YESU NI JIBU

Jumamosi, 11 Aprili 2015

IFAHAMU BIBLIA YAKO NA UJIFUNZE KUFAHAMU MAMBO MENGII JUU YA BIBLIA,

1.Toa maana sita za rafiki wa kweli kwa mfumo wa kiblia ni nani?
answer:
1. Rafiki ni mtu anayekupenda (yohana15:12)
2.ni mtu aliyetayari kujitoa maisha kwa ajili ya marafiki zake(yohana 15 :13) Yesu pia alionesha hilo kwa kutufia msalabani (rumi 5:8)
3.ni mtu ambaye yupo tayari kukutendea lile jema utakalomwomba akutendee (yohana 15:14)
4. ni mtu anayehusika na kushirikiana nawe(yohana15:15)
maombezi ,mafundisho na makemeo ya urafikiYesu anainua ,kuponya na kuadibisha.
5.ni yule anayejitolea kwa hiari kudumisha urafiki uliopo(yohana 16:16)
kujitoa kwa  moyo wa hiari kulinda kudumisha uhusiano wa kirafiki(yoh 7:17)
6.ni yule ambaye anaendelea  kuchagua kuwa  rafiki wakati wengine wote wanajitenga na kukimbia kwa sababu mbalimba(yoh15:17)

2.Kuabudu maana yake ni nini?
Answer:Ni tendo linalogusa akili,hisia,nafsi na utu wa mtu na mwili pia kwa kusujudu,kuanguka kifudifudi,au uso kwa uso.
Mwanzo 17:3
Kuabudu katika Roho na Kweli kunaweza kukafanywa wakati wowote na mahali popote mradi lengo ni kufanyia Mungu Ibada.
3.Kuna aina ngapi za hekima zitaje
1.Hekima za kibinadamu ambayo wakati mwingine hujulikana kama hekima ya dunia
  mathayo 11:25,1korintho 1:20.
2.Hekima ya kishetani   ezekieli 28:17
3.Hekima ya Mungu  Daniel 2:23, 2timotheo 3:15

Hakuna maoni :

Chapisha Maoni