
kwa idadi kubwa ya wazazi ambao wamekosa miili ya wapendwa wao.
Muungano wa walimu na wafanyakazi wa
vyuo vikuu (UASU) yadai kuwa takriban wanafunzi 166 hawajulikani waliko.
Source BBC,
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni