Wakizungumza jijini Dar es Salaam na
vyombo vya habari, maaskofu na wachungaji kutoka makanisa mbalimbali, licha ya
kukataa kusema walichozungumza na mkuu wa jeshi la polisi nchini, wamewataka
wakristo kote nchini kuwa katika hali ya utulivu huku wakiendelea kuenzi tunu
ya amani iliyopo hapa nchini wakati vyombo vya sheria vikiendelea kushughulikia
sakata hili la askofu Josephat Gwajima.
Wakizungumzia kauli ya askofu
Gwajima aliyotamka kwa vyombo vya habari wakati akitoka kuhojiwa katika kituo
cha polisi cha Osterbay jijini Dar es Salaam kuhusu kusimamia kauli zake,
maaskofu hao wamesema kwamba askofu Gwajima hawawezi kusaliti kauli iliyotolewa
na jukwaa la waakristo Tanzania na akifanya hivyo hata wao watamshangaa na ndio
maana askofu Gwajima aliwaambia waandishi wa habari kwamba yeye kama mtumishi
wa mungu lazima akemee jambo analoona haliendi sawa.
Maaskofu hao na wachungaji
wamempongeza kwa dhati askofu mkuu wa jimbo kuu la Dar es Salaam Cadinali
Polcarp Pengo kwa kutangaza kusamehe yote yaliyotokea kati yake na askofu
Josephat Gwajima kwani kwa kufanya hivyo ndio ukristo wa kweli.
Cadinali
Polcarp Pengo
Waumini wa askofu Gwajima wakiandamana kuelekea osterbey.
Mwenyekiti wa chama cha CUF Profesa Ibrahim Lipumba akimjulia hali Askofu Gwajima.
Mch. Kiongozi Dr. Anny Fernandes alipomtembelea hospitalini Askofu Gwajima.
Waumini wa huduma ya ufufio na uzima wakimuaga askofu wao baada ya kutoka kituo cha polisi cha Osterbey.
Hakuna maoni :
Chapisha Maoni